Posts

Showing posts from July, 2022

KIRARE BADO AISOTEA RUMANDE

Image
  FATMA HAMAD PEMBA. Mahakama ya mkoa B iliopo Kusini Pemba imeghairisha kesi ya kuingilia kinyume na maumbile inayomkabili kijana Khamis Abdala Khamis marufu kirare mwenye umri wa [20] mkaazi wa Kangani wilaya ya Mkoani baada ya mtuhumiwa huyo kukataa kusomewa shitaka lake . Kijana huyo wakati akiwa ametulia kizimbani na kusubiri asomewe shitaka lake aliambia mahakama hiyo kuwa hali yake sio mzuri anaomba kesi ighairishwe na ipangiwe siku nyengine. ‘’Mheshimiwa hakimu leo naumwa siwezi kukakaa hivyo naiomba mahakama yako ighairishe shauri hilo kwa leo’’ alieleza mtuhumiwa kirare. Hakimu wa mahakama hiyo Muumin Ali Juma   amesema hii ni mara ya pili unasema unaumwa   daktari anakuja na kurudi ila ujue baadae fursa hii hutoipata tena nitakua sikusikilizi tena , na mahakama itatoa oda ya kumruhusu daktari afanye shughuli zake mpaka utakapo kuwa tayari   ndio tutamleta na wewe   utarudi rumande hadi tarehe 9/ 8 2022kwa ajili ya kusikiliza mashahidi. Mtuhumiwa h

AFUNGWA JELA KWA KUTOROSHA MSICHANA

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Hatimae kijana  Ramadhan Khamis Mohd  mwenye umri wa miaka 19 mkazi wa Tironi  Mkoani Pemba  anza  maisha  mapya  ya kutumikia chuo cha Mafunzo kwa muda  wa miaka 5 baada ya kutiwa  hatiani  kwa kosa  la  kutorosha  msichana  wa  miaka  16. Baada ya kijana huyo kupanda kizimbani na kusubiri asomewe hukumu yake Mwendesha mashtaka  wa Serikali Mussa Khamis amemuambia  hakimu anaendesha kesi hiyo kuwa kesi iko kwa ajili ya kutolewa uwamuzi hivyo wao hawana pingamizi kama mtuhumiwa yuko tayari basi asomewe huku yake. ‘’Kama mtuhumiwa yuko tayari basi na sisi hatuna tatizo nivyema  asomewe hukumu yake ili ajue hatma yake’’ alieleza  DPP Mussa. Hakimu wa mahakama ya mkoa B  iliyopo Chake chake  Muumin  Ali Juma   alisema jumla ya mashahidi 4 walisikilizwa mahakamani hapo akiwemo muathirika mwenyewe na Mahakama imemtia hatiani mtuhumiwa huyo. Hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 113 [1] [a] cha sharia ya adhabu namba  6  na  kifungu  cha  299  cha sharia  ya mwenendo wa mak

ALIEDAIWA KUWA NI BUBU SASA AANZA KUSEMA

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Hatimae  Mahakama  ya  mkoa  B  Wete  yanza kusikiliza kesi ya ulawiti inayomkabili kijana  Nuhu Kombo Nuhu  miaka 19  mkaazi wa Kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba. Mwendesha mashtaka wa Serikali Juma Mussa Omar amemuambia hakimu anaendesha  kesi hiyo kuwa shauri hilo lipo kwa ajili ya kusikilizwa na tulikua tunasubiri  cheti  kutoka kwa mtaalamu wa Afya kuthibitisha kwamba kijana huyo ni mgonjwa hawezi kuzunguza  ama ni kiziwi. ‘’Mheshimiwa hakimu tulitoa ombi  mahakama yako impeleke  hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi  kama tayari basi tupo tayari kwa ajili ya kuskila’’ alisema DPP Juma. Hakimu wa  Mahakama hiyo Abdulrahman  Ali  ameleza  kuwa  tayari tumesha pokea uthibitisho kutoka  Hospitali na majibu hayakuonesha  kwamba  mtuhumiwa  huyo  ana  ugonjwa wowote. ‘’Majibu yanaonesha kwamba si kibubu wala kiziwi anazungumza hivyo naighairisha hadi tarehe 25/7   na mashahidi waitwe tuanze kuwasikiliza’’  alieleza hakimu Abdulrahman. Tu

NUHU AENDELEA KULA BATA RUMANDE

Image
  NA FATMA HAMAD Pemba.  Mahakama   ya mkoa   B iliyopo   Wete   imeghairisha   shauri   la   Ulawiti   linalo mkabili   kijana   Nuhu Kombo   Nuhu   mwenye   umri   wa   miaka 19   mkazi   wa   Kijichame   wilaya   ya   Micheweni   Mkoa   wa Kaskazini   Pemba baada ya mtuhumiwa kudai   kuwa anaumwa na homa. Mtuhumiwa huyo     ameiambia mahakama hiyo kuwa hajisikii vizuri anaumwa hivyo anaiomba   kughairisha shauri hilo na apangiwe siku nyengine kwa ajili ya kusikilizwa. Mwenedesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Mussa Omar   amewambia mashahidi waliofika kwa ajili ya kutoa   ushahidi   wao kwamba mtuhumiwa leyo kasema anaumwa hivyo tukiendelea   tutakua tunamnyima haki yake . ‘’Kwa vile mtuhumiwa kasema hayuko vizuri nawaomba murudi na musichoke muje tena siku mutakayoitwa’’ alieleza DPP Juma. Hakimu wa mahakama hiyo amekubaliana na ombi hilo nan a kusema kuwa mtuhumiwa   atarudi rumande hadi siku ya tarehe 3/ 8/ 2022 kwa ajili ya kusikil

WEZI WA KARAFUU WATAKIONA MKUU WA MKOA ASEMA

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Serikali ya mkoa wa Kaskazini Pemba kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama   mkoani humo imesema hawatomvumilia mtu yoyote atakaefanya   vitendo vya   uhujumu    wa zao   la karafuu katika msimu   wa mwaka huu. Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya micheweni Mgeni Khatib Yahya   kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Kaskazini pemba Salama Mbarouk Khatibu   mbele ya Masheha pamoja na wakulima wa   karafuu mkoa huo   huko jamuhuri Holl Wete Pemba. Amesema   wakati wa msimu wa karafuu   wapo watu   wanafanya ubabaishaji ikiwemo ununuaji   karafuu za vikombe   pamoja na uzwaji   wa karafuu chafu katika vituo vya ZSTC. ‘’Niwambie wezee wenzangu haipendezi kuonekana kwamba karafuu inanunuliwa na mchanganyiko wa uchafu tunaona aibu kama sisi viongozi, hivyo kwa msimu huu hatutokua tayari kuliona hilo tutahakikisha tumewafichua wote watakaofanya hivyo’’ alieleza mkuu wa mkoa. Wakitoa changamoto   ambazo zimekua   zikiwaumiza   wakulima hao ni kuzuka kwa wizi na uk

WAKULIMA WA KARAFUU MKOANI PEMBA WA NENA.

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wakulima wa zao la karafuu  wilaya ya Mkoani wameliomba shirika  la biashara la ZSTC  kuweka mikakati madhubuti  ili waweze kuwadhibiti wale wote  wanao jishuhulisha na biashara ya  ununuzi wa  karafuu   mbichi.  Wamesema uwepo wa watu wanao nunua karafuu mbichi za vikombe ni moja  ya sababu kubwa inayochangia  ongezeko la wizi  wa  zao hilo. Ushauri huo wameutoa katika mkutano wa  tathmini juu ya zao la karafuu katika msimu  wa mwaka huu huko Zstc Mkoani wamesema asilimia kubwa ya wanaoiba karafuu wanaziuza kwa wale wanao nunua karafu za vikombe, hivyo ni vyema watendaji wa Zstc kuwa makini na watu hao ili kuepusha uharibifu, pamoja na wizi  katika msimu wa mwaka huu. ‘’Mheshimiwa mkuu wa mkoa kweli tunaumizwa tunaibiwa karafuu zetu na hawa wanunuzi wa karafuu za vikombe ndio wanaosababisha tunaomba hilo mliangalie’’ walieleza wakulima. Kwa upande wake mkulima Zubeir Mohd Said amesema  sababu inayowapelekea wakulima kuuza karafuu mbichi ni ule uchelewes

MTUHUMIWA AKATAA SHITAKA

  NA FATMA HAMAD PEMBA. Mahakama  ya  mkoa B iliopo   Kusini Pemba  imeghairisha  kesi ya  kuingilia kinyume na maumbile   inayomkabili   kijana  Khamis  Abdala Khamis  marufu   kirare   mwenye  umri   wa   [20] mkaazi  wa  Kangani  wilaya ya Mkoani   baada ya mtuhumiwa huyo  kukataa kusomewa shitaka lake .   Kijana  huyo wakati akiwa  ametulia  kizimbani  na  kusubiri  asomewe  shitaka  lake  aliambia mahakama  hiyo kuwa hali yake sio mzuri  anaomba  kesi ighairishwe na ipangiwe  siku nyengine.  ‘’Mheshimiwa hakimu leo naumwa   siwezi kukakaa hivyo  naiomba mahakama yako  ighairishe shauri  hilo kwa leo’’ alieleza  mtuhumiwa  kirare. Hakimu wa mahakama hiyo  Muumin  Ali  Juma hakufurahishwa na kauli  hiyo  na kumueleza   mtuhumiwa  huyo  kwamba  hiyo ni haki yako  na inahitajika upewe.  Lakini tu  nikueleze  leo  shahidi  ambae  ni  daktari  amekuja wewe unasema unaumwa  ila  na siku akidharurika  yeye  tutamruhusu aende na safari zake utaendelea  kukaa ndani atakapo rudi. ‘’ Usije uk

VIONGOZI DINI WAPEWA DAWA YA KUMALIZA MIGOGORO

Image
    NA FATMA HAMAD PEMBA. Viongozi   wa   dini   wametakiwa   kuwa   mstari   wa   mbele   kuwaelimisha   Wananchi    juu ya kulipa paumbele suala   zima la mirathi   jambo   ambalo   litapunguza   migogoro   katika   Jamii. Ushauri huo umetolewa na wadau waliopata mafunzo juu ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani katika kongamano la jenga amani yetu lililoandaliwa na shirika la Seach for Comman Ground lililofanyika Mgogoni Chake chake Pemba. Wamesema kuwa migogoro ya ardhi ndio tatizo kubwa ambalo linaonekana kuota mzizi   katika familia nyingi hapa Visiwani. Wameeleza kuwa   familia nyingi hazina tamaduni ya kurithishana mali wanazoachiwa na wazazi wao pindi wanapofariki kitu ambacho ndicho kinachochochea   kuongezeka   kwa migogoro   ya   ardhi   ndani ya Jamii. ‘’Kwa keli tunatatizo tusifichane   hatuna tabia ya kurithishana, na hiyo inapelekea wengine   kukosa haki yao stahiki, hivyo nyinyi mashekha munadhima kubwa   ya kutoa elimu juu ya hilo’’ walieleza wadau wa ama

mbunge wa wawi aekeza kwenye sekta ya michezo

Image
  NA FATMA HAMAD FAKI. Uwanja wa mpira wa miguu   wa   mtega   uliopo   Wilaya ya Chake Mkoa wa kusini Pemba   umeanza kufanyiwa   matengenezo   ili   kuona   unachezeka na unatumika muda   wote. Akizungumza na wandishi wa habari   mbele ya ukarabati   huo   Mbunge wa jimbo la Wawi Khamis   Kassim    Ali kupitia chama cha Mapinduzi    Amesema   takribani    miaka 45   uwanja   huo   umeonekana   kuchakaa   hivyo   ameamua   kufanyia   ukarabati    ili uwe uwanja    ambao   unaendana   kimichezo. ‘’Nimeamua kutengeneza uwanja huu ili kuwaondoshea changamoto   vijana ambao wameamua kuwekeza katika michezo’’ alieleza mbunge. Hivyo   Ametaka   wanamichezo hao   kuutunza   na kuulinda   uwanja huo   ambao utaleta manufaa kwao na kwa kizazi chao. Aidha   mbunge huyo   amesema   suala la mpira   kwa   sasa ni ajira,    hivyo ni wakati vijana kuchangamkia fursa hiyo   kwani kutawawezesha   kujipatia   kipato.   kwa  upande wake katibu wa timu ya Wawi star   Juma Muhammed Tamimu   ame

JAMII YAHINIZWA KUITUNZA AMANI

  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wadau   wa    ujenzi    wa    Amani   Kisiwani Pemba wametakiwa   kuendelea    kuielimisha jamii   juu    ya   athari    za   migogororo     na weweze    kujiepusha   ndani    ya    familia    zao. Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini ofisi ya rais tawala za mikoa na idara malum za SMZ   wakati akizungumza na wadau waliopatiwa   taluma ya   ujenzi wa amani huko   Green Folage Hotel iliyopo Chake chake   Mkoa wa Kusini Pemba. Amesema amani ndio msingi mkuu unaosababisha   maendeleo   Nchini, hivyo ni wakati   kwa kila   mtu kwa anafasi yake   kuchukua hatua ya kuwaelimisha wenzake   kuepuka kufanya mambo ambayo yanapelekea   migongano na mifarakano   isiyoyalima. ‘’Wadau   wenzangu   bado tunajukumu kubwa la kuisaidia jamii   kuwafahamisha jinsi ya kutatuwa   migogoro   kwa njia   ya   amani ili   kuona wanaishi kwa   kuvumiliana   na kusameheana   bila ya kulipiziana visasi ’’ alieleza Ofisa mdamini. Aidha kwa upande mwengine amewataka   wananchi   kut

HAKIMU AKATAA OMBI LA MBAKAJI.

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Mtuhumiwa   wa   kesi   ya   ubakaji    Mosi   Othman   Mosi    mkazi wa   Mchakwe   Muambe   ameiomba   Mahakama   kumfutia   shitaka   lake   kwa vile   shahidi ambae ndio muathirika   mwenyewe kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi. ‘’tarehe iliyopita    shahidi huyo hakuja,   na leo hakuja   basi muheshimiwa hakimu bora kesi ifutwe ili nirudi zangu kijijini niendelee na maisha yangu’’ alieleza mtuhumiwa mosi. Hakimu wa mahakama maalumu inayoshuhulikia kesi za ushalilishaji Mkoa wa kusini Pemba Mumin Ali Juma alikataa ombi la mtuhumiwa huyo na kumuambia kuwa kesi hiyo hawezi kuifuta, kwani kuna muda malumu uliowekwa kisheria kama mashahidi hawakuja ifutwe ila hiyo haijafikia muda wa kufutwa. ‘’Si kiubaliani na ombi hilo na kama shahidi huyo hakupatikana basi naomba aitwe shahidi mwengine ili tuweze kusikiliza kesi’’ alisema hakimu Muumin. Mtuhumiwa Mosi Othman Mosi utaendelea kukaa rumande na utarudi tena mahakamani hapa   tarehe 26/7/2022 kwa a

DK, MWINYI ALA SKUKUU NA MAYATIMA ZANZIBAR.

Image
  NA KAIJE SALUM ZANZIBAR. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi DK Hussein Ali Mwinyi amesema serikali itaendelea kushirikiana na taasisi mbali mabli za maendeleo kwajili ya kustawisha hali za wananchi. Dk mwinyi ameyasema hayo huko maoustung katika ghafla ya chakula   kilicho jumuisha makundi mbali mbali wakiwemo watototo Mayatima. Amesema kufuatia kuandaliwa kwa chakula hicho kunaashiria kuwepo kwa misingi ya upendo,mshikamano ni njia ya kuwathamini  Mayatima kuwa kama wale ambao hawajaondokewa na wazazi wao. Amesema misingi ya imani na hali ya utulivu uliyopo kumepelekea kuwepo kwa mapenzi ya dhati kwa wadau ambao wanaguswa na watoto mayatima. Amesema waislamu wanawajibu katika kuwahudumia Mayatima hivyo kulingana na maelekezo ya dini kuna faida kubwa katika kuwalea mayatima. Kwa upande wake mwenyekiti wa mandalizi ya ghafla hiyo   Mama Zainab Kombo Shaibu ametoa shukurani kwa wale wote waliyo saidia kufanikisha shughuli hiyo. Ghafla hiyo ya chakula cha pa

WANDISHI WA HABARI WAPEWA RUNGU PEMBA

Image
  Wandishi  wa  habari  wamehimizwa   kuendelea  kutumia nafasi   zao  kuihamasisha jamii  kushiriki zoezi la Sensa  ya watu na makazi ambalo linatarajiwa kuanza hivi karibuni . Wito huo umetolewa na Kamisaa  wa  sensa  Zanzibar  Balozi  Mohd  Haji  Hamza  wakati akizungumza na wandishi wa habari katika  mkutano ulioandaliwa na  Ofisi ya Mtakuimu mkuu wa Serikali  Zanzibar  huko  Jamhuri Holli Wete  Pemba. Balozi Hamza amesema vyombo vya habari vinamchango mkubwa katika kuendesha shughuli mbali mbali za Nchi, hivyo ni wakati wenu sasa kuwaelimisha Wananchi juu ya suala zima la sasa ili waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo. ‘’Wandishi wa habari tumieni sauti zenu na kalamu zenu  kuwashajiisha Jamii juu ya kushiriki zoezi zima la sensza  ya watu na makazi na kuhakikisha wanatoa tarifa sahihi’’ amesema kamisaa wa sense. Amesema  Sensa ya watu na makazi hufanyika kila baada ya miaka kumi [10] ambapo  lengo kuu la  kuepo  kwa zoezi hilo ni  kujua idadi ya watu  waliomo Nchini. Aidh
Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wandishi  wa  habari  wamehimizwa   kuendelea  kutumia nafasi   zao  kuihamasisha jamii  kushiriki zoezi la Sensa  ya watu na makazi ambalo linatarajiwa kuanza hivi karibuni . Wito huo umetolewa na Kamisaa  wa  sensa  Zanzibar  Balozi  Mohd  Haji  Hamza  wakati akizungumza na wandishi wa habari katika  mkutano ulioandaliwa na  Ofisi ya Mtakuimu mkuu wa Serikali  Zanzibar  huko  Jamhuri Holli Wete  Pemba. Balozi Hamza amesema vyombo vya habari vinamchango mkubwa katika kuendesha shughuli mbali mbali za Nchi, hivyo ni wakati wenu sasa kuwaelimisha Wananchi juu ya suala zima la sasa ili waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo. ‘’Wandishi wa habari tumieni sauti zenu na kalamu zenu  kuwashajiisha Jamii juu ya kushiriki zoezi zima la sensza  ya watu na makazi na kuhakikisha wanatoa tarifa sahihi’’ amesema kamisaa wa sense. Amesema  Sensa ya watu na makazi hufanyika kila baada ya miaka kumi [10] ambapo  lengo kuu la  kuepo  kwa zoezi hilo ni  kujua idadi

OFISI YA MUFTI YA NENA JUU YA WATU WENYE ULEMAVU.

Image
NA FATMA HAMAD FAKI. Waumini wa dini ya kiislamu pamoja na watu wenye uwezo wa Kusaidia misaada mbalimbali ya kijamii wamehimizwa kuendele   kuwasaidia   wanyonge   hususan   jamii ya watu wenye ulemavu. Kauli hiyo imetolewa na naibu katibu mufti ofisi ya Pemba Said Ahmad mara baada ya kumtembelea mwalimu wa madrsatul juhudia Sada Khamis Hamad mwenye ulemavu wa viungo mkazi wa Shumba vyamboni wilaya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema ziara hiyo ya kumtembelea mwalimu huyo imekuja kufuatia tarifa iliyotolewa na vyombo vya habari ikiwemo mtandao wa Pemba Ya Leo  Blog iliyonesha changamoto zinazo mkabili mwalimu huyo ya ukosefu wa madrsa ya kufundishia wanafunzi wake. ‘’Kama ofisi ya mufti tumeguswa na hilo na ndio mana tukaamua kuja kukuona na sisi tuweze kukusikiliza kero zako ambazo zinakukabili katika madrasa yako’’ alisema sheikh Said. Alisema kwa vile ofisi ya mufti ndio mlezi mkuu wa madrsa zote za quran watafanya jitihada mbali mbali pamoja na kutafuta wahisani ili kuona a