Posts

Showing posts from February, 2024

UTELEKEZWAJI WA WANAWAKE UNAVYOCHANGIA KUONGEZEKA KWA UDHALILISHAJI

Image
      NA FATMA HAMAD,PEMBA Utelekezwaji wa Wanawake na Watoto imedaiwa ni moja ya sababu inayo changia kutokea kwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia   ikiwemo kubakwa, kulawitiwa, kwa watoto. Hayo yamesemwa na hakimu wa Mahakama maalumu ya kupambana na Udhalilishaji iliyopo Wete, Muumin Ali Juma wakati akizungumza na Wananchi katika mkutano malumu wa kuwaelimisha Wananchi umuhimu wa kuripoti na kutoa ushahidi Mahakamani huko Chamboni wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema wilaya ya Micheweni ni moja   ya wilaya inayongoza kwa utelekezaji wa wanawake, katika mkoa wa Kaskazini Pemba   jambo ambalo   linachangia   watoto kudhalilishwa. ,,Unamuacha mwanamke na watoto humpi huduma yoyote jee umetegemea nini, niwaulize wanaume wenzangu kesho mbele ya Mungu tutakwenda kujibu nini,aliuliza. Alisema   mara nyingi kesi   zinazofikishwa mahakamani   za waliofanyiwa udhalilishaji ni watoto ambao wamekosa malezi ya pamoja kati ya Baba na Mama, hivyo aliwataka wananchi ha

MIUNDO MBINU MIBOVU YA SKULI YA PUJINI KERO KWA WANAFUNZI SKULINI HAPO

Image
      NA FATMA HAMAD, PEMBA Walimu wa Skuli ya msingi Pujini wilaya ya Chake chake mkoa wa Kusini Pemba wametoa ya moyoni juu ya uwepo wa   miundombinu mibovu, pamoja na uhaba wa madarsa ya kufundishia Wanafunzi wao. Wakizungumza mbele ya viongozi wa jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chake chake wamesema baadhi ya madarsa yanavuja jambo linalopelekea kipindi cha mvua kushindwa kuendelea na vipindi kutokana na kukosa sehemu ya kufundishia. ,,Tunakilio Skuli yetu inavuja ikinyesha mvua inabidi tutafute sehemu tujifiche mpaka mvua ipite ndio tuendelee na vipindi, walieleza. Aidha walisema kuwa bado wanachangamoto ya uhaba wa vyumba vya kufundishia, hivyo wanahitaji kusaidiwa kuezekewa jingo lao ambalo tayari walishalijenga. Badhi ya wanafunzi wanaosoma Skulini hapo wamesema darasa moja lina zaidi ya wanafunzi 80,hivyo wameutaka uongozi huo kuwafanyia msaada wa kuwezekea pamoja na kuwajengea madarasa mengine jambo ambalo litaondosha usumbufu kwa wanafunzi pamoja na

WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUWANZISHA MIRADI AMBAYO ITAWALETEA MAENDELEO

Image
      NASALIM HAMAD PEMBA. Kaimu mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria wilaya ya Micheweni [Midipao] Saleh Hamad Juma amewataka wajasiriamali kuanzisha miradi kama vile utengenezaji wa Sabuni,Ukulima wa mboga ili waweze kujipatia faida itakao saidia kuendesha vikundi vyao. Ushauri huo ameutoa wakati akizungumza na wanakikundi cha kueka na kukopa cha Hatusemani kilichopo   Tumbe kaliwa wilaya ya Micheweni mkoa wa Kakazini Pemba katika kikao maalumu kilichoandaliwa na jumuiya hiyo cha kuishajiisha jamii kujiunga na vikundi vya ujasiriamali. Alisema endapo watazalisha Sabini, au kujingiza kwenye kilimo cha mboga mboga watajipatia kipato na kukuza vikundi vyao kupiga hatua kimaendeleo. ‘’Niwaombe mama zangu musishie tu kuja mukiweka pesa na kuondoka, bali anzisheni miradi ili muweze kuviendeleza vikundi vyenu pamoja na kujipatia kipato ambacho kitainua maisha yenu, alisema.   Aliendelea kusema endapo watazalisha bidhaa zenye ubora ambazo zitaendana na soko la dunia wanawez

.KATIBU MKUU WA CHAMA CHA CUF AMEVITAKA VYAMA VYA SIASA KUITUNZA NA KUILINDA AMANI YA NCHI

Image
      NA FATMA HAMAD, PEMBA. Katibu Mkuu wa chama cha wananchi [CUF] Hamad Masoud Hamad amevitaka Vyama Vya Siasa kufanya siasa za kistarabu ili kuepusha maafa   yanayoweza kujitokeza katika Nchi. Katibu huyo ameyasema hayo katika hafla ya kuwaombea duwa wafuasi wa chama hicho waliofariki katika Mandamano ya mwaka 2001   pamoja na wanzilishi wa chama hicho iliyofanyika Mchanga mdogo Wete Pemba. Alisema maafa yakitokea hayachagui, hivyo ni vyema Viongozi wa vyama vya siasa kuendesha siasa zao kistarabu na kwa mujibu wa taratibu na sheria zinavyoelekeza ili kuepusha migogoro isiyoyalazima. ‘’Niwaombe viongozi wenzangu tujitahidi sana katika siasa zetu ili kilichotokea mwaka 2001 tuhakikishe hakitokei tena kwenye maisha yetu ni hatari, alisisitiza Aidha aliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuweka mkakati madhubuti ili kuona kila mmoja anaheshimu haki ya mwenzake, jambo ambalo litasaidia kuendelea kuwepo kwa Amani na Utulivu Nch

AFISA MDHAMINI WIZARA YA UTALII PEMBA ATOA NENO KWA WANDISHI WA HABARI

Image
                                     NA FATMA HAMAD, PEMBA Afisa mdhamini   wizara ya Utalii na mambo ya kale Pemba Zuhura Mgeni amewataka Wananchi   wa Pemba pamoja na wageni kutoka nje ya Pemba kuvitembelea vivutio vya Utalii vilivyopo kisiwani humo ili waweze kuitangaza Pemba kiutalii. Akizungumza na Wandishi wa habari kutoka Chama cha wandishi wa habari [PPC] kisiwani Pemba   mara baada ya kumaliza   ziara ya kutembelea vivutio vya Utalii vilivyopo kisiwani humo. Alisema kisiwa cha Pemba hususani mkoa wa kaskazini umejaliwa na vivutio vingi vya utalii, hivyo ni vyema wananchi pamoja na wageni kuvitembelea vivutio hivyo ili viweze kuinua Pemba katika Sekta ya Utalii. ‘’Niipongeze Jumuiya ya Wandishi wa habari Pemba kwa uwamuzi muliochukuwa wa kutembelea vivutio   mbali mbali vya   Utalii vilivyopo Pemba ili muweze kuutangaza utalii kisiwani humo,alisema. Alisema sekta ya Utalii ni moja ya sekta ambayo inaisaidia Serikali kuingiza mapato, hivyo watahakikisha wanavitunza viv