Posts

Showing posts from June, 2021

KAMATI ZA ULINZI NA USALAMA PEMBA ZA TAKIWA KUWA WADILIFU WAKATI WA UKODISHWAJI WA MASHAMBA YA MIKARAFUU

Image
NA LAILAT MSABAH PEMBA. Kamati za ulinzi na usalama katika mikoa miwili ya Pemba zimetakiwa kuwa makini katika kusimamia zoezi la ukodishwaji wa mashamba ya karafuu ya Serikali ili kuona misingi ya ukodishaji wa mashamba hayo inafuatwa na kuepusha upotevu wa mapato ya serikali. Akizungumza katika kikao na kamati iliyoonda kusimamia ha ukodishwaji wa mashamba hayo Mkuu wa Mkoa wa kaskazi Pemba Salama Mbarouk Khatibu amesema kamati hizo zinao wajibu mkubwa wa kuona mashamba ya karafuu yanakodishwa katika hali ya amani bila ya kuwepo na migogoro. ‘’Munadhamana kubwa kuhakikisha hakutokei migogoro yoyote wakati wa zoezi hilo la ukodishwaji mikarafuu’’ Alisema bi salama. Amewafahamisha kuwa endapo watasimamia zoezi hilo kwa uadilifu wa hali ya juu   na kufuata taratibu zilizowekwa kutasaidia kuiongezea Serikali mapato yanayotokana na zao la karafuu.   Mkuu wa wilaya ya Wete Mgeni Khatibu Yahya ameziomba kamati za ulinzi na usalama kufuatilia maeneo ambayo tayari uchumaji wa karafu

Wawili washikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za wizi wa mifugo.

Image
FATMA HAMAD FAKI -  PEMBA. Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba linawashikilia vijana wawili wakituhumiwa kwa wizi wa mifugo huko Kiwani na Mgagadu Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa kusini Pemba. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba ACP Richard Tadei Mchovu amewataja vijana hao kuwa ni Moh`d Salum (35) Mkaazi wa Kilimani Mgagadu na Yussuf Rashid Moh`d  (30) Mkaazi wa Nanguji Kiwani katika Wilaya ya Mkoani Pemba ambapo wamekamatwa afajiri ya jana June 21 wakiwa na ng`ombe kwenye gari aina ya keri.. Akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini kwake Madungu Chake Chake Kamanda Mchomvu amesema watuhumiwa hao wamekatwa na ng`ombe na wawili katika operesheni iliyofanya na jeshi hilo la kudhibiti wizi wa mifugo. Aidha Kamanda Mchovu ametoa wito kwa wananchi kushirikiana pamoja katika kuzuia wimbi la wizi wa mifugo ambalo limekithiri katika maeneo mbali mbali huku akitoa wito kwa wafuagaji kuwa makini katika uangalizi wa mifugo yao. Kwa upande mwengine Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini P
Image
NA FATMA HAMAD PEMBA Jamii imeonywa kuacha tabia yakuwaficha wahalifu wanaowafanya matukio ya udhalilishaji wa kijinsia na kuzifanyia suluhu kesi za hizo majumbani jambo ambolo linapelekea kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji. Akizungumza na Wazazi na Walezi katika mkutano wa kuielimisha jamii juu ya athari za udhalilishaji katibu wa kamamati ya madili Zanzibar Abdala Mnubi Abass huko Tumbe wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema vitendo vya udhalilishaji vinajitokeza siku hadi siku, lakini bado jamii inaonekana ikizifumbia macho na  kuzifanyia suluhu kesi hizo wenyewe kwa wenyewe. ‘’ wakishafanya makosa ya udhalilishaji mna watorosha watoto wenu, wazazi wacheni hii tabia, Alisema Abdala Mnubi’’. Amesema wengi wafanyaji wa matukio hayo ni watu wa karibu katika familia, hivyo wazazi wanapodhalilishiwa watoto wao wasiwaonee haya wala wasiogope maneno ya mitaani bali wasimame kidete  na kuwaripoti katika vyombo vya sheria ili kuchukuliwa hatua kali dhidi yao.
Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Familia zimetakiwa kuendeleza kutoa huduma wakati wanapoachana na wanandoa wenzao ili kuwakinga watoto wao na udhalilishaji wa kijinsia. Wito huo umetolewa na Mohd Adam Makame kadhi kutoka Wilaya ya Mkoani  katika mkutano wa kujadili changamoto za utekelezaji wa majukumu ya ufuatiliaji wa matukio ya udhalilisha kwa wadau wa kupinga udhalilishaji wa Mkoa wa Kusini  huko  ukumbi wa Chama cha Wandishi wa habar Wanawake Tanzania [Tamwa] Chake chake Pemba. Amesema imebainika kuwa maranyingi Wazazi wanapoachana huwa ni pigo na mama na Watoto, kwani huwelemezewa mzigo wa malezi Mama peke yake jambo linalopelekea kukosa huduma stahiki. Amesema watoto wengi ambao wazazi wao wameachana hujiingiza katika ajira ikiwemo biashara ili kujitafutia mahitaji yao hali ambayo inasababisha kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia. Hivyo amewataka wanandoa kuvumiliana katika ndoa zao ili waweze kuishi na wenza wao na kuwalelea watoto wao katika malezi ya pamoja. Kwa upande mwe

WIZI WA MBUZI WAMSABABISHIA KWENDA JELA PEMBA

Image
NA FATMA HAMAD PEMBA  11/6/2021. Jeshi la Polisi   Mkoa wa Kusini Pemba limefanikiwa kuwakamata watu 30 wanaotuhumiwa kujihusisha   na matukio mbali mbali ikiwemo wizi wa mazao pamoja na   mifugo. Akizungumza na Wandishi wa habari huko ofisini kwake Madungu   Kamanda wa polisi mkoa huo Richad Mchovu amesema watuhumiwa hao wamewakamata kupitia opereshen ya wiki moja iliofanywa na jeshi hilo     Mkoani hapa kwa ajili ya kupambana na uhalifu ambao wanafanyiwa wananchi katika Vijiji vyao. Amesema wahalifu hao 30,   saba ni wezi wa mifugo,   sita ni wezi wa mazao katika maeneo tofauti ,   wawili ni wezi wa mbuzi, wanne   walikamatwa maeneo ya mtambile wakiwa wameiba ngombe 3, watatu walikamatwa na madawa ya kulevya   na   kumi na mbili ni     wizi wa kuku. Amefahamisha kuwa   mmoja   wawili kati ya hao walioiba mbuzi tayari hatua za kisheria zimeanza kuchukuliwa dhidi yake na ameshahukumiwa   kutumikiwa chuo cha mafunzo. Aidha amesema upareshen hiyo bado inaendelea hivyo amewataka w

`UCHELEWESHWAJI WA UENDESHWAJI WA KESI MAHAKAMA KUNASABABISA MASHAHIDI KUSHINDWA KUFIKA MAHAKAMANI KUTOA USHAHIDI

Image
  NA   FATMA   HAMAD   - PEMBA       Ucheleshwaji wa uendeshwaji wa kesi mahakamani ni chanzo kinachochangia baadhi ya wananchi kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi katika kesi za udhalilishaji hali ambayo inapelekea kesi hizo kushindwa kupata hukumu na hatimae hupelekea kufutwa. Wakizungumza katika   mkutano wa majadiliano juu ya kupambana na udhalilishaji wa kijinsia, wananchi wa mkoa wa kusini pemba katika mkutano   ambao umewakutanisha watumishi mbali mbali wa Serikali wakiwemo mahakimu, madpp, mapolisi, mafias ustawi wa jamii pamoja na wasaidizi wa sheria huko ukumbi wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Chake chake Pemba. Wamesema bado uwendeshwaji wa kesi mahakamani unaonekana kusua sua, hivyo hupelekea wazazi wa wahanga   wa matukio ya udhalilishaji kukata tama na kukataa moja kwa moja kwenda mahakamani kutoa ushahidi. ‘’Ukienda leo unaambiwa mjoo, kesho ukija unaambiwa kesho kutwa hii inatuumiza hatuna nauli za kila siku, wakati hata nauli hatup