Posts

Showing posts from April, 2022

NUHU KOMBO NUHU AENDELEA KUSOTA RUMANDE

Image
  NA FATMA HAMAD-- PEMBA. Hatimae mahakama ya mkoa B Wete, imemrejesha tena rumande mtuhumiwa wa ulawiti Kombo Nuhu Kombo miaka 19 baada ya kubainika kuwa ni mtu mzima licha ya awali kupewa dhamana kama ni mtoto mahakamani hapo. Awali mtuhumiwa alipelekwa rumande mwanzoni mwa mwaka huu kwa tuhuma za ulawiti kwa kijana mwenye ulemavu wa akili ingawa upande wa utetezi ulidai na kuthibitisha kuwa mteja wao hakutendewa haki kupelekwa rumande kwa sababu ni mtoto. Wakati kesi yake ikiendelea miezi mitatu iliyopita   na kuwasilishwa   vielelezo mahakamani hapo na upande wa utetezi mahakamani   iliridhia na kumpa dhamana mtuhumiwa huyo   kama mtoto. Huku upande wa mashtaka ukiendelea kung’ang’ania   kwamba mtuhumiwa ni mtu mzima, kisha uliwasilisha vielelezo kadhaa ikiwemo cheti cha kuzaliwa cha mtuhumiwa na mahakama kutengua uwamuzi wake wa awali juu ya umri wa mtuhumiwa. Mwendewsha mashtaka katika shauri hilo Juma Ali Juma alidai mahakamani hapo kuwa anaelewa kuwa mtuhumiwa Nuhu Ko

UDHALILISHAJI BADO NI KILIO KWA WANAWAKE NA WATOTO

Image
  NA FATMA HAMAD- PEMBA. Mahakama   maalum inayoshughulikia kesi za udhalilishaji mkoa wa Kusini Pemba imeihairisha kesi ya ubakaji inayomkabili mtuhumiwa Ali Usi Simai mtumzima wa miaka 32 mkaazi wa Mchakwe Muambe anaedaiwa kumbaka msichana wa   miaka   nane (8)ambapo kufanya hivyo ni kosa kisheria. Akizungumza mbele ya Mahakama hiyo mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka Ofisi ya mkurugenzi   wa mashtaka DPP   Seif Mohd Khamis ,aliiambia mahakama   iihairishe kesi hiyo   kwani   upande wa mashtaka hawakupokea   chaji shiti   ya kesi wenyewe. “Mheshimiwa sikupokea chaji shiti, kwa hivyo siwezi kucheza na haki ya mtu   kwani sijui kilichoandikwa kwenye file hilo naomba uipangie siku nyengine ili niweze kulipitia’’, alisema DPP Seif. Kwa upande wake wakili wa kujitegemea Saleh Said Moh’d alisema hakubaliani na ombi hilo kwani   wamekuja na mashahidi 4 akiwemo   mwenyewe   mtuhumiwa, hivyo kuihairisha itakuwa shida lazima tuwaangalie   mashahidi wenyewe wametoka mbali jambo ambalo

KUKOSEKANA MKALIMANI MASKULINI BADO NI TATIZO KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

Image
  NA FATMA HAMAD-- PEMBA. Kukosekana kwa walimu wanaojua lugha za alama maskulini bado ni kilio kikubwa kinacho wa kwaza wanafunzi wenye ulemavu kisiwani Pemba. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao Kwale gongo wilaya ya Wete kaskazini Pemba, wazazi wa watoto wenye ulemavu walisema suala la kuchanganywa darasa   pamoja na wanafunzi wengine bila ya kuepo kwa   mwalimu wa lugha za alama kunachangia wanafunzi hao kutofaulu mitihani yao na kusababisha kushindwa kufikia malengo yao. ‘’Mfumo wa elimu mjumuishi wa kuchanganywa pamoja na wanafunzi wenye ulemavu na   wengine   bado hauja watendea haki watu wa aina hiyo   maskulini,’’ alisema mama mzazi wa Abdala Hussein mwenye ulemavu wa uziwi, mdomo na mguu. Alisema mtoto wake anasoma darasa la kumi ila hana tamaa ya kufaulu kutokana na changamoto hiyo   na kuiomba   wizara ya elimu kumuona   kijana huyo na kuweza kumsaidia kwa hali na mali ili kuona na yeye amekuja na ufaulu mzuri. Akiendelea kueleza kwa masiki

Kukosekana kwa mkalimani maskulini kunadumaza mafanikio ya wanafunzi wenye ulemavu Pemba

Image
  NA FATMA HAMAD-- PEMBA. Kukosekana kwa walimu wanaojua lugha za alama maskulini bado ni kilio kikubwa kinacho wa kwaza wanafunziwenyeulemavu kisiwani Pemba. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao Kwale gongo wilaya ya Wete kaskazini Pemba, wazazi wa watoto wenye ulemavu walisema suala la kuchanganywa darasa  pamoja na wanafunzi wengine bila ya kuepo kwa  mwalimu wa lugha za alama kunachangia wanafunzi hao kutofaulu mitihani yao na kusababisha kushindwa kufikia malengo yao. ‘’Mfumo wa elimu mjumuishi wa kuchanganywa pamoja na wanafunzi wenye ulemavu na  wengine  bado hauja watendea haki watu wa aina hiyo  maskulini,’’ alisema mama mzazi wa Abdala Hussein mwenye ulemavu wa uziwi, mdomo na mguu. Alisema mtoto wake anasoma darasa la kumi ila hana tamaa ya kufaulu kutokana na changamoto hiyo  na kuiomba  wizara ya elimu kumuona  kijana huyo na kuweza kumsaidia kwa hali na mali ili kuona na yeye amekuja na ufaulu mzuri. Akiendelea kueleza kwa masikitiko mama