Posts

Showing posts from March, 2021

Mrithi wa Maalim Seif huyu hapa

Mrithi wa Maalim Seif huyu hapa

VIONGOZI WA DINI WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA JAMII JUU YA UMUHIMU YA MWANAMKE KUWA KIONGOZI

Image
  Viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuielimisha jamii juu ya   umuhimu wa mwanamke kushika nafasi za ungozi katika ngazi mbali mbali za kutunga Sheria. Akizungumza na viongozi wa dini ya kiislamu Kisiwani Pemba   Afisa fatwa kutoka ofisi ya Mufti Sheikh Said Ahmad Muhammed katika mkutano wa uwasilishwaji wa ripoti ya miezi mitatu juu ya mwanamke kuwa kiongozi huko   Tamwa   Chake chake Pemba. Sheikh Said alisema Uislamu hauja mkataza mwanamke kua kiongozi ilihali tu afuate Sheria,Mila na Maadili yake . ‘’Dini haijamzuia mwanamke kuwa kiongozi bali afuate sheria na Madili ya dini yake’’ Alisema Sheikh Said. Hivyo alisema wakati umefika kwa viongozi wa dini mbali mbali kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha mwanamke nayeye anashiriki katika nafasi mbali mbali za uongozi. Aidha Shikh Said amewataka wazazi na Walezi kutowabagua watoto   Kijinsia   katika kutoa fursa za kuwapatia Elimu. Wakichangia katika mkutano huo baadhi ya viongozi hao   walisema kuwa ipo haja ya kutolewa

Waandishi wa Habari Pemba Watakiwa kutoa elimu kwa vyama vya siasa juu ya nafasi ya mwanamke.

Image
  Wandishi wa habari wametakiwa kutoa elimu kwa vyama vya siasa waweze kutoa fursa sawa za uongozi kwa Wanawake na Wanaume ili kuona Wanawake na wao wanashika nafasi za uongozi katika ngazi mbali mbali za maamuzi. Hayo yamesemwa na mwezeshaji wa mafunzo ya uhamasishaji wa Wanawake katika ushiriki wa Demokrasia na uongozi kwa wandishi wa habari huko Ofisi za Tamwa Mkanjuni Chake chake Pemba. Amesema imeonekana bado hakuna uwiano sawa baina ya wanaume na Wanawake katika ngazi mbalimbali za maamuzi, hivyo ni jukumu la wandishi wa habari kuwa eilimisha viongozi wa vyama vya siasa kuondosha vikwazo ambavyo vinawakosesha fursa ya uongozi wanawake wenye nia ya kugombea. ‘’Ni jukumu lenu Wanahabari kuwapa elimu viongozi wa kisiasa kuondosha vikwazo vinavyowafanya wanawake washindwe kuwa viongozi’’. Alisema Bi sabah. Amesema mwanamke ana nafasi kubwa ya kuwasilisha matatizo ya jamii yakiwemo ya Wanawake katika vyombo vya mamuzi kwa kulinganisha naWanaume. Hivyo ameisihi jamii kuondosh