Posts

Showing posts from November, 2022

JAMII YAHIMIZWA KUTUNZA USAFFI MAZINGIRA

  NA SAID ABRAHMAN PEMBA.   WANAJAMII wametakiwa kutunza mazingira yao na kuhifadhi maji taka ( maji machafu) ili kuepusha maradhi ya mripuko yanayoweza kutokezea katika maeneo yao.   Hayo yalielezwa na Bwana afya kutoka Baraza la Mji Wete Salim Mbarouk Rashid wakati alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Wete.   Alieleza kuwa kumekuwepo na utiririkaji Mkubwa wa maji taka (machafu) katika majumba jambo ambalo ni tatizo kubwa Kimazingira na hivyo kufanya mazingira kuwa katika hatari na kuwa Kero katika jamii.   "Kutokana na Hali ambayo ipo katika jamii,suala la kutiririka Kwa maji taka linahatarisha afya Kwa wananchi na hivyo kupelekea kuibuka Kwa maradhi mbali mbali ya miripuko ikiwemo matumbo na kipindupindu," alieleza Salum.   Aidha Salim alifahamisha kuwa ikiwa Baraza la Mji Wete ndio wasimamizi wakuu wa Usafi katika Mji wamekuwa na mikakati mbali mbali ili kuona hali hiyo inapungua au kuondoka kabisa katika jamii.   "Mikakati

JAMII YAHIMIZWA KUONGEZA USHIRIKIANO ILI KUMALIZA UDHALILISHAJI UDHALILISHAJI

Image
                                  NA FATMA HAMAD FAKI PEMBA 23/11/2022. Jamii imetakiwa kuacha tabia  ya kuzifanyia suluhu  mitaani kesi  za udhalilishaji wa kijinsia  na badalayake  wasimame mahakamani  kutoa ushahidi ili kupunguza ukatili  kwa wanawake na watoto. Ushauri huo ametolewa na mwenyekiti wa kamati za asasi za kiraia Nassor Bilal Khamis wakati akitoa tarifa kwa vyombo vya habari katika  kuelekea  shamra shamra ya madhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili kwa wanawake na watoto huko tamwa chake chake Pemba. Amesema  bado matendo ya udhalilishaji yafanyika kila siku katika shehia zetu, hivyo ni wakati jamii kuondosha rushwa muhali ili kuona wahanga wa matukio hayo wanapata haki zao stahiki. ‘’kwa kweli jamii imekua na muhali mkubwa juu ya kusimama mahakamani na kutoa ushahidi kwenye vyombo vya kisheria matukio ya udhalilishaji’’ alisema mwenyekiti. Amesema kwa mujibu wa ripoti za takwimu za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia  Zanzibar takwimu kutoka ofisi ya mtakwi

KOSA LA ULAWITI LAMSABABISHIA KWENDA JELA MIAKA 7

Image
                                NA FATMA HAMAD, PEMBA MSHITAKIWA Nuhu Kombo Nuhu miaka 19, mkaazi wa Kijichame wilaya ya Micheweni, amehukumiwa kwenda chuo cha Mafunzo kwa   muda wa miaka saba ‘7’ na kulipa fidia ya shilingi milioni 1, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumlawiti kijana mwenzake mwenye ulemavu wa akili. Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka, Juma Mussa Omar alisema kosa alilolifanya kijana huyo ni kitendo kibaya ndani ya jamii. Alisema, kila siku jamii imekuwa ikilalamikia uwepo wa matendo hayo, hivyo kama kila upande umeshatekeleza wajibu wake ni wakati sasa wa mahakama kutoa adhabu kali. ‘’Jamii imekua na kilio kikubwa juu ya matukio ya udhalilishaji wa kijinsia, hivyo tunakuomba utoe adhabu kwa mujibu wa kifungu kinavyoelekeza, ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia kama hiyo,’’alishauri. Baada ya kupanda kizimbani na kusubiri asomewe hukumu yake mshtakiwa huyo, aliomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwani bado ni k

WASTAAFU WATARAJIWA WAFUNDWA

Image
                        NA FATMA HAMAD FAKI PEMBA. Kaimu mkurugenzi wa huduma kwa wateja kutoka   mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF Khatib Iddi Khatib amewataka wafanyakazi katika tasisi za umma kuwa na utaratibu wa kuamzisha miradi nbali mbali wanapokuwa kazini ili iwasaidie   mara watakapo staafu. Ushauri huo ameutoa wakati akiwasilisha mada juu ya matayarisho ya kustaafu katika mkutano wa mafunzo ya   wastau watarajiwa uliofanyika katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Pemba. Amesema Kila mtumishi wa umma kwa vile ameajiriwa ajuwe kama kuna siku ataondoka, hivyo ni vyema kubuni mbinu mbadala ikiwemo kuweka miradi   ambayo itawapatia kipato cha halali katika maisha yao ya kustaafu kwao. ‘’hatuwezi kudumu milele makazini tukubali kuwa ipo siku tutaondoka hivyo ni lazima   tuweke vyanzo ambavyo vitakuja kutupatia kipato Pencheni sio kama mshahara haitoshi kuendesha maisha yetu’’alikumbusha kaimu mkurugenzi. Akifungua mafunzo hayo Ofisa mdhamini wizara ya Nchi Fedha na Mipan

KIRARE AFUNGWA JELA

  NA FATMA HAMAD PEMBA Mahakama ya mkoa C iliyopo Chake chake imemuhukumu kijana Khamis Abdala Khamis maarufu   [Kirare]   mwenye umri wa miaka 20 mkaazi wa Kangani   wilaya ya Mkoani Pemba kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 19 na fidia ya shilingi Milioni mbili[200,000] baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutorosha na kulawiti mvulana wa miaka 10. Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka [DPP] Ali Amour Makame ameiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa huyo makosa yote mawili alioyafanya ni makubwa na kwa maelezo kutoka kwa daktari ni kwamba amesababisha ulemavu kwa mhanga, hivyo naiomba mahakama yako itowe adhabu kali ambayo itakuwa ni funzo kwake na wengine wanaotenda makosa hayo. ‘’Jamii imekua ikisikitika sana kwa matendo haya ya kihalifu hivyo nivyema mahakama yako ikampa adhabu kali kijana huyo’’ alidai Dpp Ali. Hakimu wa mahakama hiyo Muumin Ali Juma amemueleza   mtuhumiwa kwamba mahakama imekuona na hatia kwa makosa yote mawili la kutor