KOSA LA ULAWITI LAMSABABISHIA KWENDA JELA MIAKA 7

 






                              NA FATMA HAMAD, PEMBA

MSHITAKIWA Nuhu Kombo Nuhu miaka 19, mkaazi wa Kijichame wilaya ya Micheweni, amehukumiwa kwenda chuo cha Mafunzo kwa  muda wa miaka saba ‘7’ na kulipa fidia ya shilingi milioni 1, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumlawiti kijana mwenzake mwenye ulemavu wa akili.

Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka, Juma Mussa Omar alisema kosa alilolifanya kijana huyo ni kitendo kibaya ndani ya jamii.

Alisema, kila siku jamii imekuwa ikilalamikia uwepo wa matendo hayo, hivyo kama kila upande umeshatekeleza wajibu wake ni wakati sasa wa mahakama kutoa adhabu kali.

‘’Jamii imekua na kilio kikubwa juu ya matukio ya udhalilishaji wa kijinsia, hivyo tunakuomba utoe adhabu kwa mujibu wa kifungu kinavyoelekeza, ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia kama hiyo,’’alishauri.

Baada ya kupanda kizimbani na kusubiri asomewe hukumu yake mshtakiwa huyo, aliomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwani bado ni kijana mdogo na anafamilia inayomtegemea.

‘’Mheshimiwa hakimu naomba mahakama yako inipe adhabu ndogo japo kifungo cha nje tu, nitakuja kufyagia ofisini kwako au hata Hospitali,’’aliomba mshitakiwa huyo.

Hakimu wa mahakama ya mkoa inayoshughulikia makosa ya udhalilishaji mkoa wa Kaskazini Pemba Abdulrahman Ali Abdul rahman alisema kesi hiyo imesikilizwa ikiwa na mashahidi wa watano, ambao ulitosha kuishawishi mahakama kumtia hatiani.

‘’Mashahidi walioletwa na upande wa mashtaka, ulikidhi vigezo na haukucha chembe ya shaka, hivyo kuishawishi mahakama kumtia hatiani mshitakiwa Nuhu,’’alieleza.

Tukio hilo lilitokea Disemba 13, mwaka 2021, majira ya saa 1:30 asubuhi eneo la Kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba, ambapo mshitakiwa huyo, alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili.

Kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 116 (1), cha sheria Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.

                     

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.