Posts

Showing posts from December, 2020

Watendaji wa wizara ya maji kisiwani, Pemba wamelalamikia kunyimwa haki zao

Image
  Watendaji wa wizara ya maji kisiwani, Pemba wamelalamikia juu ya ukosefu  wa haki na fursa za kielimu ambazo zimekua zikipatikana kupitia wizara hio kwa muda mrefu sasa. Malalamiko hayo wameyatoa mbele ya waziri wa wizara ya maji na nishati Zanzibar Sleimani Masoud Makame,wakati alipokutana na watendaji wa wizara hio kisiwani Pemba ambapo watendaji hao  wamedai kua wamekua wakikoseshwa fursa mbalimbali kutoka wizara hiyo ikiwemo fursa ya mafumzo. ‘’Mheshimiwa Waziri Mkurugenzi wetu mtu aliekua hana elimu ndio anaempa kipao mbele na maranyingi huwateuwa nafasi kubwa wale waliokua hawana elimu’’Walisema  wafanyakazi wa wizara hiyo. Baada ya kupokea malalamiko hayo waziri wa wizara hio amemuagiza mkurugenzi  wa mamlaka ya maji Pemba Omari Mshindo Bakari, kushughulikia upatikanaji wa stahiki za wafanyakazi hao. ‘’Mkurugenzi naomba kuanzia sasa kila mmoja hakikisha anapata haki yake, sitaki kuletewa  tena malalamiko ya mtu kakosa haki yake’’Alisema Waziri. Aidha waziri huyo amew

AFUNGWA JELA MIAKA KUMI KWA UBAKAJI PEMBA

Image
  MAHAKAMA ya Mkoa Wete iliyopo Kaskazini Pemba imemhukumu kwenda chuo cha mafuno kwakipindi cha miaka kumi Khalfa Khalfan Mwaveso baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kubaka. Mwaveso mwenye umri wa miaka 25 alitenda kosa hilo mwezi oktoba 2019, ambapo alimbaka msicha mwenye umri wa miaka 17. Kabla ya kusomewa hukumu na hakimu wa mahakama hiyo Abdalla Yahya Shamun, Mwaveso aliomba amahakama impunguzie adhabu ikiwa ni pamoja na kumpa kifungo cha nje ili aende kutumikia jamii. “Naiomba mahakama yako inipunguzie adhabu ikiwa ni pamoja na kunipa adhabu mbadla ya kutumikia jamii kwani hili ni kosa langu la kwanza”alisema. Hata hivyo upaande wa mashitaka ukingozwa na jopo la waendesha mashtaka Juma Mussa, Ali Amour na Mhammed Said waliiomba mahakama itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa wote wenye tabia kama hiyo  kwani matendo ya aina hii yamekithiri ndaani ya jamii. “Tunaiomba mahakama itoe dhabu kali kwa mtuhumiwa ili fundisho kwake na wengine wenye tabia kama hii kwani matendo k