Posts

BANDA LA DHARURA LA KULALA WANAFUNZI LAUNGUA MOTO

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Banda la dharura la wanafunzi 80 wa Kiume katika  Skuli ya Sekondari ya Chwaka tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, limeteketea kwa moto na kuunguza kila kitu kilichokuwemo katika jengo hilo.   Akizungumzia kutokea kwa moto huo mmoja kati ya wanafunzi wa Skuli hiyo Ibrahim Bakar Hamad alisema moto huo ulitokea majira ya saa nne wao wakiwa madarasani na ndipo walipowapigia simu zimamoto kutoa taarifa ya moto huo .   Alisema waliona moto unawaka  kwenye Banda hilo wakaanza kuitana na walimu wao na kuchukua hatua ya  kuwasilina na Kikosi Cha Zima Moto na Uokozi kuja kusaida kuuzima Moto huo.   Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Chwaka tumbe Abdalla Hamad   alisema banda hilo lilikuwa linatumika kwa dharura kama kambi kwa wananfuzi wanaotarajia kufanya mitihani na hadi moto huo unazimwa hakuna mwanafunzi aliyepata majereha.   Alisema walikuwa watumia banda hilo kwa dharura kusubiri kumalizika kwa ujenzi wa Bweni unaoen...

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   MTAALAMU wa masuala ya Utafit kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii Tanzania (Economic and Social Research Foundation) Richard Ngilangwa  amewataka waandishi wa habari kuandika habari za uchunguzi na zenye ukweli ambazo zinazingatia takwimu na tafiti, ili zilete tija kwa umma.   Mtaalamu huyo aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo ya habari za Utafiti yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya ZRA Gombani Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.   Alisema, Tafiti zinafaida kubwa kwa jamii, hivyo ni vyema kwa waandishi wa habari kujikita katika eneo hilo la uwandishi wa habari za utafiti na kuzichambua kwa ajili ya kufichua shida za wananchi ili zipatiwe kwa ufumbuzi.   ‘’Tafiti zinazofanywa ni haki ya kila mmoja na sio kubakia Makabatini, hivyo zichukueni mzichambue na mziandikie zipate kujulikana, ili kama kuna jambo linahitaji kufanyika basi lifanyiwe kazi kwa urahisi na kwa wakati muafaka...

WANDISHI JISOGEZENI KWA WATAFITI, MUIBUE KERO ZA JAMII

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wandishi wa Habari wametakiwa  kuzitumia Tafiti wakati wanapoandika habari zao, ili kuibua changamoto zinazoikabili jamii na kupatikana kwa ufumbuzi wa  jambo husika.   Ushauri huo umetolewa na commissiona wa ufuatiliaji na tathmini kutoka Tume ya Mipango Zanzibar zuhura Mohd Abdallah kwa niaba ya katibu mtendaji wakati   akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, yaliyofanyika   ZRA Gombani Chakechake mkoa wa Kusini pemba. Alisema wandishi wa Habari wanasauti kubwa katika jamii, hivyo, endapo watazitumia tafiti mbalimbali zinazofanywa wakati wakiandika habari zao, wataibua matatizo yanayowakumba wanajamii   na kufanyiwa kazi kusaidia kupatikana kwa maendeleo Nchini     Aidha alisema Tume ya mipango   Zanziba imeona ipo haja kutoa mafunzo hayo ya utafiti kwa Wandishi wa habari kwani kutawaongezea uwelewa wa kufahamu mbinu za uandishi wa habari za uchambuzi, zilizo...

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZILIZOJIFICHA

Image
  Waandishi wa habari Pemba wametakia kuibua na kuandika habari zinazochangia kufanyika kwa vitendo vya udhalilishaji katika maeneo yasio maarufu (yasio tambulika).   Agizo hilo   limetolewa na Mratibu wa Mradi wa Tunaweza pamoja kutoka Tamwa Zanzibar Asya Hakim Makame   katika mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari   wa vyombo mbalimbali,yaliyofanyika Ofisi za TAMWA Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.   Alisema yapomaeneo kadhaa ambayo wanawake na watoto wamekua wakidhalilishwa kama vile kwenye usafiri wa Umma, Bandarini, Masokoni na hata katika mitandao ya kijamii, na hata kwenye viwanja vya Skukuu za Iddi.   Alisema licha ya udhalilishaji unaofanywa katika sehemu hizo, lakini bado wandishi wa habari hawaripoti, hivyo ipo haja kwa sasa kutupa jicho lao na kuibua kesi hizo, ili kuona usalama unatawala ndani ya maeneo hayo ambayo sio rasmi.   ‘’Wandishi wa habari msiishie tu kuandika udhalilishaji unaofanywa   Madrsa, Mitaani,amma...

WANANCHI WALIOCHUKULIWA ARDHI ZAO WAOMBA KULIPWA FIDIA ZAO

Image
  WANANCHI KISIWANI Pemba ambao walichukuliwa Ardhi zao kwa ajili ya Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo na Uwekezaji waliokua hawajalipwa fidia zao wameiomba Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kuwasikiliza kilio chao na kuwafuatilia ili wapate haki zao serikalini.   Akizungumza katika kikao cha Uwasilishaji wa Ripoti ya Uandaaji wa Sheria ya Sekta Miliki Zanzibar kilichofanyika Gombani Chakechake Pemba, Suleiman Mansur mwananchi wa Chakechake alisema tokea alipochukuliwa ardhi yake kwa ujenzi wa Skuli ya Uwandani bado hajalipwa fidia yake.   Alisema kila siku amekua akihangaika kwa ajili ya kutafuta haki yake, lakini ameshindwa, hivyo   aliomba Wiazara ya Ardhi kuwafuatilia kero lao na kuwaonesha njia ya kupita, ili kuona wanapata haki zao,   ‘’Kila siku nahangaishwa mara peleka barua kwa mkuu wa Wilaya mara Mkoa wala sjaona lolote, tunawaomba wenzetu wa wizara ardhi mtusaidie tupate fidia zetu,alisema. ‘’’alisema,   Kwa upande wake wakili wa kuji...

KILIMO MSITU TARAJIO LA KUJIKOMBOA NA UMSKINI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA MKURUGENZI WA Jumuia ya uhifadhi Mazingira Pemba CFP Mbarouk Mussa Omar   amezitaka kamati zinazosimamia masuala ya uhifadhi wa mazingira kuhakikisha wanaendeleza shughuli hizo ikiwemo kilimo msitu, ili kuona wanajipatia kipato. Mkurugenzi huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na wanakamati hao ambao ni kutoka shehia za Chwale, Kambini kichokochwe, Kiuyu na Mchangamdogo katika mafunzo ya siku mbili ya kuweka mikakati madhubuti ya kuendeleza shughuli za uhifadhi mazingira,yaliofanyika Ofisi za CFP huko Minyenyeni mkoa wa Kaskazini Pemba.   Alisema kilimo ndio tegemeo kubwa la Taifa, hivyo ni vyema wanakamati hao kuendelea kulima kilimo msitu, waweze kuzalisha mazao ambayo yatawasaidia kupata chakula pamoja na pesa ambazo   zitaendesha maisha yao. ‘’Ndugu zangu shughuli hizi za kulima kilimo msitu msifanye kwa sababu tu ya mradi, bali ifanyeni   kama ni kazi yenu ya kila siku, kwani mukifanya hivyo mtapata mazao mtakula nyumbani na...

TUNAANDAA SHERIA YA BIASHA KUPUNGUZA MIGOGORO YA ARDHI ''MDAMINI ANAESEMA

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanziba imesema, imo kwenye mchakato wa   kuandaa Sheria ya Biashara ya Majengo na Ardhi kwa lengo la kuimarisha sekta ya uwekezaji wa majengo pamoja na usimamizi bora wa ardhi visiwani Zanzibar.   Hayo yameelezwa na Afisa Mdhamini wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Bakar Ali Bakar katika kikao cha uwasilishaji wa ripoti ya uandaaji wa sheria ya sekta   miliki Zanzibar kilichofanyika ukumbi wa Wizara ya Fedha Gombani kisiwani Pemba.   Afisa huyo alisema kwamba Hatua hiyo inalenga kuweka mfumo rasmi wa kusimamia biashara ya nyumba, viwanja, upangishaji wa nyumba pamoja na mauzo ya mali zisizohamishika, ili kuhakikisha shughuli hizo zinafanyika kwa uwazi na kwa kufuata sheria.   ‘’Tunandaa sharia ya biashara ya Majengo na Ardhi ili kuepo na usimamizi mzuri wakati watu wanapouziana Ardhi ama kukodishana Majengo, ambapo kutaimarisha sekta ya uwekezaji Nchini,’’alisema.   Kwa upa...