Posts

HOFU YA UDHALILISHAJI MTANDAONI INAVYOWANYAMAZISHA WANAWAKE

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Katika ulimwengu wa kidijitali, mitandao ya kijamii imekuwa sauti ya wengi, ni mahali ambapo watu hujadili siasa, biashara, elimu na masuala ya kijamii.   Ingawa kwa wanawake wengi, majukwaa haya yamekuwa pia uwanja wa matusi, vitisho na udhalilishaji unaowafanya waogope kujieleza hadharani. Mara nyingi mwanamke anapotoa maoni kuhusu suala la kijamii au kisiasa, hukumbana na mashambulizi yanayolenga jinsia yake badala ya hoja aliyoitoa. Matokeo yake, baadhi yao huamua kunyamaza, kufunga akaunti au kujiondoa kabisa kwenye mijadala ya umma.   Kwa sasa Tatizo hilo linaonekana kuwa changamoto kubwa ya haki za kidijitali na usawa wa kijinsia duniani.   Utafiti wa kimataifa uliofanywa na UNESCO kwa kushirikiana na International Center for Journalists (ICFJ) mwaka 2021, uliowahusisha wanawake wanahabari 901 kutoka nchi 125, ulibaini kuwa asilimia 73 walikuwa wamewahi kukumbana na vurugu au udhalilishaji mtandaoni kutokana na kazi zao.   Utafiti ...

SERIKALI YAAHIDI KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI KWA MTOTO

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Naibu waziri wa wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Zawad Amour Nassor,  amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kupitia Wizara hiyo  imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto.   Naibu waziri huyo ameyasema hayo wakati   akifungua Kongamano la Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afirika lililofanyika Viwanja vya kufurahishia watoto Tibirinzi Chkachake mkoa wa Kusini Pemba.   Alisema Hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto katika ngazi zote, kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na lishe, kuhamasisha malezi chanya pamoja na kuendeleza ushiriki wa watoto katika masuala yanayowahusu.   ‘’Maisha bila udhalilishaji yanamaanisha mtoto kulindwa dhidi ya ukatili wa kimwili, kihisia, kingono, kutelekezwa, unyanyasaji mtandaoni, ajira za watoto na mila au desturi zinazoweza kuathiri ustawi wake,’’alisema...

ZAMECO YAITAKA SERIKALI KUHARAKISHA MSWADA WA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI ZANZIBAR

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) imeiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuharakisha mchakato wa kuuwasilisha Barazani Mswada wa Sheria ya Huduma za Habari Zanzibar ili uweze kujadiliwa na hatimaye kuwa sheria, baada ya kusubiriwa kwa zaidi ya miaka kumi. Kwa mujibu wa ZAMECO, sekta ya habari Zanzibar bado inasimamiwa na sheria mbalimbali zilizotungwa katika nyakati tofauti, hali inayosababisha kuwepo kwa mfumo wa kisheria usioendana kikamilifu na mahitaji ya sasa ya sekta hiyo pamoja na maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano. Kamati hiyo imeeleza kuwa baadhi ya sheria zilizopo zimezipa mamlaka makubwa taasisi za Serikali katika kusajili na hata kufungia vyombo vya habari, jambo ambalo linaonekana kutokidhi kikamilifu misingi ya demokrasia, uwazi na utawala bora wa sheria. Ahadi za Muda Mrefu ZAMECO imekumbusha kuwa taarifa za kukamilika kwa Mswada huo zimekuwa zikitolewa na viongozi mbalimbali wa Serikali kwa nyakati t...

TAMWA YAWAFUMBUA MACHO WANAWAKE, WANAWAKE VIJANA NA WANAWAKE WENYE ULEMAVU

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA CHAMA CHA Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZANZIBAR ), kimezindua mradi wa Wanawake Viongozi kwa ajili Usawa, Uwajibikaji na   Demokrasia( W-LEAD) unaolenga kuimarisha nafasi za uongozi na ushiriki wa wanawake, hususan wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu, katika mifumo ya kidemokrasia na kushika nafasi mbalimbali za maamuzi. Akizungumza katika uzinduzi huo kwa wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu   katika ukumbi wa Ofisi za Tamwa Mkanjuni Chakechake Pemba,   Afisa Tathmini na ufatiliaji Mohammed Khatib Mohammed alisema mradi huo utaimarisha uongozi wa wanawake , wanawake wenye ulemavu na wanawake   vijana Zanzibar. Alisema kwa   mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 wanawake wako   asilimia 51 ambao ni wengi ulkilinganisha na wanaume,   lakini katika nafasi za uongozi wanawake   ni asilimia 38 tu   idadi ambayo bado haijaridhisha ipasavyo. Alisema kwa sasa Zanzib...

BANDA LA DHARURA LA KULALA WANAFUNZI LAUNGUA MOTO

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Banda la dharura la wanafunzi 80 wa Kiume katika  Skuli ya Sekondari ya Chwaka tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, limeteketea kwa moto na kuunguza kila kitu kilichokuwemo katika jengo hilo.   Akizungumzia kutokea kwa moto huo mmoja kati ya wanafunzi wa Skuli hiyo Ibrahim Bakar Hamad alisema moto huo ulitokea majira ya saa nne wao wakiwa madarasani na ndipo walipowapigia simu zimamoto kutoa taarifa ya moto huo .   Alisema waliona moto unawaka  kwenye Banda hilo wakaanza kuitana na walimu wao na kuchukua hatua ya  kuwasilina na Kikosi Cha Zima Moto na Uokozi kuja kusaida kuuzima Moto huo.   Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Chwaka tumbe Abdalla Hamad   alisema banda hilo lilikuwa linatumika kwa dharura kama kambi kwa wananfuzi wanaotarajia kufanya mitihani na hadi moto huo unazimwa hakuna mwanafunzi aliyepata majereha.   Alisema walikuwa watumia banda hilo kwa dharura kusubiri kumalizika kwa ujenzi wa Bweni unaoen...

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   MTAALAMU wa masuala ya Utafit kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii Tanzania (Economic and Social Research Foundation) Richard Ngilangwa  amewataka waandishi wa habari kuandika habari za uchunguzi na zenye ukweli ambazo zinazingatia takwimu na tafiti, ili zilete tija kwa umma.   Mtaalamu huyo aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo ya habari za Utafiti yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya ZRA Gombani Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.   Alisema, Tafiti zinafaida kubwa kwa jamii, hivyo ni vyema kwa waandishi wa habari kujikita katika eneo hilo la uwandishi wa habari za utafiti na kuzichambua kwa ajili ya kufichua shida za wananchi ili zipatiwe kwa ufumbuzi.   ‘’Tafiti zinazofanywa ni haki ya kila mmoja na sio kubakia Makabatini, hivyo zichukueni mzichambue na mziandikie zipate kujulikana, ili kama kuna jambo linahitaji kufanyika basi lifanyiwe kazi kwa urahisi na kwa wakati muafaka...

WANDISHI JISOGEZENI KWA WATAFITI, MUIBUE KERO ZA JAMII

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wandishi wa Habari wametakiwa  kuzitumia Tafiti wakati wanapoandika habari zao, ili kuibua changamoto zinazoikabili jamii na kupatikana kwa ufumbuzi wa  jambo husika.   Ushauri huo umetolewa na commissiona wa ufuatiliaji na tathmini kutoka Tume ya Mipango Zanzibar zuhura Mohd Abdallah kwa niaba ya katibu mtendaji wakati   akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, yaliyofanyika   ZRA Gombani Chakechake mkoa wa Kusini pemba. Alisema wandishi wa Habari wanasauti kubwa katika jamii, hivyo, endapo watazitumia tafiti mbalimbali zinazofanywa wakati wakiandika habari zao, wataibua matatizo yanayowakumba wanajamii   na kufanyiwa kazi kusaidia kupatikana kwa maendeleo Nchini     Aidha alisema Tume ya mipango   Zanziba imeona ipo haja kutoa mafunzo hayo ya utafiti kwa Wandishi wa habari kwani kutawaongezea uwelewa wa kufahamu mbinu za uandishi wa habari za uchambuzi, zilizo...