MARADI WA MALEZI,MAKUZI YA AWALI YA MTOTO ULIVOBADILISHA MITAZAMO KWA WAZAZI PEMBA
NA FATMA HAMAD, PEMBA WAZAZI NA WALEZI kisiwani Pemba wamesema uwepo wa Mradi wa Malezi,Mkuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto umewasaidia, kwani wameelewa umuhumu wa kukaa karibu na watoto wao na kucheza nao. Walisema mradi umewazesha kujua kipindi cha siku 1000 ndicho kipindi pekee mtoto anachohitaji uangalizi zaidi na kuwandaliwa kuwa mtoto bora wa baadae. Akizungumza katika kikao cha tathmini juu ya mradi huo mzazi Asha kutoka N’gambwa Chake, alisema baada ya kupata elimu ya malezi na makuzi ya awali ya mtoto amejenga ukaribu na watoto wake na wamekua na uthubutu wa kuiga baadhi ya mambo ambayo wanamuona akiyafanya. ‘’Kwa mfano wakati nikiwa jikoni nikipika nilikua mtoto namuweka mbali kwani nahisi ananikera, ila kwa sasa napika nae na nikimenya mbatata yeye anamenya vitunguu,’’alisema. Kwa upande wake mzazi Kassim Masoud Hamad kutoka Piki Wete alisema zamani ilikua watoto wake hawakua na ukaribu nawala hawakisubutu kumueleza shida zao, bali ...