WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZILIZOJIFICHA
Waandishi wa habari Pemba wametakia kuibua na kuandika habari zinazochangia kufanyika kwa vitendo vya udhalilishaji katika maeneo yasio maarufu (yasio tambulika). Agizo hilo limetolewa na Mratibu wa Mradi wa Tunaweza pamoja kutoka Tamwa Zanzibar Asya Hakim Makame katika mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali,yaliyofanyika Ofisi za TAMWA Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema yapomaeneo kadhaa ambayo wanawake na watoto wamekua wakidhalilishwa kama vile kwenye usafiri wa Umma, Bandarini, Masokoni na hata katika mitandao ya kijamii, na hata kwenye viwanja vya Skukuu za Iddi. Alisema licha ya udhalilishaji unaofanywa katika sehemu hizo, lakini bado wandishi wa habari hawaripoti, hivyo ipo haja kwa sasa kutupa jicho lao na kuibua kesi hizo, ili kuona usalama unatawala ndani ya maeneo hayo ambayo sio rasmi. ‘’Wandishi wa habari msiishie tu kuandika udhalilishaji unaofanywa Madrsa, Mitaani,amma...