WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI
NA FATMA HAMAD, PEMBA MTAALAMU wa masuala ya Utafit kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii Tanzania (Economic and Social Research Foundation) Richard Ngilangwa amewataka waandishi wa habari kuandika habari za uchunguzi na zenye ukweli ambazo zinazingatia takwimu na tafiti, ili zilete tija kwa umma. Mtaalamu huyo aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo ya habari za Utafiti yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya ZRA Gombani Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema, Tafiti zinafaida kubwa kwa jamii, hivyo ni vyema kwa waandishi wa habari kujikita katika eneo hilo la uwandishi wa habari za utafiti na kuzichambua kwa ajili ya kufichua shida za wananchi ili zipatiwe kwa ufumbuzi. ‘’Tafiti zinazofanywa ni haki ya kila mmoja na sio kubakia Makabatini, hivyo zichukueni mzichambue na mziandikie zipate kujulikana, ili kama kuna jambo linahitaji kufanyika basi lifanyiwe kazi kwa urahisi na kwa wakati muafaka...