Posts

ALIANZIA UWAZIRI WA WANAWAKE NA WATOTOU WA SERIKALI YA WANAFUNZI NA SASA UKATIBU TAWALA

Image
              NA FATMA HAMAD,PEMBA   ‘’Sitoisahau siku nilioteuliwa nafasi ya  Ukatibu Tawala’’. Hayo ni maneno ya Bi Mkufu Faki Ali (51) ambae ni Katibu tawala wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba Kwa hofu aliokua  nayo mwanzoni nafasi hiyo hakuifurahia, kwani alihisi ni nafasi kubwa kwake. ‘’Watu wakipata uteuzi huwa wanafurahia, ila sikufichi  mimi sikuile ya  mwanzo nilishindwa hata kula nilikua nikilia,’’anasema. Aliteuliwa Octoba 2017 kipindi hicho alikua mfanya kazi wa Tume ya Uchaguzi  wilaya Wete Kaskazini Pemba. Nafasi hiyo ilimuia vigumu, kwani ilikua bado ni mdogo, akiangalia anaowaongoza anaona wengine ni watu wanaomzidi na anaowaheshimu ‘’Nilipokua Chuoni nilikuwa Waziri wa Wanawake na watoto na niliiweza, hivyo nikajipa moyo na hiyi nitaiweza,’’alifahamisha. Mwana mama huyo aliezaliwa mwaka 1973, kijiji cha Utaani, kwasa anaishi Kizimbani wilaya ya Wete, Safari yake ya utumishi, ilianzia katika taaluma ya ...

VIONGOZI WANAWAKE NA TISHIO LA UDHALILISHAJI

Image
                                  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wakati taifa likijivunia ongezeko la wanawake katika nafasi za maamuzi, changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia inaendelea kuwa kikwazo kinachowakatisha tamaa wanawake wengi kuingia katika siasa na uongozi.   Matusi ya mitandaoni, kejeli zinazolenga mwonekano, vitisho, lugha ya kudhalilisha na propaganda zinazolenga jinsia badala ya uwezo wa kiongozi zinaendelea kushamiri.   Licha ya kwamba hata Raisi wa Tanzania ni mwanamke bado wapo baadhi ya wanajamii wamekua na  mitazamo tofauti dhidi ya viongozi wanawake kwa kutokana na jinsia zao.   Wadau wa haki za binadamu wanaonya kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sababu matukio mengi hayaripotiwi kutokana na hofu, aibu au mila zinazowazuia waathirika kuzungumza.   WENYEWE VIONGOZI WANAWAKE WANASEMAJE JUU YA HILI   Mkufu Faki Ali ni Katibu taw...

HADIA OMAR DADI, SHEHA WINGWI NJUGUNI KIONGOZI DHAHABU KWA WANANCHI WAKE

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Katika miaka ya hivi karibuni, ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi, unaendelea kupewa kipaumbele nchini Tanzania na Zanzibar.  Kupitia Katiba, sera za usawa wa kijinsia pamoja na mikataba ya kimataifa kama Mkataba wa CEDAW na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG 5), ambayo yanasisitiza ushiriki sawa wa wanawake katika uongozi na maamuzi ya maendeleo.   Kwa muda mrefu, nafasi za uongozi zinaonekana kuwa ni za wanaume zaidi, ingawa wanawake wengi wanaendelea kuthibitisha kuwa wana uwezo mkubwa wa kusimamia maendeleo ya jamii pale wanapopewa nafasi.    Miongoni mwao ni Sheha wa Njuguni, Bi Hadia Omar Dadi, (48) mzaliwa wa Wingwi, ambaye wananchi wengi wanamwelezea kama kiongozi anayesikiliza, anayeshirikiana na jamii na anayesimamia maendeleo kwa vitendo.   Safari ya Hadia Omar Dadi, haikuanza alipoteuliwa kuwa sheha, ilianza akiwa mwanachama wa kikundi cha ushirika katika jamii yake.   Bi Hadia, kwa sasa anaishi kij...