Posts

VIONGOZI WANAWAKE NA TISHIO LA UDHALILISHAJI

Image
                                  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wakati taifa likijivunia ongezeko la wanawake katika nafasi za maamuzi, changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia inaendelea kuwa kikwazo kinachowakatisha tamaa wanawake wengi kuingia katika siasa na uongozi.   Matusi ya mitandaoni, kejeli zinazolenga mwonekano, vitisho, lugha ya kudhalilisha na propaganda zinazolenga jinsia badala ya uwezo wa kiongozi zinaendelea kushamiri.   Licha ya kwamba hata Raisi wa Tanzania ni mwanamke bado wapo baadhi ya wanajamii wamekua na  mitazamo tofauti dhidi ya viongozi wanawake kwa kutokana na jinsia zao.   Wadau wa haki za binadamu wanaonya kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sababu matukio mengi hayaripotiwi kutokana na hofu, aibu au mila zinazowazuia waathirika kuzungumza.   WENYEWE VIONGOZI WANAWAKE WANASEMAJE JUU YA HILI   Mkufu Faki Ali ni Katibu taw...

HADIA OMAR DADI, SHEHA WINGWI NJUGUNI KIONGOZI DHAHABU KWA WANANCHI WAKE

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Katika miaka ya hivi karibuni, ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi, unaendelea kupewa kipaumbele nchini Tanzania na Zanzibar.  Kupitia Katiba, sera za usawa wa kijinsia pamoja na mikataba ya kimataifa kama Mkataba wa CEDAW na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG 5), ambayo yanasisitiza ushiriki sawa wa wanawake katika uongozi na maamuzi ya maendeleo.   Kwa muda mrefu, nafasi za uongozi zinaonekana kuwa ni za wanaume zaidi, ingawa wanawake wengi wanaendelea kuthibitisha kuwa wana uwezo mkubwa wa kusimamia maendeleo ya jamii pale wanapopewa nafasi.    Miongoni mwao ni Sheha wa Njuguni, Bi Hadia Omar Dadi, (48) mzaliwa wa Wingwi, ambaye wananchi wengi wanamwelezea kama kiongozi anayesikiliza, anayeshirikiana na jamii na anayesimamia maendeleo kwa vitendo.   Safari ya Hadia Omar Dadi, haikuanza alipoteuliwa kuwa sheha, ilianza akiwa mwanachama wa kikundi cha ushirika katika jamii yake.   Bi Hadia, kwa sasa anaishi kij...

WANAWAKE WENYEULEMAVU WASHIKA MKIA KWENYE KAMATI ZA SHEHIA

Image
                     NA FATMA HAMAD, PEMBA                                                  WATU WENYE ulemavu, wana haki ya kushirikishwa katika nyanja zote za kiuchumi, kama raia wote, bila ya kujali ulemavu wao, maana kinachoangaliwa sio ulemavu bali ni haki zao na uwezo wao . Na ndio maana, serikali, ikaweka muongozo maalumu, ili maendeleo ya nchi yasiwaache nyuma kwa kuimarisha muundo wa tasisi za watu wenye ulemavu.  Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD), wa mwaka 2006 Ibara ya 29   unahimiza serikali, kuhakikisha ushiriki sawa wa watu wenye ulemavu katika siasa na maamuzi. Hata Katiba ya Zanzibar ya 1984, ambayo ndo sheria mama, kupitia kifungu chake cha 21(1) nacho kinatambua haki ya kila raia kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi bila ubaguzi. Sh...