‘’TUTAHAKIKISHA TUNAULINDA UTAMADUNI WA ZANZIBAR’’ANASEMA HEMED
NA FATMA HAMAD, PEMBA SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itahakikisha inafanya juhudi mbalimbali kuona utamaduni wa mzanzibari unadumu, ili uweze kuinua uchumi wa vijana wa kizanzibari. Hayo yalisemwa na Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Hemedi Suleiman Abdulla kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Ali Hassan Mwinyi, wakati akizindua Tamasha la 31 la Utamaduni wa Mzanzibar, huko Gombani wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema Utamaduni wa kizanzibar ni moja ya jambo linalochangia uchumi wa Nchi, hiivyo ipo haja kuendeleza Utamaduni huo ili kuleta ajira kwa vijana wa Zanzibar. ‘’Tutahakikisha tunaulinda utamaduni wetu uweze kudumu, na kuwa kivutio kwa wageni wanaoingia Zanzibar,'alisema. Alisema Serikali imeshetenga Bilioni 40 kwaajili ya kujenga kijiji cha utamaduni ili wazanzibari wakuze bidhaa zao za kiutamaduni kamavile mapishi ya asili, ikiwemo Vitobwesha, Mkate wa gae, Ugali wa muhogo pamoja na Msambwija ( muhogo wa ndizi). ...