UCHUMI WA BULUU YAJA NA MRADI WA KUIMARISHA UVUVI ENDELEVU
Sekta ya uvuvi, ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani iznaendelea kuwa nguzo muhimu ya ajira na kipato kwa wananchi wa Zanzibar huku Serikali na taasisi binafsi ikiweka mkazo katika matumizi ya rasilimali za baharini kama fursa ya biashara na uwekezaji. Hayo yalisemwa na Afisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Buluu DK Salim Mohamed Hamza wakati akizungumza katika mkutano wa wadau wa Mradi wa Kuimarisha Uvuvi Endelevu na Ufugaji wa Mazao ya Baharini Tanzania, TASFAM, huko katika ukumbi wa ZRA Gombani Chakechake Kusini Pemba. Alisemesema ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kuongeza uzalishaji, ajira na kipato kwa wananchi. ALisema kwa Sasa serikali imeelekeza zaidi katika sekta ya Bahari, hivyo imeamua kuleta Mardi huo wa kuimarisha usimamizi endelevu wa uvuvi na ufugaji wa mazao baharini, ili wadau waunge mkono Mradi huo na lile lengo la serikali liweze kutimia la kujipatia kipato kupitia Bahari. "Nyinyi wadau mnaoshughulika na masuala ya Bahari mnamchango maku...