ZRA yafanya mabadiliko Sheria za Kodi
NA ZUHURA JUMA, PEMBA SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imekuwa ikifanya mabadiliko ya Sheria za kodi, ili kuleta unafuu kwa walipakodi sambamba na kupatikana kodi vizuri. Akizungumzia Sheria zilizofanyiwa maboresho, Ofisa Kitengo cha Habari, Uhusiano na Huduma kwa Walipa Kodi, kutoka Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA), Makame Khamis Mohamed alisema, kabla ya kurekebishwa Sheria, Serikali hufanya utafiti kwanza ili zisimuathiri mlipakodi wala Serikali. Alisema kuwa, hatua hiyo ya kuzifanyia maboresho Sheria za kodi ni katika kuwajali wananchi wake, kwani kuna baadhi ya vitu vimeondolewa ushuru na vyengine vimepunguzwa kwa asilimia 25, jambo ambalo litasaidia sana katika kuboresha utekelezaji wao wa majukumu, pamoja na kuleta unafuu kwa walipakodi. “Mabadiliko haya yamekuja kuleta unafuu kwa walipakodi na wananchi kwa ujumla, hivyo kama waandishi wa habari tunapaswa kuuhabarisha umma, ili waelewe maboresho haya na kuyafanyia kazi,” alisema Makame. Alieleza kuwa, lengo la kufanyia mabor...