VIONGOZI WANAWAKE NA TISHIO LA UDHALILISHAJI
NA FATMA HAMAD, PEMBA Wakati taifa likijivunia ongezeko la wanawake katika nafasi za maamuzi, changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia inaendelea kuwa kikwazo kinachowakatisha tamaa wanawake wengi kuingia katika siasa na uongozi. Matusi ya mitandaoni, kejeli zinazolenga mwonekano, vitisho, lugha ya kudhalilisha na propaganda zinazolenga jinsia badala ya uwezo wa kiongozi zinaendelea kushamiri. Licha ya kwamba hata Raisi wa Tanzania ni mwanamke bado wapo baadhi ya wanajamii wamekua na mitazamo tofauti dhidi ya viongozi wanawake kwa kutokana na jinsia zao. Wadau wa haki za binadamu wanaonya kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sababu matukio mengi hayaripotiwi kutokana na hofu, aibu au mila zinazowazuia waathirika kuzungumza. WENYEWE VIONGOZI WANAWAKE WANASEMAJE JUU YA HILI Mkufu Faki Ali ni Katibu taw...