Posts

UCHUMI WA BULUU YAJA NA MRADI WA KUIMARISHA UVUVI ENDELEVU

Image
Sekta ya uvuvi, ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani iznaendelea kuwa nguzo muhimu ya ajira na kipato kwa wananchi wa Zanzibar huku Serikali na taasisi binafsi ikiweka mkazo katika matumizi ya rasilimali za baharini kama fursa ya biashara na uwekezaji.   Hayo yalisemwa na Afisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Buluu DK Salim Mohamed Hamza wakati akizungumza katika mkutano wa wadau wa Mradi wa Kuimarisha Uvuvi Endelevu na Ufugaji wa Mazao ya Baharini Tanzania, TASFAM, huko katika ukumbi wa ZRA Gombani Chakechake Kusini Pemba.  Alisemesema ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kuongeza uzalishaji, ajira na kipato kwa wananchi. ALisema kwa Sasa serikali imeelekeza zaidi katika sekta ya Bahari, hivyo imeamua kuleta Mardi huo wa kuimarisha usimamizi endelevu wa uvuvi na ufugaji wa mazao baharini, ili wadau waunge mkono Mradi huo na lile lengo la serikali liweze kutimia la kujipatia kipato kupitia Bahari.  "Nyinyi wadau mnaoshughulika na masuala ya Bahari mnamchango maku...

WAVUVI WATAKIWA KUTUMIA ZANA MBADALA KULINDA RASILIMALI BAHARI

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   AFISA MRADI wa Kuimarisha Uvuvi endelevu na usimamizi wa Mazao ya Bahari TASFAM Salma Sururu Juma amewataka wananchi wanaofanya shughuli za  Uvuvi kuhakikisha wanafanya shughuli hizo wanatumia zana za kisasa ambazo zinaruhusiwa kisheria, ili kulindavrasilimali za Bahari na kuona zinakua endelevu. Wito huo meutoa wakati akizungumza na Maafis Uvuvi na wadau wanaosimamia shughuli za Uvuvi, katika mkutano wa kuutanbulisha Mardi huo wa kuimarisha Uvuvi endelevu na usimamizi wa Mazao ya Baharini TASFAM huko ukumbi wa wizara ya Fedh Gombani Chakechake Kusini Pemba.  Alisema bila kutumia  zana za kisasa na zinazokubalika kisheria, sio rahisi rasilimali Bahari zikaweza kuhifadhika na kua endelevu. Alisema lengo la Mardi huo ni kuhivadhi Mazao ya Bahari, hivyo ipo haja kwa maafisa Uvuvi kusimamia ipasavyo kuona wavuvi na wanaofanya shughuli za abaharini kuwa na zana zinazokubalika, ili lengo liweze kulengo lifikiwe na kuona serikali inaingiza ki...

ZRA yafanya mabadiliko Sheria za Kodi

Image
  NA ZUHURA JUMA, PEMBA SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imekuwa ikifanya mabadiliko ya Sheria za kodi, ili kuleta unafuu kwa walipakodi sambamba na kupatikana kodi vizuri. Akizungumzia Sheria zilizofanyiwa maboresho, Ofisa Kitengo cha Habari, Uhusiano na Huduma kwa Walipa Kodi, kutoka Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA), Makame Khamis Mohamed alisema, kabla ya kurekebishwa Sheria, Serikali hufanya utafiti kwanza ili zisimuathiri mlipakodi wala Serikali. Alisema kuwa, hatua hiyo ya kuzifanyia maboresho Sheria za kodi ni katika kuwajali wananchi wake, kwani kuna baadhi ya vitu vimeondolewa ushuru na vyengine vimepunguzwa kwa asilimia 25, jambo ambalo litasaidia sana katika kuboresha utekelezaji wao wa majukumu, pamoja na kuleta unafuu kwa walipakodi. “Mabadiliko haya yamekuja kuleta unafuu kwa walipakodi na wananchi kwa ujumla, hivyo kama waandishi wa habari tunapaswa kuuhabarisha umma, ili waelewe maboresho haya na kuyafanyia kazi,” alisema Makame. Alieleza kuwa, lengo la kufanyia mabor...

NAJIVUNIA KUONA WANANCHI WA MJINI KIUYU WAKIKANYAGA BARABARA YA LAMI

Image
                                          NA FATMA HAMAD, PEMBA                                                                                                                             ‘’Ama kweli mwenye kutafuta haachi kupata’’ Msemo huo umesadilifu kwa Nassra  Salim Mohamed Diwani mstaaf wa wadi ya Kiuyu Minungwini wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba. MAISHA YA NASRA Baada ya kuzaliwa  1969, Nasra alianza kuisaka haki ya elimu ya msingi mwaka 1976 katika skuli ya msingi Piki wilaya Wete. Akiwa darasani, Nasra hakuwa mtulivu na jinsia yake ya kike, wak...

ALIANZIA UWAZIRI WA WANAWAKE NA WATOTO WA SERIKALI YA WANAFUNZI NA SASA UKATIBU TAWALA

Image
              NA FATMA HAMAD,PEMBA   ‘’Sitoisahau siku nilioteuliwa nafasi ya  Ukatibu Tawala’’. Hayo ni maneno ya Bi Mkufu Faki Ali (51) ambae ni Katibu tawala wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba Kwa hofu aliokua  nayo mwanzoni nafasi hiyo hakuifurahia, kwani alihisi ni nafasi kubwa kwake. ‘’Watu wakipata uteuzi huwa wanafurahia, ila sikufichi  mimi sikuile ya  mwanzo nilishindwa hata kula nilikua nikilia,’’anasema. Aliteuliwa Octoba 2017 kipindi hicho alikua mfanya kazi wa Tume ya Uchaguzi  wilaya Wete Kaskazini Pemba. Nafasi hiyo ilimuia vigumu, kwani ilikua bado ni mdogo, akiangalia anaowaongoza anaona wengine ni watu wanaomzidi na anaowaheshimu ‘’Nilipokua Chuoni nilikuwa Waziri wa Wanawake na watoto na niliiweza, hivyo nikajipa moyo na hiyi nitaiweza,’’alifahamisha. Mwana mama huyo aliezaliwa mwaka 1973, kijiji cha Utaani, kwasa anaishi Kizimbani wilaya ya Wete, Safari yake ya utumishi, ilianzia katika taaluma ya ...

VIONGOZI WANAWAKE NA TISHIO LA UDHALILISHAJI

Image
                                  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wakati taifa likijivunia ongezeko la wanawake katika nafasi za maamuzi, changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia inaendelea kuwa kikwazo kinachowakatisha tamaa wanawake wengi kuingia katika siasa na uongozi.   Matusi ya mitandaoni, kejeli zinazolenga mwonekano, vitisho, lugha ya kudhalilisha na propaganda zinazolenga jinsia badala ya uwezo wa kiongozi zinaendelea kushamiri.   Licha ya kwamba hata Raisi wa Tanzania ni mwanamke bado wapo baadhi ya wanajamii wamekua na  mitazamo tofauti dhidi ya viongozi wanawake kwa kutokana na jinsia zao.   Wadau wa haki za binadamu wanaonya kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sababu matukio mengi hayaripotiwi kutokana na hofu, aibu au mila zinazowazuia waathirika kuzungumza.   WENYEWE VIONGOZI WANAWAKE WANASEMAJE JUU YA HILI   Mkufu Faki Ali ni Katibu taw...