TAMWA YAWAFUMBUA MACHO WANAWAKE, WANAWAKE VIJANA NA WANAWAKE WENYE ULEMAVU
NA FATMA HAMAD, PEMBA CHAMA CHA Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZANZIBAR ), kimezindua mradi wa Wanawake Viongozi kwa ajili Usawa, Uwajibikaji na Demokrasia( W-LEAD) unaolenga kuimarisha nafasi za uongozi na ushiriki wa wanawake, hususan wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu, katika mifumo ya kidemokrasia na kushika nafasi mbalimbali za maamuzi. Akizungumza katika uzinduzi huo kwa wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu katika ukumbi wa Ofisi za Tamwa Mkanjuni Chakechake Pemba, Afisa Tathmini na ufatiliaji Mohammed Khatib Mohammed alisema mradi huo utaimarisha uongozi wa wanawake , wanawake wenye ulemavu na wanawake vijana Zanzibar. Alisema kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 wanawake wako asilimia 51 ambao ni wengi ulkilinganisha na wanaume, lakini katika nafasi za uongozi wanawake ni asilimia 38 tu idadi ambayo bado haijaridhisha ipasavyo. Alisema kwa sasa Zanzib...