WANAHABARI, WADAU WAOMBA VIFUNGU VINAVYOMINYA UHURU WA HABARI VIREKEBISHWE
NA FATMA HAMAD,PEMBA KILA baada ya miaka 10 sheria huwa zinahitaji kubadilishwa ili kuondosha mapungufu ya vifungu ambavyo vitakua haviendani na utekelezaji wa sheria hiyo. Ijapo kuwa wakati mwengine sio lazima kusubiriwe hadi itimie miaka 10 ndio iweze kufanyiwa marekebisho. Na hii itasaidia kuweka sawa vifungu vyenye mapungufu ili viweze kuendana na muda na mazingira ya sasa. Lakini tukiangalia sheria ya Usajili wa Uwakala wa habari, Magazeti na Vitabu namba 5 ya mwaka 1988 iliyofanywa marekebisho na Sheria Namba 8 ya mwaka 1997, haiendani na mazingira ya sasa kwani ni kongwe hivyo inahitajika ifanyiwe marekebisho. Takriban ni miaka 26 tangu Sheria hiyo kufanyiwa marekebisho ingawa bado baadhi ya vifungu vyake vina mapungufu ambavyo vinaminya uhuru habari. Miongoni mwa vifungu hivyo ni kifungu cha 30 kinachompa mamlaka makubwa Waziri kiasi ambacho kinaminya uhuru wa habari pamoja na kifungu cha 27[1], 27[2]. A