Posts

WANDISHI WA HABARI IELIMISHENI JAMII MATUMIZI YA MITANDAO

Image
  NA FATMA HAMAD,PEMBA MTAALAMU WA Masuwala ya Mitandao ua Kijamii kisiwani Pemba Mustafa Mohd Abdul Rabi Moyo amewataka Wandishi wa Habari kuendelea kuielimisha jaamii  hususani  ya wanawake, kufuata  miko na maadili ya mitandao, ili kuepuka kufanyiwa udhalilishaji  mitandaoni. Mtaalamu huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Chakechake Pemba, alisema imeonekana jamii haina elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya mitandao, hivyo ipo haja wandishi wa habari kutoa elimu, ili kuepuka udhalilishaji huo. Alisema kutokana na kuzuka kwa wimbi la udhalilishaji katika mitandao ya kijamii kwa wanawake, ni budi jamii kuelimika na kufahamu madhara ya udhalilishaji mtandaoni. Alisema kwa sasa udhalilishaji ambao unatumika zaidi  katika mitandao ni wa mashambulizi ya matusi, na huu unakuja pale mwanamke anapotuma  picha za maungo yake  yakiwa utupu. ‘’Niwambie tu dada zangu, licha kua mnatangaza biashara zenu i...

JINSI MICHEWENI ILIVYOWAOKOA WATOTO DHIDI YA AJIRA ZA UTOTONI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Miaka iliyopita, katika baadhi ya vijiji vya Micheweni, ilikuwa kawaida, kumuona mtoto mwenye umri mdogo akiwa shambani, bandarini au sokoni badala ya kuwa darasani.   Wengine walikuwa wakibeba mizigo, kuvua samaki, kuuza bidhaa au kufanya kazi za nyumbani kwa muda mrefu, huku ndoto zao za elimu zikififia taratibu.   Ingawa kupitia ushirikiano kati ya serikali ya wilaya, kamati za skuli, walimu, wazazi, viongozi wa dini pamoja na mashirika ya kutetea haki za watoto, Micheweni inaanza kushuhudia mwanga mpya katika mapambano dhidi ya ajira za watoto. Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, anasema kwa miaka ya sasa Micheweni, inaanza kuandika historia mpya, tofauti na zamani ambapo watoto wengi walionekana mashambani na bandarini,   wengi wao wanaonekana wakiwa madarasani wakijenga ndoto zao.   Sheha wa Sizini Suleiman Shaame Hamad anasema mkakati umezaa matunda kwani   kuanzia mwaka 2023 hadi 2025   Shehia yake peke...

HOFU YA UDHALILISHAJI MTANDAONI INAVYOWANYAMAZISHA WANAWAKE

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Katika ulimwengu wa kidijitali, mitandao ya kijamii imekuwa sauti ya wengi, ni mahali ambapo watu hujadili siasa, biashara, elimu na masuala ya kijamii.   Ingawa kwa wanawake wengi, majukwaa haya yamekuwa pia uwanja wa matusi, vitisho na udhalilishaji unaowafanya waogope kujieleza hadharani. Mara nyingi mwanamke anapotoa maoni kuhusu suala la kijamii au kisiasa, hukumbana na mashambulizi yanayolenga jinsia yake badala ya hoja aliyoitoa. Matokeo yake, baadhi yao huamua kunyamaza, kufunga akaunti au kujiondoa kabisa kwenye mijadala ya umma.   Kwa sasa Tatizo hilo linaonekana kuwa changamoto kubwa ya haki za kidijitali na usawa wa kijinsia duniani.   Utafiti wa kimataifa uliofanywa na UNESCO kwa kushirikiana na International Center for Journalists (ICFJ) mwaka 2021, uliowahusisha wanawake wanahabari 901 kutoka nchi 125, ulibaini kuwa asilimia 73 walikuwa wamewahi kukumbana na vurugu au udhalilishaji mtandaoni kutokana na kazi zao.   Utafiti ...