Mkurugenzi wa TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia
NA MWANDISHI WETU Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar. “Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio ng...