WANDISHI WA HABARI IELIMISHENI JAMII MATUMIZI YA MITANDAO
NA FATMA HAMAD,PEMBA MTAALAMU WA Masuwala ya Mitandao ua Kijamii kisiwani Pemba Mustafa Mohd Abdul Rabi Moyo amewataka Wandishi wa Habari kuendelea kuielimisha jaamii hususani ya wanawake, kufuata miko na maadili ya mitandao, ili kuepuka kufanyiwa udhalilishaji mitandaoni. Mtaalamu huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Chakechake Pemba, alisema imeonekana jamii haina elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya mitandao, hivyo ipo haja wandishi wa habari kutoa elimu, ili kuepuka udhalilishaji huo. Alisema kutokana na kuzuka kwa wimbi la udhalilishaji katika mitandao ya kijamii kwa wanawake, ni budi jamii kuelimika na kufahamu madhara ya udhalilishaji mtandaoni. Alisema kwa sasa udhalilishaji ambao unatumika zaidi katika mitandao ni wa mashambulizi ya matusi, na huu unakuja pale mwanamke anapotuma picha za maungo yake yakiwa utupu. ‘’Niwambie tu dada zangu, licha kua mnatangaza biashara zenu i...