BANDA LA DHARURA LA KULALA WANAFUNZI LAUNGUA MOTO
NA FATMA HAMAD, PEMBA Banda la dharura la wanafunzi 80 wa Kiume katika Skuli ya Sekondari ya Chwaka tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, limeteketea kwa moto na kuunguza kila kitu kilichokuwemo katika jengo hilo. Akizungumzia kutokea kwa moto huo mmoja kati ya wanafunzi wa Skuli hiyo Ibrahim Bakar Hamad alisema moto huo ulitokea majira ya saa nne wao wakiwa madarasani na ndipo walipowapigia simu zimamoto kutoa taarifa ya moto huo . Alisema waliona moto unawaka kwenye Banda hilo wakaanza kuitana na walimu wao na kuchukua hatua ya kuwasilina na Kikosi Cha Zima Moto na Uokozi kuja kusaida kuuzima Moto huo. Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Chwaka tumbe Abdalla Hamad alisema banda hilo lilikuwa linatumika kwa dharura kama kambi kwa wananfuzi wanaotarajia kufanya mitihani na hadi moto huo unazimwa hakuna mwanafunzi aliyepata majereha. Alisema walikuwa watumia banda hilo kwa dharura kusubiri kumalizika kwa ujenzi wa Bweni unaoen...