Posts

WANANCHI WALIOCHUKULIWA ARDHI ZAO WAOMBA KULIPWA FIDIA ZAO

Image
  WANANCHI KISIWANI Pemba ambao walichukuliwa Ardhi zao kwa ajili ya Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo na Uwekezaji waliokua hawajalipwa fidia zao wameiomba Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kuwasikiliza kilio chao na kuwafuatilia ili wapate haki zao serikalini.   Akizungumza katika kikao cha Uwasilishaji wa Ripoti ya Uandaaji wa Sheria ya Sekta Miliki Zanzibar kilichofanyika Gombani Chakechake Pemba, Suleiman Mansur mwananchi wa Chakechake alisema tokea alipochukuliwa ardhi yake kwa ujenzi wa Skuli ya Uwandani bado hajalipwa fidia yake.   Alisema kila siku amekua akihangaika kwa ajili ya kutafuta haki yake, lakini ameshindwa, hivyo   aliomba Wiazara ya Ardhi kuwafuatilia kero lao na kuwaonesha njia ya kupita, ili kuona wanapata haki zao,   ‘’Kila siku nahangaishwa mara peleka barua kwa mkuu wa Wilaya mara Mkoa wala sjaona lolote, tunawaomba wenzetu wa wizara ardhi mtusaidie tupate fidia zetu,alisema. ‘’’alisema,   Kwa upande wake wakili wa kuji...

KILIMO MSITU TARAJIO LA KUJIKOMBOA NA UMSKINI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA MKURUGENZI WA Jumuia ya uhifadhi Mazingira Pemba CFP Mbarouk Mussa Omar   amezitaka kamati zinazosimamia masuala ya uhifadhi wa mazingira kuhakikisha wanaendeleza shughuli hizo ikiwemo kilimo msitu, ili kuona wanajipatia kipato. Mkurugenzi huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na wanakamati hao ambao ni kutoka shehia za Chwale, Kambini kichokochwe, Kiuyu na Mchangamdogo katika mafunzo ya siku mbili ya kuweka mikakati madhubuti ya kuendeleza shughuli za uhifadhi mazingira,yaliofanyika Ofisi za CFP huko Minyenyeni mkoa wa Kaskazini Pemba.   Alisema kilimo ndio tegemeo kubwa la Taifa, hivyo ni vyema wanakamati hao kuendelea kulima kilimo msitu, waweze kuzalisha mazao ambayo yatawasaidia kupata chakula pamoja na pesa ambazo   zitaendesha maisha yao. ‘’Ndugu zangu shughuli hizi za kulima kilimo msitu msifanye kwa sababu tu ya mradi, bali ifanyeni   kama ni kazi yenu ya kila siku, kwani mukifanya hivyo mtapata mazao mtakula nyumbani na...

TUNAANDAA SHERIA YA BIASHA KUPUNGUZA MIGOGORO YA ARDHI ''MDAMINI ANAESEMA

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanziba imesema, imo kwenye mchakato wa   kuandaa Sheria ya Biashara ya Majengo na Ardhi kwa lengo la kuimarisha sekta ya uwekezaji wa majengo pamoja na usimamizi bora wa ardhi visiwani Zanzibar.   Hayo yameelezwa na Afisa Mdhamini wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Bakar Ali Bakar katika kikao cha uwasilishaji wa ripoti ya uandaaji wa sheria ya sekta   miliki Zanzibar kilichofanyika ukumbi wa Wizara ya Fedha Gombani kisiwani Pemba.   Afisa huyo alisema kwamba Hatua hiyo inalenga kuweka mfumo rasmi wa kusimamia biashara ya nyumba, viwanja, upangishaji wa nyumba pamoja na mauzo ya mali zisizohamishika, ili kuhakikisha shughuli hizo zinafanyika kwa uwazi na kwa kufuata sheria.   ‘’Tunandaa sharia ya biashara ya Majengo na Ardhi ili kuepo na usimamizi mzuri wakati watu wanapouziana Ardhi ama kukodishana Majengo, ambapo kutaimarisha sekta ya uwekezaji Nchini,’’alisema.   Kwa upa...
Image
   Kiungoni walia na huduma ya Maji NA FATMA HAMAD, PEMBA WANACHI WA SHEHIA ya Kiuongoni wilaya ya Wete Kaskazini Pemba   wamelalamikia juu ya kadhiya inayowakabili, ya   ukosefu wa huduma za Maji safi na salama kijijini mwao. Wananchi hao walisema tokea ulipoanza ujenzi wa barabara suala la Maji   ya Zawa   vijijini   mwao imekua ni kama ndoto, jambo linalopelekea usumbufu wa kutafuta huduma hiyo maeneo ya mbali. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi   huko kijijini kwao, kiungoni mwananchi Zainab Abdallah Hassan na Ngindo Kombo Faki   walisema   wanategemea huduma ya maji kupitia Kisima cha Msikitini, ambapo kupandishwa   kwake kwenye Tenki ni nadra, kwani hadi wananchi walipie pesa ndio yapandiswhe.   ‘’ Hayo maji tunayotegemea hapo msikitini hayapatikani kama wananchi hawajachanga pesa, hivyo kupatikana kwake ni shida,’ walisema. Walisema kuwa tatizo hilo limeshakua kubwa na linahitaji kuwangaliwa, kwani waka...

Mkurugenzi wa TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia

Image
  NA MWANDISHI WETU Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar. “Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio ng...

UNYANYAPAA ADUI ASIEONEKANA KWA WAGONJWA WA KIFUA KIKUU

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   NI kawaida ya binadamu walio wengi wanapoumwa hunasibisha maradhi yao na imani za kishirikina.   Na aina hii ya watu hawasikii, hawaoni wala hawashauriki kuhusu huduma za hospitali na hatimae kuangukia kwenye waganga wa kienyeji.   Ingawa baadhi yao huelekeza imani zao kwengine baada ya kuona huduma za hospitali hazikuzaa matunda huku wakiwa wanaripoti kila wanapopangiwa.   Ugonjwa wa kifua kikuu ni moja ya ugonjwa ambao watu wengi huelekeza imani zao kwengine kutokana na jinsi unavyokuja huku ukiwa dalili za mwanzo kutoonekana.   ‘’Kila siku unapoenda hospitali ukisema unaumwa na kifua unapewa dawa tu bila kupimwa, hivyo hali ikiendelea kudhoofu mtu anajiona kama tayari ana magonjwa mengine ya kishirikina,’’ alisema mwananchi Faida Hassan mkaazi wa Finya Wilaya ya Wete,  Anasema, wakati mwengine kutokufanyiwa vipimo ndipo kunakosababisha watu wengi kukimbilia kwa waganga wa kienyeji, jambo ambalo linaweza kuhatarish...

JAMII YAHIMIZWA KUITUNZA AMANI ILIYOPO NCHINI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA Viongozi wa kamati za  dini mbali mbali kisiwani Pemba (Pemba Interfaith Committee) wameipongeza jamii ya  wazanzibari kwa kuendelea kuishi kwa umoja na mshikamano, jambo lililoifanya Zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu na utulivu. Akitoa tamko la kamati hiyo katika kikao cha kufanya tathmini ya juhudi zilizofanywa na kamati hiyo za kushajihisha amani  kabla, wakati na baadhi ya uchaguzi mkuu uliofanyika Zanzibar mwenzi Oktaba mwaka huu, Mwenyekiti wa kamati ya dini mbali mbali kwa upande wa wanawake Amina Salim Ahmed  katika ukumbi wa mikutano wa Samail Gombani Pemba aliipongeza jamii ya kwa kuendelea kuishi kwa umoja na mshikamano jambo lililoifanya zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu. Alisema hali hiyo ilikuja kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na viongozi wa dini, Serikali, na wananchi katika kudumisha misingi ya maelewano ambayo imeijenga Zanzibar. Alieleza tamko hili ni mwendelezo wa wito wa kila mara unaosisitiza kwamba amani ...