WANANCHI WALIOCHUKULIWA ARDHI ZAO WAOMBA KULIPWA FIDIA ZAO
WANANCHI KISIWANI Pemba ambao walichukuliwa Ardhi zao kwa ajili ya Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo na Uwekezaji waliokua hawajalipwa fidia zao wameiomba Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kuwasikiliza kilio chao na kuwafuatilia ili wapate haki zao serikalini. Akizungumza katika kikao cha Uwasilishaji wa Ripoti ya Uandaaji wa Sheria ya Sekta Miliki Zanzibar kilichofanyika Gombani Chakechake Pemba, Suleiman Mansur mwananchi wa Chakechake alisema tokea alipochukuliwa ardhi yake kwa ujenzi wa Skuli ya Uwandani bado hajalipwa fidia yake. Alisema kila siku amekua akihangaika kwa ajili ya kutafuta haki yake, lakini ameshindwa, hivyo aliomba Wiazara ya Ardhi kuwafuatilia kero lao na kuwaonesha njia ya kupita, ili kuona wanapata haki zao, ‘’Kila siku nahangaishwa mara peleka barua kwa mkuu wa Wilaya mara Mkoa wala sjaona lolote, tunawaomba wenzetu wa wizara ardhi mtusaidie tupate fidia zetu,alisema. ‘’’alisema, Kwa upande wake wakili wa kuji...