WANDISHI JISOGEZENI KWA WATAFITI, MUIBUE KERO ZA JAMII
NA FATMA HAMAD, PEMBA Wandishi wa Habari wametakiwa kuzitumia Tafiti wakati wanapoandika habari zao, ili kuibua changamoto zinazoikabili jamii na kupatikana kwa ufumbuzi wa jambo husika. Ushauri huo umetolewa na commissiona wa ufuatiliaji na tathmini kutoka Tume ya Mipango Zanzibar zuhura Mohd Abdallah kwa niaba ya katibu mtendaji wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, yaliyofanyika ZRA Gombani Chakechake mkoa wa Kusini pemba. Alisema wandishi wa Habari wanasauti kubwa katika jamii, hivyo, endapo watazitumia tafiti mbalimbali zinazofanywa wakati wakiandika habari zao, wataibua matatizo yanayowakumba wanajamii na kufanyiwa kazi kusaidia kupatikana kwa maendeleo Nchini Aidha alisema Tume ya mipango Zanziba imeona ipo haja kutoa mafunzo hayo ya utafiti kwa Wandishi wa habari kwani kutawaongezea uwelewa wa kufahamu mbinu za uandishi wa habari za uchambuzi, zilizo...