Posts

WANAWAKE WENYEULEMAVU WASHIKA MKIA KWENYE KAMATI ZA SHEHIA

Image
         NA FATMA HAMAD, PEMBA WATU WENYE ulemavu, wana haki ya kushirikishwa katika nyanja zote za kiuchumi, kama raia wote, bila ya kujali ulemavu wao, maana kinachoangaliwa sio ulemavu bali ni haki zao na uwezo wao. Na ndio maana, serikali, ikaweka muongozo maalumu, ili maendeleo ya nchi yasiwaache nyuma kwa kuimarisha muundo wa tasisi za watu wenye ulemavu.   Tanzania imeridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD), wa mwaka 2006 unahimiza serikali, kuhakikisha ushiriki sawa wa watu wenye ulemavu katika siasa na maamuzi. Katiba ya Zanzibar ya 1984, Kifungu kidogo cha 3 kinaeleza kwamba, kila mzanzibari anayohaki ya kushika nafasi yoyote ya kazi na shughuli yoyote iliyoko chini ya mamlaka ya Zanzibar. Sheria ya watu wenye ulemavu namba 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 29 kinaeleza, umuhimu wa watu wenye ulemavu kufikia miundombinu pamoja na taarifa, mawasiliano na haki zote za kibinadamu. Tathmini ya Utekelezaji wa Se...

MARADI WA MALEZI,MAKUZI YA AWALI YA MTOTO ULIVOBADILISHA MITAZAMO KWA WAZAZI PEMBA

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA WAZAZI NA WALEZI kisiwani Pemba wamesema uwepo wa Mradi wa Malezi,Mkuzi na Maendeleo ya   awali ya mtoto umewasaidia, kwani wameelewa umuhumu wa kukaa karibu na watoto wao na kucheza nao. Walisema mradi umewazesha kujua   kipindi cha siku 1000 ndicho kipindi pekee mtoto anachohitaji uangalizi zaidi na kuwandaliwa kuwa mtoto bora wa baadae. Akizungumza katika kikao cha tathmini juu ya mradi huo mzazi Asha kutoka N’gambwa Chake, alisema baada ya kupata elimu ya malezi na makuzi ya awali ya mtoto amejenga ukaribu na watoto wake na wamekua na uthubutu wa kuiga baadhi ya mambo ambayo wanamuona akiyafanya. ‘’Kwa mfano wakati nikiwa jikoni nikipika nilikua mtoto namuweka mbali kwani nahisi ananikera, ila kwa sasa napika nae na nikimenya mbatata yeye anamenya vitunguu,’’alisema. Kwa upande wake mzazi Kassim Masoud Hamad kutoka Piki Wete alisema zamani ilikua watoto wake hawakua na ukaribu   nawala hawakisubutu kumueleza shida zao, bali ...

ADAIWA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA MIWILI

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA KIJANA SHAAME Ali Hamad anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka (38) mkaazi wa Mchangamdogo wilaya ya Wete Pemba, ashikiliwa na adaiwa za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka miwili na miezi mitatu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko nyumbani kwake, mama wa mtoto huyo alisema mtoto wake alifanyiwa tukio hilo la kinyama akiwa nyumbani kwa jirani yake ambae ni mtuhumiwa. Alisema, siku ya Ijumaa ya tarehe 26/06/2026 akiwa nyumbani kwake akifanya shughuli zake, mtoto wake alikuwa hajamuona muda mrefu, ndipo aliponza kumtafuta na kumuita kwa jina ingawa hakubahatika kumuona kwa wakati huo. ‘’Nilirudi nyumbani kuendelea kufua lakini nilifanya wasiwasi na nikaamua kwenda kumtafuta tena, ndipo nikamkuta amekaa nje ya mlango wa nyumba ya Shaame, akiwa na hali ya huzuni,’’ alisema. Alisema, alimwambia asimame ili waondoke lakini mtoto huyo hakuweza kusimama na akambeba na kwenda nyumbani kwao na kumueka huku yeye akiendelea na shughuli zake. Alisema, baada ya ...

WANDISHI WA HABARI IELIMISHENI JAMII MATUMIZI YA MITANDAO

Image
  NA FATMA HAMAD,PEMBA MTAALAMU WA Masuwala ya Mitandao ua Kijamii kisiwani Pemba Mustafa Mohd Abdul Rabi Moyo amewataka Wandishi wa Habari kuendelea kuielimisha jaamii  hususani  ya wanawake, kufuata  miko na maadili ya mitandao, ili kuepuka kufanyiwa udhalilishaji  mitandaoni. Mtaalamu huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Chakechake Pemba, alisema imeonekana jamii haina elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya mitandao, hivyo ipo haja wandishi wa habari kutoa elimu, ili kuepuka udhalilishaji huo. Alisema kutokana na kuzuka kwa wimbi la udhalilishaji katika mitandao ya kijamii kwa wanawake, ni budi jamii kuelimika na kufahamu madhara ya udhalilishaji mtandaoni. Alisema kwa sasa udhalilishaji ambao unatumika zaidi  katika mitandao ni wa mashambulizi ya matusi, na huu unakuja pale mwanamke anapotuma  picha za maungo yake  yakiwa utupu. ‘’Niwambie tu dada zangu, licha kua mnatangaza biashara zenu i...

JINSI MICHEWENI ILIVYOWAOKOA WATOTO DHIDI YA AJIRA ZA UTOTONI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Miaka iliyopita, katika baadhi ya vijiji vya Micheweni, ilikuwa kawaida, kumuona mtoto mwenye umri mdogo akiwa shambani, bandarini au sokoni badala ya kuwa darasani.   Wengine walikuwa wakibeba mizigo, kuvua samaki, kuuza bidhaa au kufanya kazi za nyumbani kwa muda mrefu, huku ndoto zao za elimu zikififia taratibu.   Ingawa kupitia ushirikiano kati ya serikali ya wilaya, kamati za skuli, walimu, wazazi, viongozi wa dini pamoja na mashirika ya kutetea haki za watoto, Micheweni inaanza kushuhudia mwanga mpya katika mapambano dhidi ya ajira za watoto. Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, anasema kwa miaka ya sasa Micheweni, inaanza kuandika historia mpya, tofauti na zamani ambapo watoto wengi walionekana mashambani na bandarini,   wengi wao wanaonekana wakiwa madarasani wakijenga ndoto zao.   Sheha wa Sizini Suleiman Shaame Hamad anasema mkakati umezaa matunda kwani   kuanzia mwaka 2023 hadi 2025   Shehia yake peke...