WANAWAKE WENYEULEMAVU WASHIKA MKIA KWENYE KAMATI ZA SHEHIA
NA FATMA HAMAD, PEMBA WATU WENYE ulemavu, wana haki ya kushirikishwa katika nyanja zote za kiuchumi, kama raia wote, bila ya kujali ulemavu wao, maana kinachoangaliwa sio ulemavu bali ni haki zao na uwezo wao . Na ndio maana, serikali, ikaweka muongozo maalumu, ili maendeleo ya nchi yasiwaache nyuma kwa kuimarisha muundo wa tasisi za watu wenye ulemavu. Tanzania imeridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD), wa mwaka 2006 unahimiza serikali, kuhakikisha ushiriki sawa wa watu wenye ulemavu katika siasa na maamuzi. Hata Katiba ya Zanzibar ya 1984, ambayo ndo sheria mama, kupitia kifungu chake cha 21(1) nacho kinatambua haki ya kila raia kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi bila ubaguzi. S...