JINSI MICHEWENI ILIVYOWAOKOA WATOTO DHIDI YA AJIRA ZA UTOTONI
NA FATMA HAMAD, PEMBA Miaka iliyopita, katika baadhi ya vijiji vya Micheweni, ilikuwa kawaida, kumuona mtoto mwenye umri mdogo akiwa shambani, bandarini au sokoni badala ya kuwa darasani. Wengine walikuwa wakibeba mizigo, kuvua samaki, kuuza bidhaa au kufanya kazi za nyumbani kwa muda mrefu, huku ndoto zao za elimu zikififia taratibu. Ingawa kupitia ushirikiano kati ya serikali ya wilaya, kamati za skuli, walimu, wazazi, viongozi wa dini pamoja na mashirika ya kutetea haki za watoto, Micheweni inaanza kushuhudia mwanga mpya katika mapambano dhidi ya ajira za watoto. Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, anasema kwa miaka ya sasa Micheweni, inaanza kuandika historia mpya, tofauti na zamani ambapo watoto wengi walionekana mashambani na bandarini, wengi wao wanaonekana wakiwa madarasani wakijenga ndoto zao. Sheha wa Sizini Suleiman Shaame Hamad anasema mkakati umezaa matunda kwani kuanzia mwaka 2023 hadi 2025 Shehia yake peke...