WANAWAKE WENYEULEMAVU WASHIKA MKIA KWENYE KAMATI ZA SHEHIA
NA FATMA HAMAD, PEMBA WATU WENYE ulemavu, wana haki ya kushirikishwa katika nyanja zote za kiuchumi, kama raia wote, bila ya kujali ulemavu wao, maana kinachoangaliwa sio ulemavu bali ni haki zao na uwezo wao. Na ndio maana, serikali, ikaweka muongozo maalumu, ili maendeleo ya nchi yasiwaache nyuma kwa kuimarisha muundo wa tasisi za watu wenye ulemavu. Tanzania imeridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD), wa mwaka 2006 unahimiza serikali, kuhakikisha ushiriki sawa wa watu wenye ulemavu katika siasa na maamuzi. Katiba ya Zanzibar ya 1984, Kifungu kidogo cha 3 kinaeleza kwamba, kila mzanzibari anayohaki ya kushika nafasi yoyote ya kazi na shughuli yoyote iliyoko chini ya mamlaka ya Zanzibar. Sheria ya watu wenye ulemavu namba 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 29 kinaeleza, umuhimu wa watu wenye ulemavu kufikia miundombinu pamoja na taarifa, mawasiliano na haki zote za kibinadamu. Tathmini ya Utekelezaji wa Se...