Posts

Mkurugenzi wa TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia

Image
  NA MWANDISHI WETU Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar. “Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio ng...

UNYANYAPAA ADUI ASIEONEKANA KWA WAGONJWA WA KIFUA KIKUU

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   NI kawaida ya binadamu walio wengi wanapoumwa hunasibisha maradhi yao na imani za kishirikina.   Na aina hii ya watu hawasikii, hawaoni wala hawashauriki kuhusu huduma za hospitali na hatimae kuangukia kwenye waganga wa kienyeji.   Ingawa baadhi yao huelekeza imani zao kwengine baada ya kuona huduma za hospitali hazikuzaa matunda huku wakiwa wanaripoti kila wanapopangiwa.   Ugonjwa wa kifua kikuu ni moja ya ugonjwa ambao watu wengi huelekeza imani zao kwengine kutokana na jinsi unavyokuja huku ukiwa dalili za mwanzo kutoonekana.   ‘’Kila siku unapoenda hospitali ukisema unaumwa na kifua unapewa dawa tu bila kupimwa, hivyo hali ikiendelea kudhoofu mtu anajiona kama tayari ana magonjwa mengine ya kishirikina,’’ alisema mwananchi Faida Hassan mkaazi wa Finya Wilaya ya Wete,  Anasema, wakati mwengine kutokufanyiwa vipimo ndipo kunakosababisha watu wengi kukimbilia kwa waganga wa kienyeji, jambo ambalo linaweza kuhatarish...

JAMII YAHIMIZWA KUITUNZA AMANI ILIYOPO NCHINI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA Viongozi wa kamati za  dini mbali mbali kisiwani Pemba (Pemba Interfaith Committee) wameipongeza jamii ya  wazanzibari kwa kuendelea kuishi kwa umoja na mshikamano, jambo lililoifanya Zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu na utulivu. Akitoa tamko la kamati hiyo katika kikao cha kufanya tathmini ya juhudi zilizofanywa na kamati hiyo za kushajihisha amani  kabla, wakati na baadhi ya uchaguzi mkuu uliofanyika Zanzibar mwenzi Oktaba mwaka huu, Mwenyekiti wa kamati ya dini mbali mbali kwa upande wa wanawake Amina Salim Ahmed  katika ukumbi wa mikutano wa Samail Gombani Pemba aliipongeza jamii ya kwa kuendelea kuishi kwa umoja na mshikamano jambo lililoifanya zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu. Alisema hali hiyo ilikuja kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na viongozi wa dini, Serikali, na wananchi katika kudumisha misingi ya maelewano ambayo imeijenga Zanzibar. Alieleza tamko hili ni mwendelezo wa wito wa kila mara unaosisitiza kwamba amani ...

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI

Image
                               NA FATMA HAMAD, PEMBA WANAWAKE wanne pekee wa shehia ya Mchanga mdogo ambao ni wanaufaika wa mfradi wa   Zanzibar Women Leadership in Adaptation (ZAN ADAPT) wako mbioni kuuwaga umaskini wa kipato. Matumaini yao, yanakuja kufuatia wote kwa pamoja kumiliki miti ya biashara na chakula 3,379 ambayo yanaweza kuwaingizia zaidi ya shilingi   Milioni Milioni 10.7.   Wanamiliki miembe 22 , wakiamini kama itaaza yote watajivunia wastani wa embe 1,1000 na pindi wakiyauza kwa bei ya juma ya shilingi 500, watajipatia jumla ya shilingi ya shilingi milioni 5,500,000.     Miti mingine wanayomiliki ni Miparachichi 9, ambapo kwa mujibu wa Mwanafunzi anaefanya Digrii ya kilimo   katika Chuo cha Kilimo na Technology cha Mwalimu Nyerere (MNUAT) kilichopo Musoma Tanzania bara   Makame Jafar Juma, anasema kila   mmoja, unauwezo wa kuzaa maparachic...

UISLAMU NA UMILIKI WA ARDHI KWA MWANAMKE

Image
  Je, ni vipi uislamu unampa nafasi mwanamke kumiliki ardhi? NA FATMA HAMAD, PEMBA Kwa muda mrefu, kumekuwepo na dhana potofu katika baadhi ya jamii, hususan Zanzibar, kwamba mwanamke hana haki ya kumiliki ardhi. Dhana hii imejikita zaidi katika mila na tamaduni kuliko katika misingi ya dini ya Kiislamu. Viongozi wa dini na wanaharakati wa haki za wanawake wamekuwa mstari wa mbele kupinga mtazamo huo, wakisisitiza kuwa Uislamu unamtambua mwanamke kama mmiliki halali wa mali, ikiwemo ardhi. Ingawa viongozi wa dini ya kiislamu wanapinga mtazamo huo, wanaeleza kuwa mwanamke ana haki ya kurithi, kununua, na kutumia mali au ardhi kwa ridhaa yake mwenyewe. Kiongozi wa dini ya kiislamu kutoka kijiji cha Wingwi Njuguni kisiwani Pemba Juma Othman Nahoda  anasema ‘’Urithi ni haki ya mwanamke, na si hisani’’ Anasema katika Suratul- Nisa, aya ya saba (7) ‘’wanaume wanafungu katika walichoachiwa na wazazi wao na wanawake pia wanafungu katika walichoachiwa, iwe kidogo au kikubwa, ni fungu l...