SERIKALI YAAHIDI KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI KWA MTOTO
NA FATMA HAMAD, PEMBA Naibu waziri wa wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Zawad Amour Nassor, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara hiyo imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto. Naibu waziri huyo ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afirika lililofanyika Viwanja vya kufurahishia watoto Tibirinzi Chkachake mkoa wa Kusini Pemba. Alisema Hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto katika ngazi zote, kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na lishe, kuhamasisha malezi chanya pamoja na kuendeleza ushiriki wa watoto katika masuala yanayowahusu. ‘’Maisha bila udhalilishaji yanamaanisha mtoto kulindwa dhidi ya ukatili wa kimwili, kihisia, kingono, kutelekezwa, unyanyasaji mtandaoni, ajira za watoto na mila au desturi zinazoweza kuathiri ustawi wake,’’alisema...