Posts

JINSI MICHEWENI ILIVYOWAOKOA WATOTO DHIDI YA AJIRA ZA UTOTONI

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA   Miaka iliyopita, katika baadhi ya vijiji vya Micheweni, ilikuwa kawaida, kumuona mtoto mwenye umri mdogo akiwa shambani, bandarini au sokoni badala ya kuwa darasani.   Wengine walikuwa wakibeba mizigo, kuvua samaki, kuuza bidhaa au kufanya kazi za nyumbani kwa muda mrefu, huku ndoto zao za elimu zikififia taratibu.   Ingawa kupitia ushirikiano kati ya serikali ya wilaya, kamati za skuli, walimu, wazazi, viongozi wa dini pamoja na mashirika ya kutetea haki za watoto, Micheweni inaanza kushuhudia mwanga mpya katika mapambano dhidi ya ajira za watoto. Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, anasema kwa miaka ya sasa Micheweni, inaanza kuandika historia mpya, tofauti na zamani ambapo watoto wengi walionekana mashambani na bandarini,   wengi wao wanaonekana wakiwa madarasani wakijenga ndoto zao.   Sheha wa Sizini Suleiman Shaame Hamad anasema mkakati umezaa matunda kwani   kuanzia mwaka 2023 hadi 2025   Shehia yake peke...

HOFU YA UDHALILISHAJI MTANDAONI INAVYOWANYAMAZISHA WANAWAKE

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA   Katika ulimwengu wa kidijitali, mitandao ya kijamii imekuwa sauti ya wengi, ni mahali ambapo watu hujadili siasa, biashara, elimu na masuala ya kijamii.   Ingawa kwa wanawake wengi, majukwaa haya yamekuwa pia uwanja wa matusi, vitisho na udhalilishaji unaowafanya waogope kujieleza hadharani. Mara nyingi mwanamke anapotoa maoni kuhusu suala la kijamii au kisiasa, hukumbana na mashambulizi yanayolenga jinsia yake badala ya hoja aliyoitoa. Matokeo yake, baadhi yao huamua kunyamaza, kufunga akaunti au kujiondoa kabisa kwenye mijadala ya umma.   Kwa sasa Tatizo hilo linaonekana kuwa changamoto kubwa ya haki za kidijitali na usawa wa kijinsia duniani.   Utafiti wa kimataifa uliofanywa na UNESCO kwa kushirikiana na International Center for Journalists (ICFJ) mwaka 2021, uliowahusisha wanawake wanahabari 901 kutoka nchi 125, ulibaini kuwa asilimia 73 walikuwa wamewahi kukumbana na vurugu au udhalilishaji mtandaoni kutokana na kazi zao.   Utafiti ...