UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI

 


                             NA FATMA HAMAD, PEMBA

WANAWAKE wanne pekee wa shehia ya Mchanga mdogo ambao ni wanaufaika wa mfradi wa  Zanzibar Women Leadership in Adaptation (ZAN ADAPT) wako mbioni kuuwaga umaskini wa kipato.

Matumaini yao, yanakuja kufuatia wote kwa pamoja kumiliki miti ya biashara na chakula 3,379 ambayo yanaweza kuwaingizia zaidi ya shilingi  Milioni  10.7.

 Wanamiliki miembe 22 , wakiamini kama itaaza yote watajivunia wastani wa embe 1,1000 na pindi wakiyauza kwa bei ya juma ya shilingi 500, watajipatia jumla ya shilingi ya shilingi milioni 5,500,000.   

Miti mingine wanayomiliki ni Miparachichi 9, ambapo kwa mujibu wa Mwanafunzi anaefanya Digrii ya kilimo  katika Chuo cha Kilimo na Technology cha Mwalimu Nyerere (MNUAT) kilichopo Musoma Tanzania bara  Makame Jafar Juma, anasema kila  mmoja, unauwezo wa kuzaa maparachichi kati ya 200 hadi 250, kutegemeana na mazingira.

Anafahamisha kuwa miche hiyo iko ya aina mbili ikiwa ni pamoja na ya muda mfupi na ya muda mrefu, ambapo hata uzaaji wake inategemeana na mazingira ya ardhi yenyewe na ushughulikiaji wenyewe.

Sasa wanawake hawa, wenyewe huwenda wakajipatia matunda hayo 2,250 ambapo kwa bei ya jumla ya sokoni ni shilingi 700, na kujipatia shilingi milioni 1.5

Fatma Hamad Bakar, alimueleza mwandishi wa makala hii, kuwa katika kilimo chao msitu, kwa sasa wanamiliki migomba 412, ya mkono mmoja.

Kumbe wanawake hawa kupitia mradi huu wa mabadiliko tabia nchi, wanategemea kujipatia wastani wa shilingi Milioni 3,296,000 ikiwa wataiuza ndizi moja kwa bei  ya jumla ya shilingi 8000.

Mwengine ni Zaitun Hassan Ali, anasema yeye peke yake anayo minanasi 497, anategemea kupata wastani wa shilingi Milioni 8.4 baada ya kuuza kila nanasi moja kwa shilingi  1700.

‘’Mimi peke yangu nategemea kujichukulia wastani wa shilling Milioni 8.4 kupitia kilimo cha minanasi, na tena kwa msimu mmoja tu,’’anasema.

Pia wamawake hao wanaeleza kwamba baada ya mafunzo ya kilimo msitu walioyapata kutoka Tamwa waliamua kupanda  Midalasini, ambapo wanayo 434, katika mashamba yao.

 ‘’Ndugu muandishi baada ya miaka mitatu Mchangamdogo kila kona utakayopita utasikia harufu ya Pilau, kwani midalasini yetu hiyi itakua imeshapea (imeshakomaa).

Wanasema kwa msimu wa kwanza wanamatumaini ya kuzitia mkononi wastani wa Shilingi Miliono 45,570,000, kupitia kilimo cha Midalasini ndani ya msimu mmoja tu.

LAKINI JEE  HOFU YAO WANAWAKE HAO NI IPI JUU YA SHUGHULI ZAO HIZO

Wakulima hao wanawake wanaeleza  kwamba wanahofu ya kuja kuzikosa pesa hizo katika misimu mwingine  kwani, wanahofu ya kupokonywa mashamba  ambayo wanafanyia shughuli  zao hizo za kilimo, kwa vile si za kwao bali ni za waume zao.

Fatma Hamad Bakar ni mmoja wa wanawake hao wakulima, anasema shamba analotumia kufanya shughuli hizo za kilimo msitu sio la kwake, bali ni  la  mama wa marehemu mume wake.

‘’Sina shamba langu mwenyewe, nalima kwenye shamba la mamayake marehemu mume wangu, mimi sijarisishwa ardhi katika familia yangu, kwani hakuna utaratibu wa kurithishana’’anasema.

Mwengine ni Zaitun Hassan Ali anasema  shughuli zake  za kilimo msitu anazifanya katika shamba la mume wake, yeye hana ardhi yake mwenyewe.

Anasema yeye, familiani kwao wanayomashamba, ingwa licha ya kua wazazi wao wameshaondoka lakini yanabakia katika mikono ya ndugu zao.

‘’Hata ukijaribu kudai utaambiwa wewe shamba la kazi gani wakati umeolewa mbali, sasa utalihudumia vipi,’’anaeleza.

Mwanamke mwengine ni Maryam Ali Juma (sio jina lake halisi) kutoka shehia jirani ya Mchangamdogo, anasema yeye alirithi shamba baada ya kufa wazazi wake, ingawa  kaka zake walishampokonya, wanalitumia wao.

‘’Baada ya kufariki wazazi wetu tulirithi, ingawa kakazangu wameshanipokonya, na sasa nalima kwenye shamba la mume wangu,’’anasema.

Asha Khamis  wa Mchangamdogo anasema yeye shamba analotumia kulima kilimo hicho ni la kwake mwenyewe.

Anasema aliamua kununua shamba lake mwenyewe ili afanye shughuli za kilimo ambazo zitaweza kumuingizia kipato, na hakuweza kutegemea shamba la ukoo.

Anasema  hakutaka kuja kusumbuana na familia yake kwa suala urithi, bali alidunduliza pesa zake hadi akafanikiwa kununua shamba lake mwenyewe.

 ‘’Nilianza kudunduliza pesa katika biashara zangu za  kachori, mandazi na malai, hadi nikatimiza nikanunua, na sasa nalima  shambani kwangu mwenyewe,’’anasema.

Hamad Haji Suleiman ni mume kati ya miongoni mwa mama hao anasema amamua kutoa shamba lake kumpa mke wake afanyeshughuli hizo za kilimo, kwa vile hana shamba lake mwenyewe kwani nyumbani kwao hajapewa, na wala hana uwezo wa kununua shamba.

''Kwa vile shughuli hizo anazozifanya mkewangu za kilimo msitu ni jambo muhimu katika maisha yetu nimeamua kumpa shmba langu mimi mwenyewe ambalo nimelipata katika familia yangu kumpa alime tupate mazao ya chakula, pesa na huku tukinga na athari za mabadiliko ya tabianchi,''anasema.

Anasema ni kweli wengi wa wakulima hao hawanamashamba yao wenyewe, kwani hawana uwezo wa kununua, na familia nyingi wanapofariki wazazi wao wanaona mwanamke kurithi ardhi sio jambo la muhimu kwake, wanahisi hawawezi kulihudumia ahata akipewa, kwa vile wao ni watu wa kuolewa na kuhamia sehemu nyengine.

JAMII

Maimuna Ali Khamis (sio jina lake halisi) mwananchi kutoka Micheweni anasema familia nyingi zinapofariki wazazi wao hawana utaratibu wa kurithi kama kuna mali zilizoachwa zaidi hwanufaisha wanaumetu, hali inayowafanya wanawake kuhangaika kwa kukosa rasilimali shamba za kuzalisha  mazao na kujipatia kipato.

Omar Khamis  Kombo (sio jina halisi) kutoka Maziwangombe micheweni anasema sababu kubwa inayopelekea wanamke siku zote kukosa ardhi zao wenyewe ni  kutokuonekana, kama hawana haki ya kurithi na kumiliki.

WANAHARAKATI

 Sada Juma Segeja mtetezi wa masuala ya wanawake kutoka Jumuia ya Uhifadhi wa misitu Pemba CFP, anasema moja ya changamoto inayowakabili  katika mradi wao wa uhifadhi mazingira ni baadhi ya wanawake kukosa  Ardhi zao wenyewe.

‘’Hofu yetu ni pale ambapo mwanamke ataachika, jee zile nguvu zake ashazozipoteza kwa kupanda Misitu itakuaje, wakati shamba ni la mume walieachana.

Anasema  kwa sasa wamekua wakiwapatia elimu ya ujasiriamali wafanye biashara wapate pesa wanunue mashamba yao wenyewe, pamoja na kupata hatimiliki kwa  walio na shamba zao wenyewe.

                                                                                                                                                                                                    

                                                                                                                                 
Mkuu wa kitengo cha  mawasiliano kutoka Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar, Sofia Ngalapi anasema wamekua wakitoa elimu mara kwa mara kwa jamii, ili ifahamu umuhimu wa mirathi, na kuona mwanamke ana uwezo wa kumiliki mali za marehemu wazazi wake ikiwemo ya ardhi.

MWANASHERIA

Naibu Mrajisi kutoka Kamisheni ya ardhi Pemba Asha  Suleiman Said anasema kwa mujibu wa Sheria ya ardhi namba 12 ya mwaka 1992 inaeleza kuwa ardhi ya Zanzibar ni mali ya umma, hivyo kila mwananchi anahaki ya kutumia ardhi.

Anasema katika Kifungu cha saba cha Sheria hiyo  kinaeleza kwamba  haki ya kutumia ardhi ya Zanziba ni kwa wazanzibari tu.

Akitaja moja ya njia ambayo mtu anaweza kupata ardhi na kutumia ni kurithi baada ya kufariki kwa wazazi wake.

‘’Sheria ya ardhi inalitambua suala la mirathi, hivyo  anapofariki mtu wale warathi wafike Kamisheni ya Wakfu na maliamana,kupata taratibu za mirathi na kupa hatimiliki,’’anaeleza.  

VIONGOZI WA DINI

Asya Amour Abrahman  Amirati kutoka Jumuiya ya wanawake wa kiislamu Pemba (JUMA WA KIPE) anasema  kwa mujibu wa Sheria ya Dini ya Uislamu  mwanamke  anahaki ya kumiliki Ardhi.

‘’Mwanamke  anahaki ya kumiliki ardhi  na akaweza kuitumia kwa shughuli za kilimo, na akajipatia kipato kutokana na Shamba lake, isipokua kuna mipaka yake katika suala la mirathi tu,’’anafafanua. 

Anasema mwanamke anahaki ya kufanya shughuli zozote za kimaendeleo na kujipatia kipato ambacho kinakubalika katika  uislamu. 

Kiongozi wa Kanisa Katoliki lililopo Mkungu Malofa Chake chake  mkoa wa Kusini Pemba Robert Miguwa Ndalami, anasema  mwanamke anahaki ya kumiliki ardhi kama mwanamme, kwani hata dini yao haijamkataza asimiliki ardhi.

MIKATABA

Mkataba wa Umoja wa Mataifa CEDAW wa mwaka 1986, unapiga marufuku ubaguzi wa kijinsia katika umiliki wa mali.

Itifaki ya Maputo (kifungu cha 21) inahakikisha wanawake wanapata urithi bila kubaguliwa na tamaduni.

Mkurugenzi wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Mzuri Issa Ali anasema ijapokua Sheria zinasema kila mwanamke anahaki ya kumiliki ardhi, ingawa bado kunaurasimu mkubwa juu ya jambo hilo

Kwa mujibu wa Utafiti alioufanya Mkurugenzi  huyo,  wa mwaka 2025, ulionesha kuwa mitazamo ya jamii na vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kuendeleza au kupunguza mitazamo hiyo potofu.

Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakwimu mku wa Serikali za mwaka 2014,/15, na 2019/20 zinaonesha kuwa ni asilimia 5.5 ya wanawake waliokua wanamiliki ardhi ikilinganishwa na wanaume ambao ni asilimia 12,  hivyo inaonekana kuna pengo kubwa la kijinsia kumiliki rasilimali muhimu.

 Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 12 (a) kinaeleza kuwa watu wote ni sawa mbele ya Sheria, na wanayohaki, bila ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya Sheria.

Makadirio  ya  Bajeti  kwa  mwaka wa  Fedha  2023/2024   ya Wizara  ya  Ardhi  na  Maendeleo  ya  Makaazi,  Kuendelea  kutoa  elimu  kwa  jamii  kuepuka  kujiingiza  kwenye  migogoro  ya  ardhi  kwa kufuata  Sheria  za  ardhi.

Ripoti ya Banki ya Dunia inaeleza kushindwa kuchukuliwa hatua za mabadiliko ya tabianchi,  kunaweza kupunguza ukuaji wa uchumi Tanzania kwa asilimia nne ifikapo mwaka 2050.

ATHARI YAKE

Endapo wanawake watakosa Ardhi na kufanyashughuli za kuzalisha, daima wataishi katika hali ya unyonge na pia zikitokezea athari za mabadiliko tabianchi zitawakumba kwa haraka,’’wakulima wenyewe wanaeleza.

NINI KIFANYIKE

Afisa mawasiliano kutoka TAMWA Zanzibar Sophia Ngalapi anasema ipohaja kwa wanawake kuamka na kuhakikisha wanafanya biashara japo ndogondogo, ili wanunue mashamba yao wenyewe, na sio kutegemea za mirathi tu.




 

 


Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’