‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’

 


NA FATMA HAMAD, PEMBA

Katibu mkuu wizara ya  Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdala Said amewataka wandishi wa habari kuielimisha jamii kufahamu umuhimu wa malezi na makuzi ya awali ya mtoto, ili kufahamu utaratibu wa kuwalea katika kipindi hicho,  na kupatikana kizazi chenye afya njema.

Alisema katika visiwa vya Zanzibar bado kuna tatizo la udumavu kwa watoto  kutokana na kukosa huduma muhimu kama vile Afya, Chakula bora, ulinzi pamoja na ushirikishwaji, hasa  katika kipindi cha awali  cha  malezi,  makuzi na maendeleo ya mtoto.

Katibu Mkuu huyo aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku nne Waandishi Vinara wa ECD Zanzibar, yaliofanyika Mjini Dar esalam.

Alisema wandishi wa habari wanajukumu kubwa katika jamii, hivyo ipo haja kuwaelimisha kufahamu umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto, ili kupata kizazi chenye madili na afya bora.

‘’Ndugu zangu wandishi wa habari nyinyi  mnadhima kubwa katika jamii, hivyo ni wakati kuifahamisha ielewe dhana nzima ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto,’’ alisema.

 Alisema kwa mujibu wa sayansi ya ECD katika kipindi cha awali cha siku 2000 ndicho kipindi pekee  ambacho mtoto anahitajika kupata huduma hizo, kwani ndipo akili ya mtoto  inatengenezwa, na anakua na uwezo wa kuchukua kwa haraka chochote  atakachokisikia.

Alisema serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya amali, Wizara ya Afya na Wizara ya Maendeleo ya Jamii inaendelea kutoa kipaombele katika uwekezaji wa awali kwa mtoto, ili kutambua misingi bora ya malezi, makuzi, na maendeleo ya awali ya mtoto.


Mapema Meneja Huduma za Jamii (ZPDB)  Dk Ibrahim Byatike Kabole alisema endapo wandishi wa habari waitumia vyema taaluma walioipata kuwaelimisha Jamii juu ya umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto, tatizo la udumavu kwa watoto litaondoka Zanzibar.

‘’Zanzibar kuwa na watoto wenye afya bora inawezekana, endapo wandishi wa habari  kama mtaitumia vizuri taaluma mliyoipata,kuwaelimisha wazazi juu ya umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo  ya awali ya mtomto,’’alisema.

Kwa upande  wake  Mtaalamu wa Programu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto  kutoka  UNSEF Alinune  Nsemwa, alisema kwa mujibu wa tafiti, katika visiwa vya  Zanzibar kuna  asilimia 47 tu ya watoto kuanzia miaka miwili hadi chini ya miaka mitano, ndio waliofikia ukamilifu wa ukuaji wao.

Alisema kutokana na takwimu hiyo ipo haja kwa wandishi wa habari kuhakikisha wanaielimisha jamii, kufahamu umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto, ili kupata kizazi chenye afya bora.

‘’Wandishi wa habari tuwafahamisheni wazazi, jinsi ya kulea watoto wao katika hatua za awali za makuzi na malezi bora,’’alisema.

Alisema wataendelea kushirikiana na  serikali ya Tanzania, ili kuona watoto wote wanaozaliwa ndani ya Nchi hii wanakua salama.


Nao wandishi walioshiriki mafunzo hayo walisema mafunzo yamewasaidia vyema, huku wakiahidi kuyafanyia kazi.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO