Posts

Showing posts from October, 2024

Gharama za Uchaguzi zinavyokatisha ndoto za wanawake wanaogombea.

Image
  Wasema hali isiporekebishwa majimbo yataendelea kuwa magumu kwao                              Na Fatma Hama, Pemba ‘’NATAMANI kugombea tena uongozi katika uchaguzi ujao wa mwaka 2025, lakini kila nikifikiria gharama…nakata tamaa,’’ Hayo si maneno ya mtu mwengine bali ni ya mwanamama Tumu Mwalim Massoud mwenye miaka 40 mkaazi wa Wingwi Limani wilaya ya Micheweni Pemba, ambae aligombea uwakilishi Jimbo la Wingwi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Mwanamama huyo kiu yake ni kuwa mwakilishi ili aweze kutetea haki za wananchi, ingawa anakumbuka gharama zilizomtoka katika uchaguzi wa mwaka 2020 na hatimae kushindwa katika kura. Anasema, kwa hali hiyo ndoto nyingi za wanawake wenye nia ya kugombea zitakatika na majimbo yataendelea kuongozwa na wanaume watupu, ambao kuna baadhi ya mambo yanaowahusu hawawezi kuyatetea. Ni mwaka wa 23 tangu Tumu aingie kwenye harakati za kisiasa, l...

Vijana Pemba waliojiajiri ufugaji Kaa wasahau ajira ya Serikali

Image
    NA FATMA HAMAD PEMBA, Vijana wameonywa  kuepuka kukaa katika vigenge viovu ,na badala yake wajiunge  na vikundi  vya ushirika,  ili waweze kujipatia kipato cha halali. Ushauri huo umetolewa na katibu wa kikundi cha ushirika  mapambano coperetive kinacho jishuhulisha na ufugaji wa Samaki, kaa, kamba  na mboga mboga  Bishara Muhammed Musa mbele ya  wanakikundi hao,  mara baada ya kuzungumza na mwandishi wa habari huko kikunduni kwao Sizini wilaya ya Micheweni Pemba. Alisema wakati umefika  kwa vijana  kuwamka na kujiajiri wenyewe, na sio kukaa tu vigengeni na kusubiri ajira Serikalini. ‘’Vijana  mtakapo jiajiri mtaepukana na  vitendo vya wizi, ubakaji na ujambazi,’’ alishauri katibu. Aidha  alieleza kuwa  sera ya Serikali  ya mapinduzi ya Zanzibar ya uchumi wa buluu  unaelekeza zaidi kwenye ba...

WAJAWAZITO WANAOKWENDA KUJIFUNGUA KITUO CHA AFYA WESHA WALAZIKA KWENDA NA NDOO KICHWANI

Image
                                                                                     NA FATMA HAMAD, PEMBA Septemba 21 mwaka huu Blog ya Pemba ya leo iliibua changamoto ya kukosekana kwa huduma ya Maji safi na salama katika kituo cha Afya cha Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, ambapo kilio hicho kimepatiwa ufumbuzi kwa sasa. Wakizungumza na mwandishi wa habari huko kituo cha afya wesha Safinia Said na Rukia Khamis ambao ni wajawazito waliokwenda kupata huduma kituoni hapo walisema zaid ya miezi 3 kulikuwa hakuna maji kituoni hapo.   Walisema kwa sasa shida ya Maji imepungua kwani Maji yanapatikana ijapokuwa hayatoki siku zote ni kwa mgao. ''kwa sasa hatuendi na madumu ya Maji tunapokwenda kujifungua kwani Maji ya zawa ikifika zamu ya kutoka huwa yanapatikana hapa kituoni...

Wananchi nendeni mkaripoti kero zenu

Image
                                 NA FATMA HAMAD PEMBA. Mkuu wa wilaya ya   Wete Hamad Omar Hamad amewataka wananchi wa mkoa wa Kaskazini Pemba kujitokeza kwa wingi katika kambi ya utoaji wa huduma ya Msaada wa kisheria ili waweze kupeleka matatizo yao na kupatiwa ufumbuzi. Mkuu huyo ameyasema hayo huko Micheweni wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya   Msaada wa kisheria ya Mama Samia kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud amesema Kambi hiyo ya siku tatu itawasaidia Wananchi kupata huduma na pia kujua wapi waripoti malalamiko yao. Amesema Jamii imekua ikikabiliwa na matatizo mbali mbali ikiwemo ya Ndoa, Ardhi,Mirathi, na Udhalilishaji hivyo ni wakati wananchi kuitumia fursa hiyo ili kuweza kupatiwa msada wa kisheria. ‘’Kambi hiyo itajumuisha Wanasheria, watoa huduma ya msaada wa kisheria hivyo tuwatumieni   kwani ni bure hakuna malipo yoyote,’’alisema. Kwa upand...

Wajumbe wanawake kamati za shehia waleta mabadiliko

Image
Shehia za Micheweni sera usawa ya kijinsia bado kitendawili NA FATMA HAMAD, PEMBA  SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua umuhimu wa kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.  Uwepo wa sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia ya mwaka 2000 na Mkakati wa Utekelezaji wake ya mwaka 2005, unathibitisha dhamira ya wazi ya Serikali ya kukuza usawa wa kijinsia. Lakini bado Sera hiyo haijatekelezwa ipasavyo, hili limeonekana katika wilaya ya Micheweni, ambayo ina masheha 25, wakiwa wanaume 17 na wanawake wanane (8) pekee.  Hata kwa upande wa wajumbe wa kamati za masheha utafiti umebaini kuwa, wapo 274, ingawa wanaume ni 169 na wanawake ni 105 tu. MASHEHA WENYEWE WANASEMAJE Sheha wa Shumbavyamboni Time Omar Said anasema Sera anaifahamu vizuri ndomana baada ya kupata uongozi akaweka wajumbe wanawake Anasema kamati yake inawajumbe 10 watano wanawake na wanaume watano. Anasema anampango wa kuongeza idadi ya wajumbe wanawake kwani wanaume ni wavivu kwenye kazi....

Wanawake watakiwa kugombea nafasi za uongozi

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA WANAJAMII Wilaya ya Micheweni kisiwani Pemba wamesema, kutokugombea nafasi za uongozi kwa wanawake, ni jambo moja linalorejesha nyuma maendeleo yao. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti walisema, ili kuondokana na  changamoto mbali mbali zinazowakabili ndani ya jamii zao, ni kuhakikisha wanawake wanagombea nafasi za uongozi. Mwananchi Biache Othman Ramadhan mkaazi wa Sizini alisema, iwapo akina mama  wataweza kujitoa wenyewe katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi, mambo yanayowakwaza yatatatuka kwa urahisi, kwani wataweza kuyasemea wenyewe kwenye vyombo vya kutoa maamuzi badala ya kusubiri wanaume kuwasemea. "Katika kugombea nafasi za uongozi kwa wanawake hakuna kizuwizi, isipokua sisi wenyewe tuwe tayari ili kuibua changamoto zinazosababisha tusiweze kugombea na kuhakikisha zinatatuliwa" alisema. Nae Salma khamis Tumu mkaazi wa Tumbe  alisema, imezoeleka siku zote mwanamke kuwekwa katika kundi la mwisho na kusab...

Wanaume msizitelekeze familia zenu

  NA FATMA HAMAD, PEMBA, Afisa mdhamini Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Hafidh Ali Mohamed amewahimiza wazazi hussusan wa kiume kusimamia majukumu yao ya kutunza na kulea familia zao ili kuwalinda watoto na vitendo viovu ikiwemo udhalilishaji na ujambazi. Afisa huyo ametoa wito huo wakati akifungua mafunzo ya siku moja yanayohusu kuwashirikisha wanaume katika malezi kwa Wasaidizi wa Sheria huko Makonyo Chake chake Pemba. Alisema wanaume ndio wenye jukumu   kubwa   la kuhudumia familia zao, hivyo endapo hawatofuata vyema   wajibu wao huo kutapelekea kupatikana kwa watoto wa mtaani pamoja na udhalilishaji kwa watoto. ‘’Niwasihi wazazi wenzangu wa kiume sisi ndio wenye dhamana za kutoa matunzo, hivyo tusizitelekeze familia zetu tutasababisha matatizo,’’alisema mdhamin. Aidha aliendelea kuwasihi wazazi kuwa na subra katika ndoa zao ili kuepusha talaka, kwani hilo ni moja ya sababu inayochangia watoto kudhalilishwa. ‘’Watoto wengi wanaokosa malezi ...