Posts

Showing posts from December, 2023

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Image
                                                     NA FATMA HAMAD PEMBA. Wazazi na walezi wenye watoto   wenye ulemavu wamekumbushwa   kuacha tabia ya   kuwanyanyapaa na kuwafungia ndani   watoto hao, kwani kufanya hivyo ni udhalilishaji kwao. Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Tumbe Mashariki katika mkutano maalumu Mkuu wa Polisi Jamii mkoa wa Kaskazini Abdala Majid Haji amesema wapo baadhi ya watu wamekuwa na itikadi potofu ya kuwachukulia watoto wenye ulemavu kama ni watu wasio na faida na badalayake huishia kuwafungia majumbani. ‘’Baadhi yetu hapa tunao watoto wetu wenye ulemavu tumewafungia tu ndani, hawatoki njee eti tunahofia jamii itatucheka,alisema. Alisema Watoto wenye ulemavu nawao ni binadamu kama wengine wanastahiki kupata haki na fursa mbali mbali kama vile Elimu, Afya,Ajira.   Alieleza kuwa ni wakati kwa wazazi wanaoishi na watoto wenye ulemavu   kubadilika na kuhakikisha wanatoa matunzo   sawa na wenzao   wengine wasio na ulemavu. Alifahamisha   udhalilis

UGUMU WA MALEZI KWA WANAFUNZI WALIOJIFUNGUA KUNAVYODIDIMIZA HAKI YAO YA KUPATA ELIMU.

Image
                          NA FATMA HAMAD, PEMBA  KUKOSEA NJIA SIO KUPOTEA NJIA. Binaadamu akipanga lake na Mungu hupanga lake. Ni usemi maarufu iliozoeleka miongoni mwa jamii ya Watanzania. Usemi huu unatumika kuonesha kwamba kwa kawaida binaadamu huishi kwa kujipangia mambo ya muda mfupi na mrefu, lakini inapokuja utekelezaji huwa ni majaaliwa. Hata hivyo msisitizo ni kwamba ili tufanikisho mambo yetu tunapaswa kujipangia kwa sababu wataalamu wanasema ukishindwa kupanga basi ujue unapanga kufeli. Ukweli wa maneno ya hapo juu haushii kwa wakubwa pekee bali Hata watoto nao huwa na mipango yao au labda tuite ndoto zao na hii pia huwa na nguvu Zaidi   kwa wanafunzi.   Huyu analenga kusoma na hatimaye awe mwalimu,   yule anata kuwa daktari, mwengine anapenda kuwa mkulima wa kileo, asakri polisi, mhasibu na kadhalika alimradi ndoto zao zinakuwa hazina mwisho Lakini kama zinavyoitwa hizo ni ndoto na ndoto zinakuwa na mambo mawili ama kutimia zikawa kweli ama kupotea njia.   Mtu a

WANDISHI WA HABARI WANAWAKE WAPEWA MBINU

Image
                                  NA FATMA HAMAD,PEMBA Wandishi wa habari   wametakiwa kuitumia    mitandao ya kijamii   kwa kufuata sheria za mtandaoni wakati wanaporusha habari zao ili kuepuka changamoto mbali mbali zinazojitokeza ikiwemo   unyayasaji. Hayo yamesemwa na Mtalamu wa mambo ya kidijitali kutoka shirika la Pen Amercan Cecilia Maundu wakati akizungumza na wandishi wa habari wanawake kutoka vyombo mbali mbali Zanzibar katika mafunzo yaliofanyika kwa njia ya mtandao [ZOOM]   juu ya kujilinda dhidi ya Unyanyasaji mtandaoni. Amesema suala la unyanyasaji katika mitandao limeongezeka,   hivyo ni wakati sasa wandishi wa habari wanawake kuhakikisha wanafuata Sheria na masharti   ipasavyo wakati wanapotuma kazi zao katika mitandao ya kijamii. ‘’Tumeona kwamba Wanawake ndio wathirika wakubwa   wa udhalilishaji   katika mitandao, hivyo tuweni makini jamani katika kutumia kwetu mitandao hiyo, alisema. Aidha Alifahamisha kuwa sio busara kutumiana picha za uchi   kwani ni njia

WADAU WA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI WAPEWA NENO

Image
                                                             NA FATMA HAMAD,PEMBA Wanaharakati pamoja na wadau mbali mbali wa kupambana na masuala   ya Udhalilishaji   wametakiwa kuendeleza mapambano dhidi ya vitendo hivyo ili kuhakikisha wanaondosha tatizo hilo ambalo limekua likiiathiri Jamii siku hadi siku. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Chama cha Wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar [TAMWA] Mzuri Issa Ali wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa kuwasilisha ripoti ya utekelezaji wa majukumu yao kwa mwaka 2023 huko Ofisi za [TAMWA] Tunguu kisiwani Unguja. Amesema vitendo vya udhalilishaji bado ni donda ndugu ambalo linaendelea kuiathiri Jamii, hivyo ni budi wanaharakati kujitoa kihali na mali kuifahamisha jamii kufahamu madhara ya udhalilishaji ili na wao waweze kuchukua hatua jambo ambalo litasaidia Watoto pamoja na wanawake kuishi kwa amani na matumaini. ‘’Niwambie wanaharakati wenzangu bado Jamii yetu inathirika na vitendo vya udhalilishaji, hivyo basi tu