WANDISHI WA HABARI WANAWAKE WAPEWA MBINU
NA FATMA HAMAD,PEMBA
Wandishi wa habari wametakiwa kuitumia mitandao ya kijamii kwa kufuata sheria za mtandaoni wakati
wanaporusha habari zao ili kuepuka changamoto mbali mbali zinazojitokeza
ikiwemo unyayasaji.
Hayo
yamesemwa na Mtalamu wa mambo ya kidijitali kutoka shirika la Pen Amercan
Cecilia Maundu wakati akizungumza na wandishi wa habari wanawake kutoka vyombo
mbali mbali Zanzibar katika mafunzo yaliofanyika kwa njia ya mtandao
[ZOOM] juu ya kujilinda dhidi ya
Unyanyasaji mtandaoni.
Amesema suala
la unyanyasaji katika mitandao limeongezeka,
hivyo ni wakati sasa wandishi wa habari wanawake kuhakikisha wanafuata
Sheria na masharti ipasavyo wakati
wanapotuma kazi zao katika mitandao ya kijamii.
‘’Tumeona
kwamba Wanawake ndio wathirika wakubwa
wa udhalilishaji katika mitandao,
hivyo tuweni makini jamani katika kutumia kwetu mitandao hiyo, alisema.
Aidha Alifahamisha
kuwa sio busara kutumiana picha za uchi kwani ni njia moja ya kuwarahisishia watu
kukufanyia unyanyasaji.
‘’Jamani
tujiepusheni kutumiana picha zetu tukiwa utupu hatakama ni mume wako,mke wako,
mpenizi wako,alifahamisha.
Alisema
lengo la mafunzo hayo kwa wandishi wa habari wanawake ni kuwapa taluma waweze kuitumia mitandao ya kijamii ipasavyo
ili waepukane na unyasasaji.
Akichangia katika mkutano huo mwandishi wa habari kutoka
Chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanzibar [TAMWA] Khairat Haji aliwataka wandishi wa habari wenzake kuepuka
kuweka vitu vyao binafsi [vya siri] ambavyo vinahusu familia zao, ili kuepuka
kudukuliwa tarifa zako.
Nao badhi ya
washiriki wengine walilipongeza Shirika la Pen Amerca kwa kuwapatia mafunzo
hayo ambayo yatakuwa ni chachu ya kuleta mabadiliko katika utumiaji wao wa
mitandao ya kijamii.
Hivyo
wameliomba shirika hilo kuendelea kuwapa taluma hiyo jambo ambalo litawasaidia kuwa
na uwangalifu wa hali ya juu wakati wanapotumia mitandao ya kijamii katika
utekelezaji wa majukumu yao ili waweze kuepukana na Unyanyasaji.
Comments
Post a Comment