RUSHWA MUHALI BADO NI GUMZO KWA KESI ZA UDHALILISHAJI
NA FATMA HAMAD PEMBA. Kuepo kwa rushwa muhali katika jamii bado ni changamoto kubwa inayopelekea kukwamisha kwa kesi za udhalilishaji zisipate hatia. Akitoa ripoti juu ya kesi za udhalilishaji mwendesha mashtaka wa serikali kutoka oisi ya mkurugenzi wa mashtaka Chake chake Mussa Khamis katika kikao cha kamati ya kupinga udhalilishaji kilichofanyika ofisi za Tamwa Kisiwani Pemba. Amesema licha ya elimu inayotolewa kwa jamii ili kuacha muhali lakini bado hawaja kuwa tayari juu ya mapambano dhidi ya udhalilishaji. ‘’Bila ya mashirikiano ya pamoja hatuwezi tukafika pahala jamani tutabakia tunaimba tu kila siku alisema PP Mussa. Aidha kwa upande mwengine alifahamisha kuwa kesi zinazowapa changamoto katika uwendeshaji wake ni za watoto wa miaka 15, 16 na 17 hawataki kutoa ushirikiano mahakamani. Baadhi ya wanakamati hiyo kutoka wilaya ya Mkoani wamekua wakivilalamikia vituo vya Polisi Mtambile na kengeja kuwa bado havijakuwa maki