Posts

Showing posts from July, 2021

WANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUANDIKA HABARI ZA VIJIJINI.

Image
  Afisa mdhamini wizara ya habri Vijana na Michezo Salum Ubwa amewataka wandishi wa habari kujikita zaid   Vijijini katika kuandika habari zao ili kuibua matatizo yanayo wakabili wananchi wa maeneo hayo. Hayo ameyasema katika Kongamano la uhuru wa kujieleza upatikanaji wa habari, mitandao ya kijamii na uandaaji wa maudhui kwa vijana na majukwaa ya maendeleo kwa vijana huko   Camail   Chake chake Pemba. Amesema vyombo vya habari ndio msemaji wa wasio na sauti, hivyo ni budi kwa wandishi wa habari kujitoa na kujituma ili kuona wananchi wa vijijini nawao wanapata fursa   ya kuzungumza na   vyombo vya habari   kutoa   kero zao na mamlaka husika na kuona   wana zitekeleza. ‘’Wandishi msiishie tu mjini nendeni vijijini kuna kero nyingi zinawakumba wananchi’’ Alisema afisa mdhamini. Amesema   wananchi   wengi wa vijijini wanaendelea kuishi katika   matatizo kutokana na kukosa taluma na taratibu za ufuatiliaji   wa shida zao kwa vyombo husika jambo ambalo linapelekea kukosa haki zao.

WANDISHI WAONYWA KUEPUKA KUANDIKA HABARI ZA UCHOCHEZI

Image
  Wandishi wa habari wametakiwa kuepuka kuandika habari zisizo na mizania na zenye viashiria vya uchochezi ili kusaidia kuepusha   kutokea   kwa   migogoro isiyo ya lazima katika jamii. Wito huo ulitolewa wakati wa mafunzo ya kujenga amani na utatuzi wa migogo kwa waandishi wa habari kisiwani Pemba yalioendeshwa na shirika la kimataifa la utatuzi wa migogor la SEARCH FOR COMAN GROUND kupitia mradi wa Dumisha amani Zanzibar. Akizungumza na wandishi wa habari katika mafunzo   ya kutatua migogoro kwa njia shirikishi yenye lengo la kudumisha amani Husein Faraji Sengu amesema lengo la mradi ni kusadia kutatua migogoro ya kisiasa hususani mara baada ya kumalizika uchaguzi Zanzibar. Amesema uzoefu unaonyesha kua Zanzibar mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi kumekua kukitokea athari nyingi za kisisiasa ambazo zinatokana na uchaguzi ikiwemo migogoro kwa matabaka tofauti ambayo ikiachiwa iendelee inaweza kuondosha amani ya zanziba iliopo. Amesema wakati mwengine vyombo vya habari vimeku

JESHI LA POLISI LA DAIWA KUFANYA SULUHU KESI ZA UDHALILISHAJI

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wadau wa kupinga ukatili na   udhalilishaji wa kijinsia kisiwani Pemba wamelalamikia juu ya uwepo   wa baadhi ya Askari wanaozifanyia suluhu kesi za udhalilishaji. Akizungumza katika mkutano wa uwasilishaji wa ripoti   ya utekelezaji wa mradi   wa kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia   msaidizi wa sheria kutoa mkanyageni mkoani pemba Shaban Juma Kassim huko ofisi za chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania [TAMWA]   Chake chake   amesema kazi ya askari ni kufanya upelelezi tu na sio kutoa suluhu. Amesema wapo baadhi ya askari huwataka wazazi wanaokwenda   kuripoti kesi za udhalilishaji kuzimalizia vituoni tu na wasiende mahakamani. ‘’Bado wenzetu wa Jeshi la polisi wanaturejesha nyuma hawajakuwa tayari kukomesha udhalilishaji,’’Alisema msaidizi wa sheria. Hivyo amewataka wazazi wa wathirika wa matukio hayo wasikubali suluhu bali wasimame kidete kutoa ushahidi ili kuona kesi zao zimepatiwa hatiani. Kwa upande wake Haji Sho

ZAEKA YATAKIWAN KUHAMIA KATIKA OFISI ZA VYAMA VYA SIASA WAKATI UNAPOFIKIA KIPINDI CHA CHAGUZI

Image
                        NA FATMA HAMAD FAKI MPEMBA. Mamlaka ya kuzuia Rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar [ZAEKA] imetakiwa kuelekeza nguvu zao za uchunguzi   katika vyama vya siasa wakati unapofikia uchaguzi mkuu wa Zanzibar ili kuwakamata na kuwachukulia hatua wale ambao watabainika kutoa rushwa kwa ajili ya kupata nafasi za uongozi Majimboni. Wito huo umetolewa na baadhi ya Wanawake waliogombea nafasi mbali mbali za uongozi katika uchaguzi mkuu uliopita   2020 wamesema wakati unapofika kipindi cha uchaguzi rushwa imekua ikitawala kwa kiasi kikubwa katika vyama siasa nchini. Wamefahamisha kuwa nafasi za uongozi majimboni asilimia kubwa huchukuliwa na wale wenye pesa tu, jambo ambalo linawakatisha tama wanawake masikini wenye nia ya kugombea kushindwa kuwania   nafasi hizo. ‘’Tuna iomba   zaeka   itende haki, katika kazi yao ya kupambana   na rushwa na uhujumu uchumi kuwachukulia hatua wale wote ambao wanatumia nguvu ya fedha kama njia ya kupata madaraka,’’ Walisema wanawake wagom

SHAHIDI APELEKEA KESI KUGHAIRISHWA.

Image
  Kutokuwepo kwa shahidi   kumesababisha hakimu wa Mahakama ya Mkoa B   iliopo Chake chake kughairisha kesi ya kuingilia kinyume na maumbile inayomkabili kijana Ayoub Mohd Hamad mwenye umri wa 18 mkaazi wa Likoni kengeja  Wilaya ya Mkoani Pemba.   Baada ya mtuhumiwa huyo kupanda kizimbani akisubiri kusomewa shitaka lake, Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka [DPP] Ali Amour Makame   amesema leo walikua wasikilize   shahidi ambae ni askari mpelelezi ila hakufika mahakamani kwani hayupo kazini yupo likizo. ‘’Mheshimiwa hakimu tunaomba uipangie sikunyengine ili tumuombe   shahidi wetu aje kutoa ushahidi hata kama amesafiri,’’ Alidai DPP. Hakimu wa mahakama hiyo Lusiano makoe nyengo amekubaliana na ombi hilo na kesi hiyo itaendelea tena tarehe 26/7/mwaka huu. Imedaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo siku ya tarehe 23/2/2021 majira ya 5;30 asubuhi, huko Likoni Kengeja wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba Alimuingilia kinyume na maumbile ambapo kufanya hiv

SHAHIDI AISHANGAZA MAHAKAMA

Image
NA FATMA HAMAD PEMBA  MTOTO mwenye miaka 17 ambae ni shahidi, ameishangaza mahakama ya Mkoa ‘B’ Chake chake kwa kuiambia kua alimtaja mtuhumiwa Ibrahim   Khamis Abdalla kwa shindikizo la wazazi wake tu, kwamba ndie aliempa ujauzito, lakini yeye hahusiki na ujauzito huo. Akitoa ushahidi wake   mbele ya mahakama hiyo, shahidi huyo ameeleza kuwa wazazi walimlazimisha kumtaja mtuhumiwa huyo,  kwanindie waliekuawa kimdhania.  Alidai kuwa mtuhumiwa ni rafiki yake wa mudamrefu, ingawa sie aliyempa ujauzito na aliamua kumtaja kutokana na sindikizo la wazazi wake. “Nakataa ujauzito sijapewa na Ibrahim nilipewa na mwanamme ambae tukikutana tu kwenye kampeni na wala si mfahamu kwao anapoishi,’’ alidai. Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka [DPP] Ali Amour Makame alidai kutokana na maelezo ya shahidi huyo kwa upande wao wanafunga ushahidi. ‘’Mheshimiwa tunafunga ushahidi wa kesi hii na tunaiachia mahakama yako iweze kutoa maamuzi,’’ alidai. Hakimuwamahak

JUMUIA YA WATU WASIONA [ZANAB] PEMBA WAOMBA MSAADA

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Jumuia ya watu wasiona [Zanab ] wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba imeitaka Serikali pamoja na watu wenye uwezo kuwapa msaada wa   kuwajengea jingo la Ofisi yao ili kuwaondoshea usumbufu kwa wanajumuia hao. Akizungumza na mwandishi wa habari mwenyekiti wa jumuia hiyo Suleimana Mansour Suleiman huko ofisini kwake Chake chake Pemba amesema   wanachangamoto kubwa ya uhaba wa vyumba katika jingo lao. Amesema Ofisi yao inawafanyakazi   mchanganyiko wa watu tofauti wakiwemo watu wenye ulemavu wa Ngozi, wenye ulemavu wa viungo na   wasiona   lakini wanachumba kimoja tu hawana sehemu nyengine   ya kufanyia shuhuli zao za kiofisi. Amefafanua kuwa unapofika wakati wa sala wanalazika wengine kukaa nje na kupishana   kwa ajili ya kutekeleza ibada ya sala.   ‘’Jengo letu ni dhaifu, Tunachumba kimoja tu hatuna hata chumba cha stara, ukiangalia tupo mchanganyiko wanawake na wanaume’’, Alisema mwenyekiti. Samba mba na hilo mwenyekiti huyo ameeleza kwa masi

FAMILIA YA AHMED AL FARSII KUTOKA DUBAI YA HIDI KUSAIDIA VIFAA VYA TIBA HOSPITALINI

Image
NA FATMA HAMAD PEMBA. Ugeni kutoka falme za kiarabu [Dubai] umeahidi kusaidi   vifaa vya   tiba kama vile vya upasuaji, usafishaji wa figo,   Exray, vifaa vya uchuguzi wa magonjwa ya akinamama na watoto, na huduma nyengine mbali mbali za matibabu katika hospitali za Wilaya Kisiwani Pemba.   Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui   amesema ahadi hiyo imefuatia ziara ya kutembelea hospitali hizo iliyofanywa kati ya uongozi wa wizara ya afya   na Ugeni huo   kujionea hali halisi ya utoaji wa huduma za afya katika hospitali ya   Wete,   Micheweni na Vitongoji pamoja na kusikiliza changamoto zilizopo.   Amesema baada ya kuwatembeza na kujionea katika hospitali hizo, Ugeni huo umejionea mahitaji ambayo yanahitajika ambapo wameyachukua na kwenda kuyafanyia kazi pamoja na   kuahidi kurudi baada ya miezi michache nayale ambayo yatashindwa kutekelezwa na ugeni huo wataangalia namna ya kuomba msaada kwa wahisani wengine.   ‘’Atahakikisha ametekeleza aha

Serekali kutoa adhabu kali kwa wafanyaji wa vitendo vya udhalilishaji.

Image
  Mama mmoja amevunja ukimya na kuiomba Serikali kutoa hukumu kali kwa watu wanaofanya ukatili ya kuwalawiti na kuwabaka watoto na wanawake ili kukomesha vitendo hivyo visitokea tena. Kauli ya mama huyo imefuatia baada ya tukio la kuhudhunisha la kuingiliwa kinyume na maumbile kwa mtoto wa mika 5 na kijana Mussa Saleh  Ali mwenye umri wa 16 huko wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba. Akizungumza kwa masikitiko makubwa mama wa mtoto huyo amesema tukio la kufanyiwa kitendo hicho mwanawe lilitokea wakati alipokwenda jisaidia vichakani majira ya saa 10 jioni baada ya nyumba yao kutokuwa na choo na kurudi kwao saa 12 jioni akitokwa na mchozi. Amesema alipo muhoji alimwambia alichomwa na ujiti, lakini mwisho wa siku alipombana zaidi na kumtishia  ndipo alisema kuwa  Mussa ndie aliyemfanya kitendo  kilichomtoa damu huku akimuamuru asiseme jambo hilo kwa mtu yeyote na akisema ataweza kumfanyia kitu kibaya. ‘’Mimi nilikua sina habari nikaambiwa na wenzake mbona hajarudi choni hapo nikaamu