WANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUANDIKA HABARI ZA VIJIJINI.


 

Afisa mdhamini wizara ya habri Vijana na Michezo Salum Ubwa amewataka wandishi wa habari kujikita zaid  Vijijini katika kuandika habari zao ili kuibua matatizo yanayo wakabili wananchi wa maeneo hayo.

Hayo ameyasema katika Kongamano la uhuru wa kujieleza upatikanaji wa habari, mitandao ya kijamii na uandaaji wa maudhui kwa vijana na majukwaa ya maendeleo kwa vijana huko  Camail  Chake chake Pemba.

Amesema vyombo vya habari ndio msemaji wa wasio na sauti, hivyo ni budi kwa wandishi wa habari kujitoa na kujituma ili kuona wananchi wa vijijini nawao wanapata fursa  ya kuzungumza na  vyombo vya habari  kutoa  kero zao na mamlaka husika na kuona  wanazitekeleza.

‘’Wandishi msiishie tu mjini nendeni vijijini kuna kero nyingi zinawakumba wananchi’’ Alisema afisa mdhamini.

Amesema  wananchi  wengi wa vijijini wanaendelea kuishi katika  matatizo kutokana na kukosa taluma na taratibu za ufuatiliaji  wa shida zao kwa vyombo husika jambo ambalo linapelekea kukosa haki zao.



Akiwasilisha mada  ya uhuru wa kujieleza na kupata habari mkufunzi wa mafunzo hayo Haji Nassor Mohd amewashauri vijana kuvitumia vyombo vya habari wakati wanapofanya shuhuli zao ili waweze kutambulika jambo ambalo litawasaidia kupata fursa mbali mbali za kimaendeleo.



Baadhi ya  wandishi walioshiriki mkutano huo wamesema bado jamii haijakua na mwamko wa kuvitumia vyombo vya habari kutoa malalamiko yao kutokana na mila na desturi walizo nazo vijijini kwao.



Nae meneja wa miradi kutoka  Zanzibar Youth Forum Almasi Mohd amesema lengo la kuepo kwa mradi unaolenga kukuza uwezo wa asasi za kiraia na ushirikiano katika utetezi wa kupata habari ni kutetea pamoja nakuwasilisha mambo ya msingi yanayohusiana na uhuru wa habari, upatikanaji wa habari pamoja  na uhuru wa kujikusanya.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.