Posts

Showing posts from December, 2022

BAADA YA BLOG YA PEMBA YA LEO KUIBUA KERO YA MWALIMU WA MADRASA MWENYE ULEMAVU KOKOSA SEHEMU SALAMA YA KUSOMESHEA SASA APATA UFADHILI WA KUJENGEWA.

Image
  BAADA YA  BLOG YA PEMBA YA LEO  KUCHAPISHA MAKALA -Mwalimu mwenye ulemavu   wa viungo ajengewa mdarassa Shumba vyamboni -Aibuka kuushukuru  mtandao  wa pemba ya leo, mfadhili, wanafunzi wasema jambo FATMA HAMAD, PEMBA JUNE  24 , mwaka 2022, Blog ya pemba ya leo, lilichapisha makala, ikielezea changamoto za ukosefu wa madrassa ya kisasa ya mwalimu wa madrasa mwenye ulemavu wa viungo. Mwalimu huyo Saada Khamis Hamad wa Shumba vyamboni wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, akikabiliwa na changamoto ya ukosefu sehemu rafiki na salama ya kusomeshea wanafunzi wake. Ndoto zake za kupata madrassa ya kisasa kwa ajili ya kufundishia wanafunzi wake, hakuwa nayo kabisa kwenye akili yake, hasa kwa vile alishasomesha miaka zaidi ya minne katika mazingira magumu. Kwa kweli alikua na kilio cha siku nyingi, cha kupata ufadhili wa kujengewa madrasa, ndipo mwandishi wa makala kupitia blog ya pemba ya leo Pemba, alipochapisha makala yake na kisha wafadhili kucho moza . Nilikua sin

WANAFUNZI WAPEWA MBINU ZA KUDHIBITI UDHALILISHAJI

  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wanafunzi     maskulini   wameaswa   kuepuka    kufanya   vitendo   vya   utovu wa nidhamu na badala yake wafuatilie masomo yao kwanza   ili waweze kufikia   katika   ndoto   zao. Hayo yamesemwa na   Afisa dawati wa jeshi la Polisi   wilaya ya Micheweni Mohd Ali wakati akizungumza na wanafunzi wa almadrasatul madyana imuslimina   iliyopo wingwi mtemani wilaya ya micheweni Kaskazini Pemba. Amesema kesi nyingi zinazoripotiwa zaidi   ni   za   watoto   kuanzia   miaka 14 hadi 16 jambo ambalo linapelekea kukosa kuendelea na masomo yao. ‘’Sasahivi ni wakati wa kusoma   tu nyinyi   msikubali kushawishika   mkajingiza kwenye starehe mtakosa haki zenu za elimu’’ alieleza afisa dawati. Kwa upande wake msaidizi wa sheria shehiya ya Micheweni   Riziki Ali Hamad amewataka wanafunzi hao kutoa tarifa kwa walimu wao ama wazazo wao wakati watakapoona kunakuwepo na viashiria vinavyopelekea udhalilishaji ili   viweze kuchukualiwa hatua   za kisheria   jambo ambalo lipaw

VIJANA WAHIMIZWA KUFANYA KAZI KWA BIDII.

Image
                           NA FATMA HAMAD FAKI PEMBA.   Vijana wamehimizwa kujiingiza katika vikundi vya mazozi pamojana mpira wa miguu ili waweze kujipatia fursambalimbalizakimaendeleo. Akizungumza na wanamichezo wampira wa miguu pamoja na wananchi mwanaharakati wakupambana na masuala ya udhalilishaji Khalfan Amour Mohamed katika shamra shamra ya kuelekea siku 16 ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto huko uwanja wa mpira wa michezo wa Majimaji uliopo Tumbe wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema udhalilishaji wa kijinsia umekua ni kilio kikubwa kwa wazanzibar waliowengi hivyo ni vyema vijana kujiepusha kukaa kwenye vigenge visivyo na tija kwao na badala yake wajikite zaid kwenye michezo. ‘’Niwasihi vijana wenzangu tuitumieni michezo, tuvitumieni vikundi vya mazoezi ili kujilinda na masuala ya udhalilishaj; alisema khalfan. Aidha amewasisitiza kuondosha muhali na kuwatayari kutoa ushahidi wakati utakapotokezea udhalilishaji kwenye familia zao. Kwa upande wake Tatu

WAZAZI WANYOOSHEWA VIDOLE

Image
                    NA FATMA HAMAD PEMBA. Wazazi na walezi wamenyoshewa kidole kwamba nawao ni moja ya chanzo kinachopelekea  vijana kujiingiza katika matendo     vya udhalilishaji wa kijinsia. Wakizungumza katika kongamano la maadhimisho ya asasi za kirai  la siku 16 za kupinga ukatili wa wanawake na watoto wanafunzi wa  skuli ya msingi mitiula wete Pemba wamesema wazazi wamekua hawana tabia za kufuatilia nyenendo za watoto wao wakati wanapotoka kwenda madrasa pamoja na shuleni. Wamesema wapo baadhi ya wanafunzi wanatabia wanapondoka skuli hawafiki majumbani kwao wanaishia vichochoroni hivyo  wazazi  kuweni makini juu ya watoto wenu msiwachie fursa mpaka wakajisahau. ‘’Unapotoka nyumbani  mzazi hakuulizi  unakwenda wapi na wala unarudi mda gani  yani mda wako mwenyeo tu na safari zako hakuna wa kukubugudhi’’ walisema wanafunzi. Bimkubwa Issa Omar mwanafunzi kutoka chuo cha afya wete amesema Kuwepo kwa masomo ya ziada yasiyo na mpangilio yanachangia watoto kufanyiwa udhalilishaji. ‘’Si

WAZAZI WAPEWAMBINU.

Image
                           NA FATMA HAMAD PEMBA. Kukosekana  kwa  malezi  ya  pamoja  [zamani]  ni  moja  ya  sababu  inyochangia   kwa  kiasi  kikubwa kuongezeka  kwa  matendo  ya  udhalilishaji  wa  kijinsia katika jamii. Hayo yamelezwa na mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania tamwa  ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said katika kongamano la madhimisho ya asasi za kiraia  ya  siku 16 ya  kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto huko micheweni mkoa wa kaskazini Pemba. Amesema licha ya elimu inayotolewa juu ya udhalilishaji lakini bado  suala hilo  linazidi kuongezeka hivyo wakati umefika kwa wazazi kukachini  ili kurudisha malezi ya zamani hali ambayo itakua ni muarubaini wa hayo. ‘’kwa kweli hali imekua tete  jamani suala la kukaa kila mtu na mwanawe imeshapitwa na wakati tukaeni tutafakari ni hatari sana’’ alieleza kwa masikitiko mratibu tamwa. Kwa upande wake afisa dawati la jinsia la wanawake na watoto wilaya ya micheweni Mohamed Ali ameitaka jamii  kuanzi

WANAHARAKATI WAPEWA MBIN

Image
                                     NA FATMA HAMAD PEMBA. Wanaharakati pamoja na asasi mbali mbali za kiraia zimekumbushwa kuwa mstari wa mbele   kuwasimamia na kuwatetea   wanawake   na watoto    wakati wanapopatwa na matatatizo   ikiwemo udhalilishwaji na utelekezwaji ili   kuona wanapata   haki   zao. Ukumbusho huo umetolewa na mkuu wa kituo cha polisi micheweni Said Khamis Juma  katika kongamano la madhimisho ya asasi za kiraia   ya   siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto huko micheweni kisiwani Pemba. Amesema asasi za kiraia   zinatambulika kisheria na kimataifa hivyo ni wakati wa kujitowa na kuwatetea wanawake na watoto wanapodhalilishwa ili kuona   hatua zinachukuliwa jambo ambalo litapunguza vitendo hivyo. ‘’Asasi za kiraia mnanafasi kubwa hivyo ni wajibu wenu kuwatetea na kuhakikisha   wanawake   na watoto wanapata haki zao zinazostahiki wakati zinapovunjwa’’alisema mkuu wa kituo. Alieleza kuwa udhalilishaji si jambo la kufanyiwa doria kwani