WANAHARAKATI WAPEWA MBIN

 







                                   NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wanaharakati pamoja na asasi mbali mbali za kiraia zimekumbushwa kuwa mstari wa mbele  kuwasimamia na kuwatetea  wanawake  na watoto   wakati wanapopatwa na matatatizo  ikiwemo udhalilishwaji na utelekezwaji ili  kuona wanapata  haki  zao.

Ukumbusho huo umetolewa na mkuu wa kituo cha polisi micheweni Said Khamis Juma  katika kongamano la madhimisho ya asasi za kiraia  ya  siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto huko micheweni kisiwani Pemba.

Amesema asasi za kiraia  zinatambulika kisheria na kimataifa hivyo ni wakati wa kujitowa na kuwatetea wanawake na watoto wanapodhalilishwa ili kuona  hatua zinachukuliwa jambo ambalo litapunguza vitendo hivyo.

‘’Asasi za kiraia mnanafasi kubwa hivyo ni wajibu wenu kuwatetea na kuhakikisha  wanawake  na watoto wanapata haki zao zinazostahiki wakati zinapovunjwa’’alisema mkuu wa kituo.

Alieleza kuwa udhalilishaji si jambo la kufanyiwa doria kwani maranyingi hufanywa na watu wa karibu kwenye familia  bali ni suala linalohitaji ushirikiano wa kila mmoja iwe jamii, Serikali na hata asasi za kirai kuhakikisha  wahalifu wa matukio hayo wanafichuliwa na kupelekwa kwenye  vyombo vya sheria.

‘’Udhalilishaji sio jambo la kuchezea jamani hivyo ni lazima  kila mmoja kwa nafasi yake atoe ushirikiano wa hali ya juu ili kuondosha tatizo hili linalokatisha ndoto za wanawake na watoto’’ alisema kwa huzuni mkuu wa kituo.



Akitoa nasaha katika kongamano hilo mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania tamwa ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amesema wakati umefika kwa wazazi kukaa chini na watoto wao wa jinsia zote bila ya aibu kuwafundisha madhara ya udhalilishaji pamoja na  kujitambua ili waepuke  kujingiza katika janga hilo.



Nao washiriki wa kongamano hilo wamesema nivyema wanaharakati kupita kijiji hadi kijiji kuendelea kuielimisha jamii kwani imeonekana bado wapo wazazi wamekua wakikwepa majukumu yao kwenye fanilia na kusababisha kutokea kwa udhalilishaji kwa wanawake na watoto.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.