Posts

Showing posts from January, 2023

WADAU WAOMBA SHERIA ZINAZOHUSU MASUALA YA UDHALILISHAJI ZIFANYIWE MAREKEBISHO

Image
                                  NA FATMA HAMAD PEMBA. Mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amewataka wandishi wa habari kupaza sauti zao   kwa kuzisemea sheria mbali mbali   zenye mapungufu     ambazo zinazohusu masuala ya udhalilishaji wa kijinsia   ziweze kufanyiwa marekebisho ili zinaendana na hali ya sasa. Mratibu huyo ameyasema hayo huko ofisini kwake   Mkanjuni Chake chake wakati akifunga mafunzo ya siku mbili   yanayohusu   mradi wa kuhamasisha hatua za kitaifa dhidi ya vitendo vya udhalilishaji Zanzibar kwa wandishi wa vyombo mbali mbali kisiwani Pemba . Amesema licha juhudi mbali mbali zinazochukuliwa ili kuondosha udhalilishaji lakini bado kuna vifungu vya sheria vinaleta ukakasi jambo ambalo linakwaza   harakati za utetezi dhidi ya masuala hayo. ‘’Vipo vifungu mbali mbali vya sheria vinakandamiza   masuala ya udhalilishaji hivyo ni jukumu lenu wandishi wa habari kuvipiga kelele ili kuona vinarekebishwa na

WANDISHI WATAKIWA KUZISEMEA KERO ZINAZOKATISHA NDOTO ZA WANAWAKE, WATU WENYE ULEMAVU NA VIJANA

Image
                                                       NA FATMA HAMAD PEMBA.   Wandishi wa habari wametakiwa kuibua na kuzisemea kero zinazo wakabili Wanawake, Vijana pamoja na watu wenye ulemavu ambazo zinapelekea kuwakosesha fursa   mbali mbali za kimaendeleo. Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa hama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa njia ya mtandao kwa wandishi wa habari wa vyombo mbali mbali kisiwani Pembakatika mafunzo ya mradi wa kuhamasisha hatua za kitaifa dhidi ya vitendo vya udhalilishaji Zanzibar . Amesema Wandishi wa habari wanamchango mkubwa katika kuisaidia jamii kupiga hatua kimaendeleo. Hivyo amesema kuwa wakati umefika kwa wandishi wa habari kuzisemea  kero zinazo kosesha kupata haki pamoja na fursa mbali mbali ikiwemo ya uongozi. ‘’Wandishi wa habari endeleeni kupaza sauti kwa kuzitetea hangamoto zinazowakumba wanawake, watu wenye ulemavu, Vijana ili kuona nawao wanaingia katika ngazi za maamuzi’’ alisema Bi

WASAIDIZI WA SHERIA WAHIMIZWA KUJITUMA KWA BIDII.

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Jumuiya   za  wasaidizi wa  sharia  zimetakiwa  kuanzisha    miradi mbali  mbali  ya  kimaendeleo  ambayo  itawapatia    fursa   zitakazowasaidia  kupata  maslahi  katika jumuia  zao. Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi kutoka jumuia ya wasaidizi wa sheria wa wilaya ya micheweni Moh’d Hassan Ali huko ofisi za wasaidizi wa sharia  iliyopo Wingwi Mapofu kaskazini  Pemba. Amesema jumuiya ya wasaidizi wa sharia sio jumuia inayotengeneza kipato, lakini ni budi kuwepo na miradi ambayo itasaidia kufikia lengo la utoaji wa msaada wa kisheria kwa jamii bila ya kutegemea ufadhili. ‘’Wasaidizi wa sheria mnajukumu la kuwasaidia wananchi wakati wanapopata matatizo hivyo msikae tu mkategemea ufadhi bali na nyinyi jiongezeni ili muweze kuifikia jamii kila pembe’ alieleza mwenyekiti wa bodi. Aidha amewataka wasaidi wa sharia kufanya kazi na vikundi vya wajasiamali  pamoja na  wafanya biashara  ili kuhakikisha nawao wanazifahamu sharia na katiba za Nchi. ‘Wapo wa

WASAIDIZI WA SHERIA WAWAPIGA MSASA WAZAZI

Image
                       NA FATMA HAMAD PEMBA. Jamii imekumbushwa kuacha tabia ya kuwaficha wahalifu wanaofanya vitendo vya udhalilishaji katika familia zao jambo ambalo linachangia kuongezeka kwa vitendo hivyo. Ukumbusho huo umetolewa na msaidizi wa sharia kutoka jumuia ya wasaidizi wa sharia ya wilaya ya Micheweni Salim Hemed Salim wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya Shumba vyamboni iliyopo wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto bado vinaendelea kufanyika, hivyo ni wakati wanajamii kuvunja ukimya na kuwafikisha kwenye vyombo vya sharia wahalifu wanatenda makossa haya ili kutiwa hatiani. ‘’Niwambie wazazi wenzangu kama tutaendelea kuwaficha na kuona muhali tutawafanya watoto waendelee kukumbwa na kadhya hiyo’’ alisema msaidizi wa sharia. Mapema msaidizi wa sharia kutoka shehiya ya Shumba vyamboni Said Masoud Rashid amesema ni vyema wazazi na walezi kukaapamoja na kurudisha malezi ya pamoja katika

UONGOZI WA HALMASHAURI MICHEWENI WASHAURIWA.

  NA FATMA HAMAD PEMBA. Spika wa baraza la wawakilishi Zubeir Ali Maulid ameutaka uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Micheweni   isiwatoleshe   tozo kubwa wajasiriamali   na wafanya biashara wadogo wadogo   ambayo itakwamisha   kuendeleza   biashara yao. Mheshimiwa   Zubeir   ameyasema hayo wakati akifungua soko la wajasiriamali huko Tumbe wilaya ya   Micheweni   Mkoa   wa   Kaskazini Pemba. Amesema lengo la Serikali ni   kuondoa kero   za kuhama hama na kuainua kiuchumi wajasiriamali hivyo   basi watolesheni tozo ngogo ambazo zinaendana na biashara zao jambo ambalo litawafanya waendeleza biashara zao na kujipatia kipato cha halali. ‘’Niwaombe nduzangu wa halmashauri   wajasiriamali wengi ni wanyonge hivyo msiwatoleshe kodi kubwa wafanya biashara wanaofanya biashara zao katika soko hili ’’ alisema Mheshimiwa Zubeir. Aidha amewataka wafanya biashara na wajasiriamali kulitumia eneo hilo maalumu   kwa ajili ya shuhuli zao za biashara kwani kufanya hivyo kutasaidia kuipatia Serika