UONGOZI WA HALMASHAURI MICHEWENI WASHAURIWA.

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Spika wa baraza la wawakilishi Zubeir Ali Maulid ameutaka uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Micheweni  isiwatoleshe  tozo kubwa wajasiriamali  na wafanya biashara wadogo wadogo  ambayo itakwamisha  kuendeleza  biashara yao.

Mheshimiwa  Zubeir  ameyasema hayo wakati akifungua soko la wajasiriamali huko Tumbe wilaya ya  Micheweni  Mkoa  wa  Kaskazini Pemba.

Amesema lengo la Serikali ni  kuondoa kero  za kuhama hama na kuainua kiuchumi wajasiriamali hivyo  basi watolesheni tozo ngogo ambazo zinaendana na biashara zao jambo ambalo litawafanya waendeleza biashara zao na kujipatia kipato cha halali.

‘’Niwaombe nduzangu wa halmashauri  wajasiriamali wengi ni wanyonge hivyo msiwatoleshe kodi kubwa wafanya biashara wanaofanya biashara zao katika soko hili ’’ alisema Mheshimiwa Zubeir.

Aidha amewataka wafanya biashara na wajasiriamali kulitumia eneo hilo maalumu  kwa ajili ya shuhuli zao za biashara kwani kufanya hivyo kutasaidia kuipatia Serikali mapato.

Akitoa  maelezo  ya  Kitaalam  juu ya mradi huo Katibu  Mkuu  Ofisi  ya  Rais Tawala za mikoa, Serikali za mitaa na Idara maalum za SMZ  Issa  Mahfudh Haji amesema  mradi huo umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 1 Milioni miatano  thalathini na tatu Laki tatu Arubaini na tatu mia tisa na thathini na tano.

Amesema mradi huo utawanufaisha wajasiriamali mbali mbali wakiwemo wa biashara ya nguo, Chakula na mboga mboga.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.