JAMII YASHAURIWA KULEA WATOTO KATIKA MALEZI YA PAMOJA
NA FATMA HAMAD, PEMBA JAMII imetakiwa kushirikiana katika malezi ya pamoja ili kupatikana kwa kizazi chenye heshma na madili mema. Ushauri huo umetolewa na Kaimu Mratibu kutoka Ofisi ya mufti Pemba Said Khalfan Issa wakati akizunumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake Chake chake amesema ni vyema jamii kurudisha Mila, Silka na tamaduni za kizanzibar katika kuwalea Vijana. Alisema zamani mtoto ilikuwa halelewi ni baba na mama pekee, bali kila mmoja alikuwa na nafasi yake, kama vile mwalimu wa madrasa, Shuleni na hata kwa wazazi wengine. ‘’Niombe jamii turudisheni tamaduni zetu za kuwalea watoto wetu katika malezi ya pamoja, ili waepukane na vitendo viou ikiwemo udhalilishaji pamoja na ukahaba,’’alisema. Alifahamisha kuwa sasahivi kumekuwa kukijitokeza viashiria vingi ambavyo ni hatari kwa watoto,hivyo wakati umefika kurudi katika misingi ya dini inavyoelekeza juu ya malezi,ili kulinda heshma ya wazanzibar. ‘’Kwa kweli hali imekuwa mbaya, kila mmoja hana amani juu