UZAZI WA MPANGO UNAVYOINUA WANAWAKE KIUCHUMI,
NA FATMA, HAMAD PEMBA
KUPANGA
kutamka au kufanya jambo kunasaidia kupata mafanikio mazuri au kupunguza hatari
na athari za matatizo.
Umuhimu huu wa kupanga pia unaonekana katika
uzazi kwa vile uzazi wa mpango umethibitisha kuwa na faida nyingi kwa mama,
mtoto, familia na taifa kwa jumla.
Uislamu umeeleza wazi kuwa uzazi wa
mpango sio unaplekea kuwa na afya njema ya mzazi na mtoto tu, bali pia furaha,
amani na mapenzi katika familia.
Baadhi ya watu katika jamii
wamekuwa na imani potofu kwamba, uzazi wa mpango unapunguza
kizazi na kusababisha matatizo kama vile kansa na
kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi.
Hili halina ukweli kwa sababu utafiti na
ushuhuda wa wanawake waliojiunga na mpango huu unathibitisha kwamba hio ni
dhana isiyokuwa na mshiko.
Asha Khamis wa Micheweni,
Pemba, anafurahia uamuzi wake wa kujiunga na auzazi wa mpango na
kueleza kwamba ulimsaidi kupata muda wa kulea vyema watoto na kufanya biashara
yake ya kuuza uji na mandazi.
‘’Nilikuwa nikinyonyesha mtoto wangu kwa
muda wa miaka miwili, na hii ilinipatia muda wa kufanya shughuli zangu za
biashara kwa ajili ya kuendesha maisha yangu,’’alisema huku akitabasamu.
Amina Omar Mselem aliyejipatia
watoto 7 waliozaliwa kwa kupishana muda mrefu kidogo alisema uzazi wa mpango
ulimpa fursa ya kushiriki katika harakati mbali mbali
za kijamii.
‘’Nilikua nikitumia uzazi wa
mpango na hii ilinipa muda wa kupumzika vizuri na kwenda
harusini, msibani, Kwenye vikoba na huku nikufurahia kulea , kucheza na
watoto na kuwa na maisha ya furaha na mume wangu,’’alieleza Amina.
Maryam Said mama wa
watoto wa 4, alisema alianza kutumia uzazi wa mpango
mara tu baada ya kupata mtoto wake wa kwanza.
‘’Nimekuwa nikitumia uzazi wa mpango kwa muda mrefu na sjapata tatizo lolote la kiafya,’’ alieleza Maryam.
Utafiti na ushuhuda unaonyesha wazi kuwa uzazi wa mpango unamsaidia sana mzazi na watoto na ndio maana wataalamu wa afya wanaishajiisha jamii kutumia mpango huu kwa vile ni salama na hauna madhara.
WATALAMU WA AFYA.
Mtaalamu wa afya
wa ofisi ya huduma za mama na mtoto
katika Hospitali ya Chake chake, Fatma Suleiman Daud,
alisema njia za uzazi wa mpango hazina madhara bali
ni tiba kwa afya ya binadamu.
‘’Mtu yoyote atakaeugua ugonjwa wa Kansa
dozi yake ya mwanzo anayotakiwa kutumia ni dawa ya uzazi wa
mpango,’’alifafanua.
Alisema uzazi wa mpango pia unasaidia
kuwa na mzunguko mzuri wa hedhi kwa akina mama ambao
hawaingiii kwenye siku zao.
Uzazi wa mara kwa mara unapelekea
kushuka na kupasuka fuko la uzazi na hii huhatarisha
maisha ya mama.
‘’Hali za wanawake wengi wanaozaa papo
kwa pao huwa na upungufu mkubwa wa damu,’’alieleza.
Alisema yeye pia anatumia uzazi wa
mpango na kwa sasa anao watoto wawili, wa kwanza ana
miaka 7 na wa pili mwaka mmoja na
nusu.
‘’Mimi
nilijiunga na uzazi wa mpango kwa
kuanzia njia ya kijiti na
sasa ninatumia Kitanzi.’’alieleza.
Alisikitishwa kuona ndoa nyingi za watu wa
Zanzibar zinapelekea mwanamke kujikuta na mke wenza kutokana na mwanamke kuzaa
mara kwa mara, jambo ambalo hupelekea kutokuwepo amani katika
nyumba na hubidi mume aongeze mke mwengine,’’ alifahamisha.
Mengi yanasemwa
na kutumia visingizio mbali mbali, lakini ukweli ni kwamba uzazi wa mpango
ulikuwepo tokea enzi za Mitume.
Maryam Ali Said , Mratibu wa huduma
za mama na mtoto Pemba, amesema maradhi humpata mtu yoyote, na
pasitafute kisingizio cha kusema sababu ni uzazi wa mpango.
‘’Tunao watu wengi walioutumia uzazi wa mpango
mpaka walipofikia umri wa uzee na hawajapata tatizo lolote la kiafya,’’
amesisitiza.
Amesema wanaume wengi wanapata ugonjwa
wa kansa na jee hii utasema sababu yake ni uzazi wa mpango,
aliuliza.
Alifahamisha kuwa maziwa ya mama ndio chakula
bora pekee kinacho mjenga mtoto kuwa na afya bora
na kukuwa kimwili na kiakili.
‘’Kitaalamu mtoto anatakiwa anyonye
maziwa ya mama kwa miaka 2, kwani maziwa ya mama ndio yenye
virutubisho vinavyohitajika kwa ukuaji mzuri wa mtoto,’’amefahamisha.
Baadhi madhara ya uzazi wa
mpango yanayotajwa na wanawake ni pamoja na kupata ugumu wa kushika mimba
baada ya kutumia uzai wa mpango, kutokwa damu mara kwa mara, kupungua au
kuongezeka kwa mwili, kuongezeka hamu ya kula, kupotea kwa hamu ya tendo la
ndoa, mabadiliko ya siku za hedhi na maumivu ya kichwa.
Lakini utafiti wa kitaalamu umeonyesha sababu zote hizo ni zaidi za nadharia kuliko hali halisi.
MTAALAMU WA AFYA YA UZAZI
Rahila Salim Omar, mtalamu wa
afya ya uzazi, amesema zipo njia nyingi za kupanga uzazi
ambazo zote ni salama na miongoni mwao ni
zile za kisayansi na za kisasa ambazo hazina madhara.
Alisema miongoni mwa njia hizo ni kutumia
Kitanzi [Kijiti] kwa mama ambaye hajazaa sana, sindano, vipandikizi, mipira ya kiume na ya
kike [Kondom] na
zote hizi ni salama, na hutolewa kulingana na afya ya mama.
‘’Sio kweli kwamba ukipanga uzazi unapata
matatizo, Tusidanganyane kwani kitaalamu hilo halipo’’, alisistiza.
Wapo ambao hutumia njia za asili za uzazi,
kama ya kutegemea kalenda. Hii hufuata mzunguko wa hedhi au kumwaga mbegu za
kiume nje ya njia ya uzazi.
Sheikh Abdalla Nassor Abdalla kutoka Jumuia ya Maimamu Pemba (JUMAZA) amesema Uislamu unaukubali uzazi wa mpango na kisheria mtoto anatakiwa anyonye maziwa ya mama kwa miaka 2 na hapo ndipo mama abebe ujauzito mwengine.
Mwenendo huu, amesema, unasaidia kuimarisha afya ya mama na mtoto,.
Sheikh Abdalla alifahamisha kwamba njia za
kufunga uzazi zipo kwa wanawake na wanaume, na sio kwa wanawake tu. Kwahivyo ni
vyema wanaume nao pia wazitumie.
Kwa mujibu wa takwimu za kituo cha huduma za
mama na mtoto Pemba wa kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu, watu 4020
walijiunga na uzazi wa mpango. Kati yao wanaume ni 63 na wanawake 3957.
Katika Hospitali ya Mkoani wanawake ni 711,
wanaume 17, Chake chake wanawake 1228, wanaume 18,Wete wanawake 1085,
wanaume 13, na kwa Micheweni wanawake ni 873 na wanaume 18.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa
juu ya matumizi ya uzazi wa mpango imeonyesha ongezeko katika baadhi ya nchi,
ikiwemo Tanzania. Takwimu zinaonyeha kwa sasa ni asilimia 27 ya
Watanzania wanatumia njia hizo, zikiwemo sindano, vipandikizi na mipira ya
kiume na ya kike.
Hofu ya njia za uzazi wa
mpango
Utafiti mpya wa Shirika la afya Duniani (WHO) umebaini kuwa theluthi mbili ya wanawake wenye uwezo wa kubeba mimba na ambao wana nia ya kuchelewesha kupata ujauzito au kudhibiti idadi ya watoto huacha kutumia huduma za uzazi wa mpango kwa hofu ya madhara ya huduma hizo.
Uzazi wa mpango sio tu ni suala la haki za binadamu bali pia ni kitovu cha uwezeshaji wa wanawake, kupunguza umasikini na kufikia malengo ya maendeleo endelevu - SDG’s (Uzazi wa mpango ni haki ya binadamu: UNFPA- 11 Julai 2018 ).
Comments
Post a Comment