Posts

Showing posts from October, 2022

WANDISHI WA HABARI WAPEWA MBINU.

Image
  FATMA HAMAD PEMBA. Wandishi wa habari  Nchini wamekumbushwa  kuitumia mitandao ya kijamii kwa kuandika habari zenye ukweli na  zenye  ubora  ili kuepuka    kuingia  katika migoghoro isio  ya lazima. Ukumbusho huo umetolewa na Mwenyekiti wa Jumuia ya wandishi wa habari Pemba Pres Clab [PPC]  Bakar Mussa Juma wakati akizungumza na wandishi wa habari wa mitandao katika mafunzo  juu ya ulinzi na usalama wa mitandao ya kijamii huko ofisi ya  Ppc  Chake chake Pemba. Amesema mitandao ya kijamii ndio chombo kinachofikisha ujumbe haraka kwa jamii hivyo ni vyema kuwa makini wakati wanaporusha habari zao ili iweze kuwajenga na kuwa huru katika kazi zenu. Amesema vyombo vya habari ndio sauti ya wasio na sauti  hivyo sasa ni wakati wa  Wandishi kubadilika  na  waweze kuandika habari zenye uhakika ambazo zitaleta tija kwa Jamii.  ‘’Mitandao ya kijamii  ndio chombo kinachofikisha ujumbe kwa haraka katika jamii hivyo lazima muwe makini sana katika kutumia hii mitandao  kwani kumekua na wat

WANAOFANYA MITIHANI WAONYWA

Image
NA FATMA HAMAD PEMBA. Wanafunzi wanaofanya mitihani ya Taifa wameonywa   kujiepusha na vitendo vya udanganyifu   wakati wakiwa katika mitihani yao ambavyo vitapelekea   kufutiwa   kwa   matokeo yao. Nasaha hizo zimetolewa   na mbunge mstaafu wa jimbo la Kiwani Abdala Haji Ali katika hafla ya kuwaaga na kuwaombea duwa wanafunzi wanaofanya mitihani ya taifa   huko Skuli ya Chambani wilaya ya Mkoani mkoa wa Kusini Pemba. Amesema nidhamu   ni moja ya sababu inayomfanya mwanafunzi kufanya vizuri hivyo ni vyema wawe na juhudu ya hali juu   kwenye masomo   ili muweze kuja kufaulu   mitihani yao. ,,Niwasihi watahiniwa   muwe na nidhamu ya hali ya juu msije mkakiuka sharia za mitihani kwani itakuja kuwa kulio kwenu’’ alisema mbunge mstaafu. Kwa upande wake mwalimu mkuu skuli   ya   msingi    Said Faki Hassan amewataka wazazi na walezi wa wanafunzi wanaosoma skulini hapo kuwa na mashirikiano ya pomoja kati yao na walimu kwani kufanya hivyo ndio msingi mkuu utakaosaidia kuleta maendeleo  

MTUHUMIWA AOMBA RUHUSA

  NA FATMA HAMAD PEMBA.   Mtuhumiwa wa kesi ya ulawiti Nuhu Kombo Nuhu ameiambia mahakama   ya   mkoa inayoshuhulikia kesi za   udhalilishaji iliyopo mkoa wa Kaskazini Pemba kumpa ruhusa kwenda kutafuta mashahidi ili waweze kuja kutoa ushahidi.   ‘’Mheshimiwa hakimu mimi nimo ndani nitawapata vipi hao mashahidi naomba niruhusu nitoke nikawatafute’’ alisema mtuhumiwa.   Hakimu wa mahakama hiyo Ali Abdulrahman Ali alimtaka mtuhumiwa huyo kutaja majina ya mashahidi   waweze kupelekewa barua ya wito ili waweze kufika mahakamani na kutoa ushahidi.   ‘’Wewe upo rumande hatuwezi kukuruhusu kwenda kutafuta mashahidi kama umeshindwa sema tufunge ushahidi’’ alisema hakimu.   Hivyo utaendelea kubaki rumande hadi tarehe 24/10/2022 kwa ajili ya kuendelea na hatua ya utetezi.   Tukio hilo lilitokea tarehe 13/ 12/ 2021 majira ya sa moja asubuhi huko kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wa   Kaskazini Pemba ambapo mtuhumiwa alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili. Ilidaiwa kuwa kufanya

UKOSEFU WA WALIMU MJUMUISHI BADO NI KIKWAZO KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

            NA FATMA HAMAD PEMBA. 17/10/2022 Wazazi   wa watoto wenye ulemavu   mkoa wa kaskazini Pemba wameikumbusha Serikali ya mapinduzi Zanziber   kuboresha miundo mbinu ya wanafunzi wenye ulemavu maskulini ikiwemo kuweka walimu wanaojua lugha za alama ili watoto wao nawao waweze kupata haki yao ya elimu.   Wakizungumza   na mwandishi wa habari hizi   kwa nyakati tofauti wamesema watoto   wengi wenye ulemavu bado wanaendelea kuikosa haki yao ya elimu kutokana na kukosa wakalimani.   Mmoja wa wazazi hao bi Asha Omar kutoka micheweni alisema   kuwa Skuli nyingi za mkoa wa kaskazini   Pemba hususan wilaya ya micheweni hazina walimu wenye ujuzi wa elimu mjumuishi hivyo wanashindwa kuwapeleka skuli watoto   wao waliopata mtihani wa ulemavu.   ‘’Tunakilio kikubwa jamani watoto wetu wenye ulemavu hawasomi wanakaa tu majumbani kwani hata wakienda skuli hawafahamu chochote kinachofundishwa’’alieleza bi Asha. Kwa upande wake baba mzazi wa Salum  Said Asaa mwenye ulemavu wa macho  k

MKUU WA MKOA AIPA TANO JKU

                      NA SAID ABRAHMAN PEMBA. MKUU wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa amesifu mbinu zinazochukuliwa na Jku za utumiaji wa eneo dogo la uzalishaji Kwa kupata mazao mengi    Alieleza kuwa Tanzania Bara wamekuwa wakitumia ardhi kubwa Kwa Kilimo huku rasilimali wanazotumia ni kidogo.   Mkuu huyo wa Mkoa aliyasema hayo Chamanangwe Wilaya ya Wete, wakati alipokuwa akiangalia shughuli mbali mbali zinazofanya na Jku, kwenye maonesho ya siku ya chakula Duniani yanayoendelea huko.   Fatma alisema kuwa amefarajika sana kuona utaalamu ambao unafanywa na Jku wa kutumia  ardhi ndogo katika shughuli za Kilimo Kwa kupanda mazao mchanganyiko huku mavuno yake yakiwa mengi.   "Nimefarajika sana kuona kumbe mkulima anaweza kulima sehemu ndogo tu lakini mavuno yake yakiwa  ni mengi, Kwani sisi kule kwetu tumekuwa tukilima maeneo makubwa na wakati mwengine mavuno yanakuwa hafifu," alisema Fatma.   Nae Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba Yussuf Ali aliwataka vijana kujiunga na Jku

WAZAZI WAPEWA MBINU YA KUWALEA WATOTO WENYE ULEMAVU WA AKILI.

                         NA FATMA HAMAD PEMBA 12/10/2022. Wazazi na walezi wanaoishi na watoto wenye ulemavu   wa akili wametakiwa kuzidisha ulinzi zaidi kwa watoto hao ili kuwalinda na vitendo vya udhalilishaji. Wito huo umetolewa na mratibu wa jumuiya ya watu wenye ulemavu kisiwani Pemba [ZAPDD]   Khalfan Amour Mohd wakati akizungumza na wanachama wa jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili huko Kiuyu mbuyuni wilaya ya Micheweni mkoa wa Kasakazini Pemba kufuatia kuzuka kwa vitendo vya udhalilishaji wanavyofanyiwa watu wenye ulemavu wa akili. Alisema   wapo watu   wamekua wakiwachukua watoto wenye ulemavu wa akili kwa ajili ya   kumaliza haja zao za matamanio, hivyo wazazi mnajukumu kubwa la kuhakikisha mnakuwa na ulinzi wa hali juu ili kuhakikisha mda wote wapo katika hali ya amani na usalama vijana hao. ‘’Licha ya halingumu mlizonazo   za kimaisha   lakini tuwashuhulikieni watoto wetu wenye ulemavu tusiwabeze jamani’’ alisema mratib khalfan. Kwa upande wake   msaidizi mwenyek

MUHALI BADO NI TATIZO.

  NA FATMA HAMAD PEMBA. Jamii imekumbushwa kujitokeza kwa wingi mahakamani kutoa   ushahidi kwa kesi za udhalilishaji    jambo ambalo   litasaidia   wahalifu wa makosa hayo kutiwa hatiani na kupata hukumu. Ukumbusho huo umetolewa na Hakimu wa mahakama aneshughulikia kesi za udhalilishaji   Mkoa wa Kusini Pemba Muumin Ali Juma   wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake amesema licha   ya Serikali ya Mapinduzi kuweka mikakati mbali mbali ili kuondosha makosa hayo,   ikiwemo uwepo wa mahakama maalumu lakini bado wananchi hawajataka kutoa ushirikiano juu ya mahakama hiyo. Amesema wananchi waliowengi hawataki kusimama mahakamani kutoa ushahidi na badala yake   huyakalia kitako na kuyafanyia suluhu matukio ya udhalilishaji wakati yanapotokezea katika familia zao   hali ambayo inasababisha kesi nyingi kufutwa mahamani kutokana na kukosa ushahidi. ‘’ kwa kweli   tunakilio kikubwa   Jamii   wenyewe hawajataka kuyaondosha matendo ya udhalilishaji’’ alisema hakimu

HALMASHAURI NA MABARAZA YA MIJI YAHIMIZWA USHIRIKIANO.

                                       NA SAID ABRAHMAN PEMBA. 12/10/2022 WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Massoud Ali Mohammed  aliwataka  watendaji  wa  halmashauri  ya Micheweni, baraza la Mji Wete pamoja na Madiwani kuwa na mashirikiano katika utendaji wao kazi za kila Siku .    Alisema kuwa hakuna miujiza yeyote ambayo inayoweza kutokezea wakati watendaji hao wakiwa hawana ushirikiano nzuri katika majukumu yao.   Waziri Massoud aliyesema hayo huko katika Ukumbi wa Jamhuri hall Wete wakati akizungumza na watendaji hao na kuwaeleza kuwa mashirikiano ndio kitu pekee ambacho kitawafanya kuwa na Ari, umoja na moyo wa kufanya kazi.   Alifahamisha kuwa kumekuwa na baadhi ya watendaji kutoka katika mabaraza ya miji,halmashauri au hata Madiwani kuweka vikwazo katika miradi ya maendeleo Kwa madai tu mrado huo umepelekwa na mtu Fulani na hivyo kuuwekea pingamizi jambo ambalo sio sahihi hata kidogo.   "Moja ya changamoto ambayo iko S

MABARAZA YA MIJI NA HALMASHAURI ZA HIMIZWA USHIRIKIANO

                                       NA SAID ABRAHMAN PEMBA. 12/10/2022 WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Massoud Ali Mohammed  aliwataka  watendaji  wa  halmashauri  ya Micheweni, baraza la Mji Wete pamoja na Madiwani kuwa na mashirikiano katika utendaji wao kazi za kila Siku .    Alisema kuwa hakuna miujiza yeyote ambayo inayoweza kutokezea wakati watendaji hao wakiwa hawana ushirikiano nzuri katika majukumu yao.   Waziri Massoud aliyesema hayo huko katika Ukumbi wa Jamhuri hall Wete wakati akizungumza na watendaji hao na kuwaeleza kuwa mashirikiano ndio kitu pekee ambacho kitawafanya kuwa na Ari, umoja na moyo wa kufanya kazi.   Alifahamisha kuwa kumekuwa na baadhi ya watendaji kutoka katika mabaraza ya miji,halmashauri au hata Madiwani kuweka vikwazo katika miradi ya maendeleo Kwa madai tu mrado huo umepelekwa na mtu Fulani na hivyo kuuwekea pingamizi jambo ambalo sio sahihi hata kidogo.   "Moja ya changamoto amba

JESHI LA KUJENGA UCHUMI [JKU] LAPEWA NENO

                                  NA SAID ABRAHMAN PEMBA. NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt, Abdalla Juma Sadalla (Mabodi) amelitaka jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU) kujitoa na kutoa elimu Kwa wananchi juu ya kilimo Bora ambacho kitaweza kuwaletea tija. Alisema kuwa ni vyema Kwa wataalamu wa kilimo wa jeshi hilo kutoa elimu zaidi Kwa wakulima ili tija iweze kupatikana.   Mabodi aliyesema hayo huko katika Viwanja vya maonesho ya siku chakula Duniani yanaendelea huko  Chamanangwe Wilaya ya Wete wakati akizungumza na waandishi wa habari.   Alieleza kuwa Jku ni jeshi la Kujenga Uchumi hasa kwani limekuwa likifanya vizuri katika sekta ya uzalishaji mali.   "Nina Imani kubwa kuwa huko mbele ya safari Kuna hatari ya katika dhana ya Uchumi wa bluu kukawa naushindani Mkubwa baina ya Jku na KM KM Kwa kiasi Fulani," alieleza Mabodi.   Sambamba na hayo Mabodi alifahamisha dhana nzima ya kuanzishwa Kwa Jku ni kutoa taaluma mbali mbali Kwa Vijana wa kizanzibari ili waweze

ZECO LAWAPA MATUMAINI WANANCHI PEMBA.

                       NA SAID ABRAHMAN PEMBA.   SHIRIKA la Umeme (ZECO) tawi la Pemba limesema kuwa litaendelea kushirikiana na wananchi wa Kisiwa hicho ili kuhakikisha nishati hiyo inaenea vijiji vyote vilivyoko huko.   Hayo yalibainishwa na Ofisa mipango na utafiti wa Shirika hilo Ali Faki Ali wakati alipokuwa akizungumza na Masheha wa Wilaya ya Wete huko katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Wete.   Alieleza kuwa Kwa Sasa Shirika limefanikiwa kupeleka nishati ya umeme katika vijiji vipatavyo 417 kati ya 424  huku Shirika hilo likipeleka nishati hiyo katika Visiwa vyote 8 vilivyomo ndani ya Pemba ikiwa ni pamoja na Njao, Fundo, Kokota, Uvinje,Kojani, Shamiani,Kisiwa panza na Makoongwe.   "Kwa Sasa tuna asilimia 98.3 ya vijiji vyote ambavyo tayari vimeshapata huduma ya umeme huku asilimia 1.7 tu ndivyo ambavyo vimebaki havina umeme, Shirika limo mbioni kuhakikisha navyo vinapata umeme mwaka huu," alieleza Ofisa Ali    Ofisa huyo alivitaja vijiji ambavyo ha

HIZI HAPA CHANGAMOTO WANAZOZIPATA WATU WENYE ULEMAVU.

Image
                          NA FATMA HAMAD PEMBA. 9/10/2022 Licha ya   juhudi   zinazochukuliwa na Serikali pamoja na mashirika mbali mbali yanayoshughulikia   watu wenyeulemavu   ili kuona watu wenye ulemavu wanaondokana na vikwazo kadhaa, lakini bado wanaendelea kukubwa na matatizo   mbali   mbali ikiwemo ukosefu wa huduma. Hayo yamebainishwa na Mama mwenye   ulemavu   wa viungo ambae   pia ana   watoto 3 wenye   ulemavu   mchanganyiko   mkaazi wa   Konde   wilaya   ya   Micheweni   mkoa wa Kaskazini Pemba   alisema bado anakabiliwa   na changamoto ya   upatikanaji pesa   kwa ajili ya   kununulia   huduma za watoto wake hao. Akizungumza na mwandisi   wa habari hizi   huko   nyumbani kwake bi Asha Khamis Juma   mkazi   wa   Konde   kiungani mwenye ulemavu   wa viungo alisema bado anakabiliwa na changamoto   kubwa   ya upatikanaji wa   pesa kwa ajili ya   kununulia   Pempasi pamoja na dawa. ‘’Kila siku natumia elfu ishirini [20000] kwa ajili ya kununulia pempasi hivyo nateseka si

WANANCHI WANAOISHI KATIKA NYUMBA ZA MAENDELEO WAHIMIZWA USAFI

NA SAID ABRAHMAN PEMBA.  SHIRIKA la nyumba Kisiwani Pemba limewataka wananchi wanaoishi katika nyumba za maendeleo zilizopo Mtemani Wete kushirikiana pamoja katika suala Zima la Usafi katika maeneo yao . Hayo yalielezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la nyumba na makaazi Kisiwani Pemba Ali Mgau wakati alipokuwa akizungumza na wakaazi wa nyumba namba 5 huko Mtemani Wete. Alieleza kuwa kuanzia Sasa Shirika limeamua kuwashirika na wananchi wanaoishi katika nyumba hizo katika matengenezo hasa uzibuaji na utapishaji wa Makaro ambayo yameshajaa au kuziba. "Kuanzia Sasa Shirika letu limeamua kuwaachia wananchi wenyewe suala la uzibuaji au utapishaji wa Makaro,Shirika litasaidia pale ambapo litahitajika kufanya hivyo," alieleza Mkurugenzi Mgau. Sambamba na hayo Kaimu huyo aliwataka wakaazi hao ambao mikataba yao imemalizika kufika ofisini kwao ili kujaza mikataba mengine mipya. "Hivi Sasa Tunataka kufanya uhakiki wa wapangaji wetu ambao wanakaa katika majumba haya ya maendeleo,