MTUHUMIWA AOMBA RUHUSA

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

 

Mtuhumiwa wa kesi ya ulawiti Nuhu Kombo Nuhu ameiambia mahakama  ya  mkoa inayoshuhulikia kesi za  udhalilishaji iliyopo mkoa wa Kaskazini Pemba kumpa ruhusa kwenda kutafuta mashahidi ili waweze kuja kutoa ushahidi.

 ‘’Mheshimiwa hakimu mimi nimo ndani nitawapata vipi hao mashahidi naomba niruhusu nitoke nikawatafute’’ alisema mtuhumiwa.

 Hakimu wa mahakama hiyo Ali Abdulrahman Ali alimtaka mtuhumiwa huyo kutaja majina ya mashahidi  waweze kupelekewa barua ya wito ili waweze kufika mahakamani na kutoa ushahidi.

 ‘’Wewe upo rumande hatuwezi kukuruhusu kwenda kutafuta mashahidi kama umeshindwa sema tufunge ushahidi’’ alisema hakimu.

 Hivyo utaendelea kubaki rumande hadi tarehe 24/10/2022 kwa ajili ya kuendelea na hatua ya utetezi.

 Tukio hilo lilitokea tarehe 13/ 12/ 2021 majira ya sa moja asubuhi huko kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wa  Kaskazini Pemba ambapo mtuhumiwa alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili.

Ilidaiwa kuwa kufanya hivyo ni kosa  kinyume na kifungu cha 116[1] cha sheria nambari 6/2018 sheria  ya Zanzibar.

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.