Posts

Showing posts from July, 2023

WANDISHI WA HABARI PEMBA WAPIGWA MSASA

Image
                      NA FATMA HAMAD Wandishi wa habari wametakiwa   kuielimisha jamii kufahamu      masuala ya Afya ya uzazi, ili kufahamu afya zao, na kuweza   kupata tiba   sahihi, jambo ambalo litasaidia kupunguza   vifo vya mama na mtoto. Ushauri huo umetolewa na afisa mradi wa afya ya uzazi, wakati akielezea kuhusu mradi huo wa uzazi salama   Zaina Abdala Mzee kwenye   mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo wandishi wa habari, kuandika habari zinazo husu masuala ya afya ya uzazi,   yaliofanyika katika ukumbi wa Tamwa Chake Chake Pemba. Alisema kwa mujibu wa tafiti kutoka wizara ya afya,   vifo vya mama na mtoto   bado ni changamoto inayoikumba Jamii. Alisema wandishi wa habari wana nafasi kubwa katika jamii, hivyo ni vyema kuwandika habari pamoja na makala ambazo zitaisaidia jamii kufahamu masuala ya   afya ya uzazi ili waweze kufika vituo vya afya kufanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu. ‘’Nyinyi waandishi wa habari mnaaminika zaidi katika jamii, hivyo ni vyema mkay

KOSA LA KUNAJISI MWENYE ULEMAVU LAMSABABISHIA KUSOTA RUMANDE

                           Na Fatma Hamad Pemba. Mahakama   ya mkoa A wete imeighairisha kesi ya kunajisi mtoto mwenye ulemavu wa akili inayomkabili kijana Khamis Salim Ali   mwenye umri wa miaka 27 mkaazi wa Selemu   wilaya ya wete mkoa wa Kaskazini Pemba. Imedaiwa   mahakamani   hapo   siku ya   tarehe   5/2/2023   majira ya   skumi   za   jioni huko Selemu Wete ulimuingialia mtoto wa Kiume    mwenye   umri   wa   miaka   12 ambae ni mwenye ulemavu wa akili   jambo ambalo ni kosa kisheria. Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Mussa Omar amesema kuwa kesi hiyo ilikua katika hatua ya utetezi lakini hatutoendelea kwani hakimu anaesikiliza kesi hiyo   hayupo. Hakimu wa mahakama ya mkoa A Said Hemed   amesema    hakimu anaendesha kesi za udhalilishaji hayupo mahakamani amepata dharura ya kikazi nje ya Pemba kesi hiyo itarudi tena mahakamani hapo   tarehe 12/7/ 2023 na kuendelea na utetezi. ‘’Naighairisha kesi hiyo hadi tarehe 12/ 7/ 2023

AACHIWA HURU BAADA YA KUDAIWA KUMUINGILIA KINYUME NA MAUMBILE MKE WAKE WA NDOA

  NA FATMA HAMAD, PEMBA MTUHUMIWA aliekuwa akidaiwa kumuigilia kinyume na maumbile   mke wake, ameishangaza Mahkama maalum ya kupambana na udhalilishaji ya mkoa kaskazini Pemba, kwa kudai kupatiwa ulinzi baada ya kuachiliwa huru mahakamani hapo .   Baada ya kuachiwa huru mtuhumiwa   huyo Mahakamani hapo aliomba Mahakama impatie ulinzi ili apelekwe nyumbani kwao kutokana na hofu aliokua nayo kitu ambacho mahakama ilikataa kufanya hivyo. Mtuhumiwa   huyo Haji Hamad Juma miaka 28, mkaazi wa Majenzi, wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba aliishukuru mahakama hiyo   kwa kutenda haki kwani hajafanya kosa hilo bali alisingiziwa tu na mke wake kwa vile walikuwa hawana maelewano sikunyingi na huku akimdai talaka. ‘’Naishukuru mahakama kwa kuliona hilo, kwani sijamfanyia mimi mke wangu kitendo hicho, ila   naamini alinibambikizia tu kesi kwa vile si kutaka kumpa talaka kama alivyokua akinidai kwa muda mrefu,’’ alieleza mtuhumiwa. Awali Hakimu wa mahakama hiyo   Ali Abdul Rahman Al

JAMII YAPEWA ONYO

Image
                                 NA FATMA HAMAD PEMBA Jamii imehimizwa kuendelea kuziripoti katika vyombo vya sharia   kesi za udhalilishaji, na sio   kuzikalia kitako na kuzifanyia suluhu kifemilia. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji iliyopo Wete mkoa wa Kaskazini Pemba, Ali   Abdul Rahman Ali amesema Serilaki imefanya jitihada mbali mbali ikiwemo kuanzisha mahakama maalum ili kuondosha tatizo hilo Nchini. Alisema licha ya elimu inayoendelea kutolewa kila siku kwa wanajamii,   ili kufahamu madhara ya udhalilishaji, lakini bado jamii imegubikwa na wimbi la rushwa muhali   na   badalayake kuzifumbia macho na kuzifanyia suluhu wenyewe kwa wenyewe, hali ambayo inapelekea kuongezeka kwa udhalilishaji. ‘’Ndugu wanajamii, tusipokuwa makini na tukiendelea kumuonea huruma mdhalilishaji, bado tutaendelea kuutilia mbolea udhalilishajikatika jamii zetu,’’ alieleza hakimu. Hakimu huyo aliendelea kufahamisha kuwa zipo baadhi ya

WAKULIMA WA VIUNGO PEMBA WAIPA TANO MRADI WA VIUNGO.

Image
                                            NA FATMA HAMAD PEMBA. Wakulima wa  mazao  ya  Viungo    kisiwani Pemba  wameushukuru  mradi  wa  viungo  ambao  unatekelezwa  kwa  mashirikiano  ya  Tamwa Zanzibe, PDF, na CFP kwa ufadhili wa  umoja  wa Ulaya kwani  umeweza  kubadilisha  maisha  yao  na kupiga hatua  kimaendeleo. Wakizungumza  na wandishi wa vyombo mbali mbali vya habari  kwa  nyakati  tofauti  katika ziara maalumu  iyondaliwa na Chama cha wandishi wa habari Wanawake Tanzania oisi ya Pemba wamesema mradi wa iungo umekua ni mkombozi kwao. Asha ali Omar mkulima wa Mdalasini na vanila  kutoka Gando wilaya ya Wete  alisema  kabla ya kuja kwa mradi wa viungo  alikua  amepanda mashina 5 tu ya mdalasini, na akipanda pembeni mwa  Nyumba  yake kwani alikua hana ujuzi wa kilimo hicho. ‘’Baada  ya kuja kwa mradi wa viungo na kutupatia elimu sasa hivi nina miliki Hekari moja  ya Midalasini  na Mivanila 120  yangu  peke yangu alisema mkulima bi Asha. Alisema kilimo hicho kimekua k

ALIEMNAJISI MTOTO MWENYE ULEMAVU WA AKILI AENDELEA KUSOTA RUMANDE

                           Na Fatma Hamad Pemba. Mahakama   ya mkoa A wete imeighairisha kesi ya kunajisi mtoto mwenye ulemavu wa akili inayomkabili kijana Khamis Salim Ali   mwenye umri wa miaka 27 mkaazi wa Selemu   wilaya ya wete mkoa wa Kaskazini Pemba. Imedaiwa   mahakamani   hapo   siku ya   tarehe   5/2/2023   majira ya   skumi   za   jioni huko Selemu Wete ulimuingialia mtoto wa Kiume    mwenye   umri   wa   miaka   12 ambae ni mwenye ulemavu wa akili   jambo ambalo ni kosa kisheria. Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Mussa Omar amesema kuwa kesi hiyo ilikua katika hatua ya utetezi lakini hatutoendelea kwani hakimu anaesikiliza kesi hiyo   hayupo. Hakimu wa mahakama ya mkoa A Said Hemed   amesema    hakimu anaendesha kesi za udhalilishaji hayupo mahakamani amepata dharura ya kikazi nje ya Pemba kesi hiyo itarudi tena mahakamani hapo   tarehe 12/7/ 2023 na kuendelea na utetezi. ‘’Naighairisha kesi hiyo hadi tarehe 12/ 7/ 2023