AACHIWA HURU BAADA YA KUDAIWA KUMUINGILIA KINYUME NA MAUMBILE MKE WAKE WA NDOA

 

NA FATMA HAMAD, PEMBA
MTUHUMIWA aliekuwa akidaiwa kumuigilia kinyume na maumbile  mke wake, ameishangaza Mahkama maalum ya kupambana na udhalilishaji ya mkoa kaskazini Pemba, kwa kudai kupatiwa ulinzi baada ya kuachiliwa huru mahakamani hapo
.

 Baada ya kuachiwa huru mtuhumiwa  huyo Mahakamani hapo aliomba Mahakama impatie ulinzi ili apelekwe nyumbani kwao kutokana na hofu aliokua nayo kitu ambacho mahakama ilikataa kufanya hivyo.

Mtuhumiwa  huyo Haji Hamad Juma miaka 28, mkaazi wa Majenzi, wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba aliishukuru mahakama hiyo  kwa kutenda haki kwani hajafanya kosa hilo bali alisingiziwa tu na mke wake kwa vile walikuwa hawana maelewano sikunyingi na huku akimdai talaka.

‘’Naishukuru mahakama kwa kuliona hilo, kwani sijamfanyia mimi mke wangu kitendo hicho, ila  naamini alinibambikizia tu kesi kwa vile si kutaka kumpa talaka kama alivyokua akinidai kwa muda mrefu,’’ alieleza mtuhumiwa.

Awali Hakimu wa mahakama hiyo  Ali Abdul Rahman Ali alisema mtuhumiwa huyo amelazimika kumuachia huru, kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo kutomunganisha na kesi husika.

 ‘’Baada ya utetezi huo alioutoa yeye  mshitakiwa kuwa sikunyingi mke wake akimdai talaka na hakutaka kumpa, Mahakama imejiridhisha na kuona  kwamba  hiyo ni kesi tu ya kusingiziwa na mke wake,’’ alisema hakimu huyo.

Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Mussa Omar aliambia Mahakama hiyo kuwa hakuridhishwa na uwamuzi huo na kuweka indhari ya kukata rufaa.

‘’Mheshimiwa  hakimu  kwa uwamuzi uliofikiwa mahakamani hapa Ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka haikuridhika na itakata rufaa juu ya shauri hilo,’’ alieleza.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa huyo alimuingilia kinyume na maumbile mke wake wa ndoa, tokeo lililotokea machi 2 mwaka huu ambapo kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 113 [a] sheria ya adhabu sheria namba 6/ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.