JAJI MKUU ZANZIBAR ATAKA WANAFUNZI WA VYUO VYA MAFUNZO KUPATIWA ELIMU YA USHAURI NASAHA
NA FATMA HAMAD, PEMBA Mahikimu wa mahakama za kadhi, Makamanda wa Vyuo vya mafunzo kisiwani Pemba wametakiwa kushirikia na Idara ya Msaada wa kisheria kuwapa elimu ya ushauri nasaha wanafunzi wa Vyuo vya mafunzo ili waweze kubadilika na kuwa na tabia njema. Agizo hilo limetolewa na Jaji mkuu wa Zanzibar Ramadhan Khamis Abdala wakati akizungumza na wanafunzi pamoja na Makamanda wa Vyuo vya mafunzo kisiwani Pemba. Alisema wengi wanaofikwa na mtihani wa kwenda kwenye vyuo vya mafunzo wanahisi kama wameonewa, hivyo ni vyema kuanzishwa utaratibu wa kupewa ushauri nasaha ili waweze kuondokana na mawazo hayo,na kuona watakaporudi katika familia zao wamebadilika tabia na kuwa Raia wema. ‘’Wenzetu hawa wanapokuja humu vyuoni huwa wanathirika kisaikologia, na kuhisi Serikali imewaonea hivyo ni budi kuwapa Mawaidha pamoja na ushauri nasaha ili ziweze kurudi akili zao, alisema. Aidha alisema ni vyema kupatiwa misada midogo mi