Posts

Showing posts from December, 2021

MELI KUBWA LA WATALII KUTOKA UFARANSA LATUA KISIWANI PEMBA.

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. JUMLA ya watalii 69 wamewasili kisiwani Pemba kwa meli maalumu, kwa lengo la kujionea vivutio mbali mbali vya utalii vilivyomo Kisiwani humo. Watalii hao raia wa Ufaransa wamewasili Kisiwani Pemba kwa ziara ya siku Moja, kwa kutumia Usafiri wa meli aina ya LE BELLOT, wameweza kutembelea na kujionea vivutio vya utalii. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwapokea watalii hao, kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema ujio wa watalii hao ni kukitangaza kisiwa cha Pemba kiutalii kupitia vivutio mbali mbali vilivyomo. Alisema ujio wao utaweza kuwanufaisha wafanya biashara na wajasiriamali, kuuza na kutangaza bidhaa na biashara zao kimataifa. “Kwa sasa ni wazi kuwa Kisiwa cha Pemba kimeanza kufunguka kiutalii, ujio wao utaweza kuonyesha dunia kuwa Pemba kuna vivutio vingi vya Kiutalii, Pemba ni sehemu salama ya watalii kutembea”alisema. Aidha Mkuu huyo alisema ni meli ya pili hiyo

ATIWA MBARONI AKIDAIWA KUMLAWITI MLEMAVU WA AKILI

Image
Msifunzwa ni mamae hufunzwa ni ulimwengu   hii imekuja baada ya Nuhu Kombo Nuhu mwenye mumri wa miaka 22   akihemea polisi kwa tuhuma za kumlawiti kijana   wa 18 mwenye ulemavu wa akili na mdomo. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mama mzazi wa kijana huyo amesema ailikua yupo nae nyumbani badae akatoka   na hakurudi tena   na alianza kumtafuta ila hakumuona. Alisema kuwa baada ya muda     mrefu kupita   aliletewa     nyumbani   na msamaria mwema na kumuambia huyu mtoto wako nimemkuta   Vichakani akiwa anafanyiwa udhalilishaji na Nuhu Kombo Nuhu. Alifahamisha   kuwa   baada ya hapo aliendelea kumuhoji na kumuambia kuwa hii ni kawaida yake kumchukua na kumpeleka vichakani   kumfanyia kitendo hicho ‘’Nilipo muhoji aliniambia ashazoea kunifanyia hivi   na ananiambia atanipa pesa na simu ya tachi’’ alieleza mama mzazi. Aidha mama huyo alisema kuwa baadhi ya wanafamili wa mtuhumiwa huyo wamekua   wakimtolea maneno mabaya huku wakimtaka   wafanye suluhu ili kesi isiendelee.

JAMII YAHIMIZWA KUWATUNZA NA KUWATHAMINI WATU WENYE ULEMAVU.

Image
  kikundi   Cha Mazoezi   ya viungo cha Gombani Fitnes Senter   kilichopo chake chake   kimemtembelea    na kumfariji kijana Asaa Khamis mwenye ulemavu   wa Viungo Mkaazi wa Shumba ya Vyamboni   wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba   kufuatia    habari iliyorushwa katika Blog ya Pemba ya leo     iliyo muhusu kijana huyo   akihitaji msaada   wa kupatiwa mtaji   kwa   ajili ya kuendeleza biashara zake. Akizungumza mara bada ya kumfariji kijana huyo   katibu wa Kikundi   hicho   Khalfan Amour   Mohd alisema mbali ya kukindi hicho kufanya mazoezi   pia kimekua kikifanya harakati mbali mbali za kijamii kama vile kusaidia watu wenye ulemavu, pamoja na kupiga vita masuala ya udhalilishaji hususan kwa walemavu . ‘’Unajua sisi tumeguswa na makala iliyorushwa kwenye mtandao inayomzungumzia Kijana Asaa jinsi anavyopata shida kutokana na ulemavu wake tukaona ipo haja kumfariji kwa vile na sisi ni walemavu watarajiwa’’alisema Khalfani. Alisema watu wenye ulemavu wanakumbana na changamo

WALIMU MASKULINI WAHIMIZWA KUJIONGEZA KIELIMU

Image
Afisa Elimu Wilaya chake chake Burhani Khamis Juma kwa niaba ya Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba amewataka  Walimu  wa skuli mbali mbali kisiwani Pemba  kuitumia  teknolojia   ya  mitandao  ya kijamii  ili waweze  kujifunza na kuwafundisha wanawafuzi  katika  kuleta  mabadiliko  katika sekta ya  Elimu. Afisa Elimu Wilaya chake chake Burhani Khamis Juma kwa niaba ya Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Afisa huyo Ameyasema  hayo  katika  hafla  ya  kukabidhi  vyeti  kwa  walimu  waliohitimu  mafunzo  ya  Elimu  Mtandao  na Masafa  kutoka  taasisi  ya  [SHAIBU  FOUNDATION ] Chake Chake  Pemba . Amesema  kupitia  mafunzo  hayo  ya  elimu  mtandao yatatoa fursa kwa walimu kuwajengea uwezo wa kuitumia mitandao katika  kutafuta  notis  za masomo mbalimbali  kwa ajili  ya kuwafundishia  wanafunzi wao. ‘’Huu ni wakati wa utandawazi  walimu musitumie vitabu tu katika kuwafundishia ni lazima muitumie mitandao ili muweze  kupata vitu vyengine’’ a

WADAU MBALI MBALI WASHAURIWA KUSHIRIKIANA KWA PAMOJA ILI KUMALIZA UDHALILISHAJI.

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mheshimiwa Matar Zahor Massoud amesema Kuna ulazima wa kila mdau kushiriki kwa pamoja katika kusimamia Sheria na kanuni za kesi za udhalilishaji Ili  kuiokoa Jamii kuondokana na majanga ya ukatili na udhalilishaji nchini Akizungumza kwa niaba ya Mkuu huyo wa Mkoa , Mkuu wa Wilaya ya Wete Dr Hamad Omar Bakar huko uwanja wa Mshaame Mata Micheweni katika maadhimisho ya siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jumuiya inayopingana na ukatili na udhalilishaji wa kijinsia TUJIPE amesema udhalilishaji umekuwa kikwazo Cha kuleta maendeleo kwa wanawake na watoto hivyo Ili kuisaidia juhudi za Taifa katika kutokomeza janga Hilo ni budi kwa kila mmoja kuendelea kusimamia jukumu alilopangiwa Mapema mratibu wa jumuiya  inayopingana na ukatili na udhalili Shaji wa kijinsia ya Tumaini Jipya  (TUJIPE) Tatu Abdallah Mselem amesema licha kuwepo kwa Sheria na hukumu zinazotokewa katika watendaji wa matendo hayo Bado udhalilishaji unaende

MUHALI BADO NI TATIZO KATIKA KESI ZA UDHALILISHAJI

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Ushiriki mdogo wa wanajamii dhidi ya utoaji wa ushahidi mahakamani bado  ni changamoto kubwa inayopelekea  kesi za udhalilishaji  kushindwa kupata hatia jambo ambalo linachangia  kuongezeka  kwa vitendo hivyo. Akizungumza kwa dharura ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya mkoani Khatib Juma Mjaja amesema ni muhimu kwa vilabu vya mazoezi kushirikiana na wanaharakati mbali mbali kuielimisha jamii kujua madhara ya rushwa muhali kwani ni adui katika mapambano hayo. Aidha ameahidi ushikiano sambamba na kuomba umoja huo kuandaa mbinu madhubuti ya kuibua na kuyaripoti matendo hayo ili kuhakikisha wafanyaji wa matukio hayo wanapatikana na kufikishwa katika vyombo vya sheria. ‘’Sasa ni wakati wa kutekeleza kwa vitendo, hivyo ni jukumu la kila mmoja kusimama kwa nafasi yake kuunga mkono juhudi za kupinga  tatizo hili ambalo limekua ni kilio  kwa wakaazi wa Zazibar’’ alisema mkuu wa wilaya. Awali akisoma risala mjumbe kutoka umoja wa vilabu vya mazoezi ya viungo  Pemba S

WAZAZI WAOMBWA KULEA WATOTO WAO KATIKA MALEZI YA PAMOJA

Image
Wazazi   wametakiwa kurejesha malezi ya pamoja katika kuwalea watoto wao jambo ambalo litasaidia kupatikana kwa kizazi chenye madili bora.   Hayo yamesemwa na kaimu mratibu wa kituo cha huduma za sheria   Safia Saleh Sultan wakati akizungumza na wanakikundi cha chapa kazi cha wanakisomo kilichopo   Kwale Gombani Chake chake Pemba. Alisema kukosekana kwa kizazi chenye madili ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia, hivyo wakati umefika kwa wazazi kushirikiana kwa pamoja ili kupunguza tatizo hilo hapa nchini.   Akiwasilisha mada katika mkutano huo Khadija kutoka kituo cha huduma za sheria   amewataka wazazi   fuatilia nyenendo za   watoto wao wakati wanapokwenda skuli na madrasa ili kuwalinda na vitendo viovu vikiwemo vya udhalilishaji. Samba mba na hilo amesema endapo jamii itatoa huduma stahiki kwa family zao inaweza ikasaidia watoto kujiepusha kujitumbwikiza katika vigenge viovu ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa wimbi la udhalili

UMOJA WA VILABU UNAWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KATIKA MADHIMISHO YA SIKU 16 YA KUPINGA UDHALILISHAJI

Image
  Katika kuelekea maadhimisho ya    siku   16   ya   kupinga udhalilishaji wa kijinsia Zanzubar Umoja wa vilabu vya mazoezi    kisiwani Pemba umedhamiria kufanya bonanza malum la kuadhimisha siku hiyo jumamosi ya   tarehe 11 mwezi   huu huko katika Uwanja wa michezo Gombani Chake chake. Akizungumza na wandishi wa habari katika ofisi za Tamwa Mkanjuni Chake chake katibu wa jumuia ya umoja wa vilabu vya mazoezi kisiwani Pemba Khalfan Amour Mohd alisema   umoja huo umeamua kuadhimisha siku hiyo ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto ambao umekua ukiwakumba mara kwa mara katika jamii. Alisema kumekuwepo na vitendo vingi vya ukatili wa kijinsia ambavyo huakumba zaid Wanawake na watoto, hivyo wameona ipo haja nawao kuchukua jitihada za makusudi   za kuzipigia kelele zile kero ambazo zinawakumba wanawake na watoto katika jamii na kuzifikisha katika mamlaka husika ili kuona haki inatendeka. ‘’Tumeona kwa vitendo vya udhalilishaji vinaf

JAMII YATAKIWA KUSIMAMA KIDETE KUKOMESHA UDHALILISHA WA KIJINSIA

Image
Afisa Mdhamini Ofisi ya Raisi tawala za mikoa Serikali za mitaa   na idara maalumu SMZ Thabiti Othmani Abdalla ameitaka Jamii kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya matendo ya udhalilishaji yanayoendelea kujitokeza siku hadi siku hapa nchini. Ushauri huo ameutoa wakati akizungumza na wanafunzi wa Vyuo mbali mbali Kisiwani Pemba huko katika kituo cha huduma za Sheria ikiwa ni shamra shamra za kuelekea katika maadhimisho ya siku 16 ya kupinga matendo ya udhalilishaji. Amesema Kila mtu anapaswa kuunga mkono juhudi za serikali katika kupinga matendo ya udhalilishaji. Amesema wakati umefika kwa jamii kuacha muhali na kusimama mahakamani kutoa ushahidi katika kesi hizo ili kuona zinafikia hatua inayostahiki . Kwa upande wake Mratib wa Kituo cha Huduma za Sheria Pemba,Safia Seleh Sultan amewaomba wanafunzi hao kuzisoma sheria ambazo zitaweza kuwasadia na kuwalinda katika mapambano dhidi ya   Vitendo vya   udhalilishaji. Nao washiriki wa mkutano huo wameitaka Serikali kuwachukuli

UTELEKEZAJI BADO NI TATIZO KWA WANAWAKE NA WATOTO

Image
Utelekezwaji wa wanawake na watoto ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa matendo ya udhalilishaji katika Jamii. Akizungumza na wandishi wa habari huko ofisini kwake mratibu wa   jumuia ya Tumaini Jipya [TUJIPE] Tatu Abdala Mselem    amesema imebainika kuwa watoto   wengi wanaotelekezwa na wazazi wao hujiingiza katika   masuala ya omba omba na kupelekea kufanyiwa udhalilishaji. Aidha alifahamisha kuwa akina baba wengi wanapoachana na wenzao wao hawatowi matunzo ipasavyo kwa watoto wao na kupelekea   kukosa   haki   zao   za   msingi. ‘’Wazazi wanapoachana watoto huathirika zaid kwani huwa ni sababu ya wao kutelekezwa na kukosa matunzo’’ alisema Bi tatu. Kwa upande wake mjumbe wa kamati tendaji kutoka tumaini jipya Ali Yussuf Ali alisema ipo haja kwa viongozi wa dini kuielimisha jamii kuwa na uvumilivu ili   kuepukana na talaka za kiholela jambo ambalo litasaidia kupunguza vitendo hivyo. Mapema makamo mwenyekiti wa tumaini jipya Suleimana Mohd Iddi alisema licha vitendo h

WAZAZI WATAKIWA KUTOA MATUNZO STAHIKI KWA FAMILIA ZAO

Image
Wazazi na walezi wamehimzwa kuendelea kutoa huduma stahiki kwa watoto wao jambo ambalo litaepusha kufanyiwa kwa  udhalilishaji wa kijinsia  kwa watoto. Ushauri huo umetolewa na Siti Habibu Mohd kutoka kituo cha huduma za Sheria ofisi ya Pemba wakati akitoa elimu juu ya kuripoti matendo ya udhalilishaji  kwa wanafunzi wa Skuli ya Madungu Msingi alisema bado suala la udhalilishaji linaendelea kufanyika kila siku , hivyo ni vyema wazazi kuwa na ukaribu wa hali ya juu pamoja na kuwapatia huduma  ili kuwalinda na vitendo hivyo. ‘’Nawasihi wazazi wenzangu tujitahidi kuwahudumia watoto wetu ili tuwalinde na vitendo viovu’’ alisema Bi siti. Sambamba na hilo aliwataka wanajamii kushirikiana na vyombo vya kisheria kwa kuwafichua watendaji wa makosa hayo pamoja na kutoa ushahidi mahakamani jambo ambalo litapunguza matendo hayo. Aidha aliwataka wanafunzi hao kutoa tarifa kwa watu wao wa karibu   ikiwa ni pamoja na wazazi, walimu wao, wakati wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji   ili kujinusuru