WALIMU MASKULINI WAHIMIZWA KUJIONGEZA KIELIMU

Afisa Elimu Wilaya chake chake Burhani Khamis Juma kwa niaba ya Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba amewataka  Walimu  wa skuli mbali mbali kisiwani Pemba  kuitumia  teknolojia   ya  mitandao  ya kijamii  ili waweze  kujifunza na kuwafundisha wanawafuzi  katika  kuleta  mabadiliko  katika sekta ya  Elimu. Afisa Elimu Wilaya chake chake Burhani Khamis Juma kwa niaba ya Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba

Afisa huyo Ameyasema  hayo  katika  hafla  ya  kukabidhi  vyeti  kwa  walimu  waliohitimu  mafunzo  ya  Elimu  Mtandao  na Masafa  kutoka  taasisi  ya  [SHAIBU  FOUNDATION ] Chake Chake  Pemba .

Amesema  kupitia  mafunzo  hayo  ya  elimu  mtandao yatatoa fursa kwa walimu kuwajengea uwezo wa kuitumia mitandao katika  kutafuta  notis  za masomo mbalimbali  kwa ajili  ya kuwafundishia  wanafunzi wao.

‘’Huu ni wakati wa utandawazi  walimu musitumie vitabu tu katika kuwafundishia ni lazima muitumie mitandao ili muweze  kupata vitu vyengine’’ alisema mgeni rasmi.

Sambamba na hilo amewaasa walimu kuitumia mitandao ya kijamii kwa lengo la kujifunza vitu ambavyo vitaleta manufaa jambo ambalo litasaidia kuleta ufaulu mzuri kwa wanafunzi katika masomo yao.

Akisoma risala katika hafla hiyo Rais wa taasisi ya Shaib Foundation Mustafa Said Moyo amesema  kuwa licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika mafunzo hayo lakini   kumekuwa na changamoto  ambazo zimejitokeza ikiwemo miundombinu isiyo rafiki

Aidha Akitaja lengo la kutolewa kwa mafunzi hayo  amesema  kwa mujimu wa takwimu na tafiti mbali mbali inaonesha  kuwa utumiaji wa mitandao umekua, huku ikionekana matumizi makubwa yamekua yakitumika vibaya kama vile kuangalia picha za ngono na michezo ya kamari ambapo mafunzo ya kitaluma yalikua chini.

Nao baadhi ya walimu waliopata fursa ya kushiriki katika mafunzo hayo wameeleza namna mafunzo hayo yalivowabadilisha kutoka hatua moja hadi kufikia hatua nyengine hasa katika kujifunza jinsi ya kutafuta  notis kwa njia ya mtandao huku wakitoa shukrani nzao kwa taasisis ya sahib foundation iliona umuhimu wa kuapatia mafunzo hayo.

Hafla hiyo imemalizika kwa kutunukiwa vyeti walimu ambao wameshiriki katika mafunzo hayo  ambapo  walijifunza mambo mbalimbali kupitia Tehama ikiwemo kusoma kumputer, historia ya kumputer, vizazi vya computer, mifumo  ya kitaluma  na usalama wa mta


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.