Posts

Showing posts from November, 2021

WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA WAPEWA MBINU JUU YA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA.

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wasaidizi wa sheria wamehimizwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili kuona wanakuwa na uthubutu wa kwenda mahakamani kutoa ushahidi pamoja na kuripoti vituo vya Polisi wakati  kesi zitakapotokezea. Hayo yamesemwa na Kamanda wa polisi mkoa wa Kusini Pemba Richad Mchovu wakati akifungua kongamano la kutimia kwa miaka 10 yautoaji wa huduma  wa msaada wa kisheria [Lsf]huko Skuli ya Michakaini Chake chake Pemba. Amesema wasaidizi wa sheria wamekua wakifanya kazi kubwa ya kuibua na kuyaripoti matendo ya udhalilishaji lakini bado jamii inaonekana imegubikwa na tatizo la rushwa muhali. Hivyo amewataka wasaidizi wa sheria kuongeza jitihada ya kuwailimisha wanajamii madhara ya rushwa muhali pamoja na kuwajengea uwezo wa kusimama mahakamani jambo ambalo lisaidia kuondokana na udhalilishaji wa Wanawake na watoto. Kamanda huyo ameahidi kutoa mashirikiano ya hali ya juu kwa wasaidizi wa sheria pamoja na ulinzi shirikishi katika mapambano dhidi ya udhalilishaji ili ku

MUHALI BADO NI TATIZO KWA JAMII

Image
Wananchi wametakiwa kushirikiana na vyonbo vya kisheria kutoa tarifa wakati  yanapotokezea matendo ya uhalifu   katika jamii ili kuona watendaji wa makosa hayo   waweze kupatikana na kutiwa hatiani. Hayo yamesemwa na mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya kuzuia Rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar Zaeca Ahmed Khamis Makarani wakati akifungua mafunzo  ya  siku moja kwa wandishi wa habari juu ya mapambano dhidi  ya Rushwa yaliofanyika Gombani Chake chake Pemba amesema bado jamii inaonekana ikiyafumbia macho matendo  ya kihalifu wakati yanapotokezea katika jami zao. Amesema kuwepo kwa rushwa katika jamii ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa matendo maovu ikiwemo Rushwa, Udhalilishaji pamoja na ujambazi, hivyo  basi ni wakati umefika kwa jamii kuacha muhali  na kutoa tarifa kwa mamlaka husika jambo ambalo litasaidia kuondokana na vitendo  hivyo. Alifahamisha kuwa kuwepo kwa muhali hakuna  maendeleo yanayopatikana bali hupelekea wanyonge kuonewa na kukosa haki zao. Akiwasilisha mada juu ya na

UGONJWA WA KOVID 19 BADO NI TATIZO KWA WATU WENYE ULEMAVU

Image
  NA FATMA HAMAD FAKI. Watu wenye ulemavu wamehimizwa kuendelea kuchukua tahadhari juu ya kujikinga na ugonjwa wa Uviko 19 katika Jamii zao. Wito huo umetolewa na mjumbe wa kamati tendaji wa jumuia ya watu wenye ulemavu [ZAPDD] Mkubwa Ahmed Omar wakati akifungua mafunzo ya siku moja juu ya kujikinga na ugonjwa kovid kwa watu wenye ulemavu huko Gombani Chake chake Pemba Alisema watu wenye ulemavu ni moja ya kundi lililotajwa kuwa hatarini zaid kupata ugonjwa huo. Alisema ipo haja kwa watu hao kuchukua jitihada ya hali ya juu ikiwemo kuosha mikono mara kwa mara, Kuchoma chanjo   pamoja na kuvaa barakoa wakati wanapokwenda katika mikusanyiko ya watu jambo ambalo litaepusha kuenea kwa ugonjwa huo. ‘’Nawaomba jamani tujitahidi sana kuchukua tahadhari kwani ugonjwa bado upoo’’aliwasihi mjumbe. Akiwasilisha mada Afisa kutoka jumuia ya watu wenye ulemavu Zanzibar [ZAPDD] Khalid Abdala Omar alifahamisha kuwa kwa mujibu wa tafiti ya mwaka 2018 jumla ya watu wanaoishi na ulemavu wa aina

SERIKALI YATAKIWA KUJENGA VINDA ABAVYO VITATOA AJIRA KWA VIJANA

  NA SAID ABRAHMAN PEMBA.   JAMII imeiomba Serikali kujenga viwanda vya kusindikia samaki ili kwenda sambamba na dhana ya uchumi wa bluu.   Wakijadili mada juu ya uchumi wa bluu katika kikao kilichoandaliwa na taasisi ya Action aid, huko Kojani Mkoa wa Kaskazini Pemba, wananchi wa Kisiwa hicho walisema kuwa ni vyema kwa Serikali kuanzisha viwanda hivyo ili waweze kunufaika na mazao yanayotokana na bahari na kufikia azma ya uchumi wa bluu.   Walieleza kuwa wananchi wananchi walio wengi hawajawa na uelewa sahihi juu ya dhana ya uchumi wa bluu, hivyo ni vyema kwa Wizara husika kutoa taaluma kwa wananchi ili waweze kuelewa maana yake.   Hamad Juma mjumbe wa Kikundi Cha Mduara alisema kuwa ili Serikali iweze kukuza uchumi wa bluu na kukuza hali za maisha ya wananchi lazima iweze kujenga viwanda vya kusindikia samaki ili iweze kwenda sambamba na azma yenyewe ya Uchumi wa bluu.   Alieleza kuwa endapo Serikali itaweza kujenga viwanda hivyo wananchi wengi wataweza kunufaika ikiwa ni p

WANANCHI WATAKIWA KUIDUMISHANI AMANI

Image
  Wananchi wametakiwa kuendelea kuutunza Umoja   na mshikamano uliopo   sasa ili   kuona Amani imetawala na nchi inapinga hatua katika nyanja mbali mbali za   kimaendeleo. Akizungumza na watendaji wa azaki za kiraia Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud wakati akifungua kongamono la kumpongeza Rais mwinyi kwa kipindi cha mwaka mmoja alichokaa madarakani lililofanyika ukumbi wa baraza mji Chake chake Pemba. Alisema suala la kutunza Umoja ni jukumu la kila mtu, hivyo ni vyema kila mmoja kwa nafasi yake kuendeleza umoja huo ili kuona hakuna vitendo vyovyote viovu vinavyojitokeza. ‘’Nawasihi wananchi tuutunzeni umoja wetu na mshikamano wetu ili tuweze kufanya kazi zetu kwa uhuru’’ alisema Mattar. Alisema bila ya kuepo kwa amani si rahisi kupatikana kwa maendeleo, hivyo   aliitaka Jamii kujiepusha kufanya vitendo viovu ambavyo vinaashiria uvunjifu wa amani. Alisema Rais Mwinyi kwa kuwajali Wananchi wake   ndio akamua kuunda umoja wa kitaifa ili kuwaunganisha Wazanzibar

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KATIKA VIYUO VYA AFYA KUCHOMA CHANJO YA UV19

  NA FATMA HAMAD FAKI. Wananchi wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya afya kuchoma chanjo ya uviko 19   ili waweze kujikinga na ugonjwa huo. Wito huo umetolewa na mratibu wa chanjo Kisiwani Pemba Bakar Hamad Bakati wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika zoezi la uchanjaji wa chazo hizo, kwa wananchi wa shehia ya Sizini wilaya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema kinga ni bora kuliko tiba, hivyo ni vyema kila mmoja kuhakikisha amechoma chanjo ya uviko 19 jambo ambalo litaepusha kuenea kwa ugongwa huo katika jamii. Alisema chanjo hiyo itaendelea kutolewa katika kituo cha Afya cha sizini, hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi kituoni hapo na kupatiwa chanjo. ‘’Tumeamua kuleta chanjo katika kituo hicho jambo ambalo liwarahisishia wananchi kufuata masafa ya mbali huduma hiyo’’ Alisema mratibu Bakari. Aidha amefahamisha kuwa wanaostahiki kupata chanjo hiyo ni watu wa zima kuanzia   umri wa miaka   18,wakiwemo na wajawazito. Baadhi ya wananchi hao w

KIJANA ASSA MWENYE ULEMAVU WA VIUNGO AOMBA MSAADA APATIWE MTAJI

Image
  NA FATMA  HAMAD, PEMBA. KIJANA Assaa Khamis Hamad mwenye umri wa miaka 35 mkaazi wa Shumba Vyamboni wilaya ya Micheweni Pemba ameomba Serikali pamoja na wahisani wamsaidie mtaji ili aendeleze biashara zake ambazo humpatia kipato cha kuhudumia familia yake. Kijana huyo mwenye ulemavu wa viungo anafanya biashara ndogo ndogo ikiwa ni pamoja na  njugu nyasa na Vocha kwa lengo la kujipatia kipato kitakacho msaidia na familia yake.   Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye machimbo ya mchanga huko Shumba Vyamboni Assaa alisema, hawezi kufanya kazi ngumu kutokana na hali yake kwani  ulemavu alionao ni wa miguu na mikono. Alisema kuwa, kwa sasa hafanyi biashara hizo kutokana na kukosa fedha za kununulia vocha pamoja na njugu, jambo ambalo anashindwa kuihudumia familia yake. “Naiomba Serikali, wahisani na taasisi zinazosaidia, wanipatie mtaji angalau wa shilingi milioni mbili ili nifanye biashara kubwa itakayonitatia kipato kikubwa kitachonikwamua kimaisha”, alisema kijan

HATIMAE MWANAFUNZI WA DARASA LA TANO MWENYE ULEMAVU WA KIUNGO APATIWA MSAADA.

Image
  NA FATMA HAMAD FAKI,PEMBA Hatimae   Wahisani na wafadhili wameanza kujitokeza kumsaidia   kijana Anifu   Jeilani Isaa mwenye ulemavu wa viungo,   mwanafunzi wa darasa la tano katika skuli ya msingi Ole   ambae ilikua anakabiliwa na changamoto ya baskeli ya maringi mawili kwa ajili ya kwendea skuli. Akikabidhi msaada huo Katibu wa CCM Jimbo la Ole Yakoub Khalfani Shaha kwa niaba ya Mwakilishi wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa nchi Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Masoud Ali Mohd ,alisema msaada huo umekuja baada ya kuona taarifa zilizo rushwa kwenye mitandao ya kijamii juu ya shida inayo mkabili kijana huyo iliyosababisha kukatisha masomo yake. ‘’Baada ya taarifa zilizo samba mitandaoni juu ya shida zilizokuwa zikimkabili kijana huyo tumeamua kumsaidia ili aondokanae na kero hizo’’ alisema katibu huyo. Mapema Diwani wa Wadi ya Ole Khadija Henok Maziku   alisema utoaji wa   msaada huo kwa mwakilishi huyo ni katika utekelezaji wa ahadi za