MUHALI BADO NI TATIZO KWA JAMII

Wananchi wametakiwa kushirikiana na vyonbo vya kisheria kutoa tarifa wakati  yanapotokezea matendo ya uhalifu  katika jamii ili kuona watendaji wa makosa hayo  waweze kupatikana na kutiwa hatiani.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya kuzuia Rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar Zaeca Ahmed Khamis Makarani wakati akifungua mafunzo  ya  siku moja kwa wandishi wa habari juu ya mapambano dhidi  ya Rushwa yaliofanyika Gombani Chake chake Pemba amesema bado jamii inaonekana ikiyafumbia macho matendo  ya kihalifu wakati yanapotokezea katika jami zao.

Amesema kuwepo kwa rushwa katika jamii ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa matendo maovu ikiwemo Rushwa, Udhalilishaji pamoja na ujambazi, hivyo  basi ni wakati umefika kwa jamii kuacha muhali  na kutoa tarifa kwa mamlaka husika jambo ambalo litasaidia kuondokana na vitendo  hivyo.

Alifahamisha kuwa kuwepo kwa muhali hakuna  maendeleo yanayopatikana bali hupelekea wanyonge kuonewa na kukosa haki zao.

Akiwasilisha mada juu ya nafasi ya vyombo vya habari katika mapambano dhidi ya rushwa Mjumbe kutoka jumuia ya wanadishi wa habari Pemba PPC Ali Mbarouk Omar amewataka wandishi wa habari kuielimisha jamii  juu ya athari za kuwepo kwa muhali ili waweze kuziibua na kuziripoti kesi zinazojitokeza.

Nae Afisa dhamana kutoka mamlaka ya uhujumu uchumi Zanziba  Zaeca ofisi ya Pemba Suleiman Ame Juma amewataka wandishi wa habari kuibua na kuandika habari zinaonesha viashiria vya uhujumu uchumi uchumi jambo amablo litasaidia mamlaka  ya zaeca kupata taarifa na kuzichukulia hatua za kisheria.

Mafunzo hayo ya siku moja kwa wandishi wa habari juu ya mapambano dhidi rushwa yameandaliwa na Zaeca Zanzibar ambapo ni miongoni mwa shamra shara   za kuazimisha siku ya Zaeca Duniani.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.