Posts

Showing posts from February, 2023

JAMII YASHAURIWA KURUDISHA MALEZI YA ZAMAN.

Image
                                   NA FATMA HAMAD  Mjumbe wa kamati tendaji wa jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Faki Khamis Simai  ameitaka jamii kurudisha  malezi ya  pamoja  katika kuwalea  watoto  wao  jambo  ambalo  litapelekea  kupatikana  kwa  kizazi  chenye  madili  mema. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi  huko katika ofisi za wasaidizi wa sheria wilaya ya wete [WEPO]  amesema    asilimia kubwa ya madili  ya wazanzibar   yameporomoka   ukilinganisha na  miaka ya  nyuma ‘’Zamani   watoto  walikua ni  wa watu wote hakukua na mtoto  wa  Fulani wala  wa Fulani akifanya kosa anahukumiwa ni  mtu yoyote  wala hakuna tatizo lolote’’ alisema Faki Simai. Hivyo  ni  wakati   wazazi   kuamka  na  kukshirikiana   kwa pamoja  ili   kurudisha  malezi  ya  zamani  jambo ambalo litakua ni muarubaini wa kupunguza  mmongonyoko wa madili ya  wazanzibar  na kupelekea watu kuishi wakiwa na hkofu ya Allah [A,T]. Aidha kwa upande mwengine ameitaka jamii kuwacha tabia ya kuzificha na k

UKOSEFU WA WALIMU MJUMUISHI UNAVYOATHIRI NDOTO ZA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU PEMBA

Image
                             NA FATMA HAMAD, PEMBA ‘’Namshukuru nimefaulu mtihani wangu wa darasa   la kumi   na leo nipo   darasani na jumuika na wenzangu, kuchota elimu hapa skuli ya sekondari Kinyasini,’’anasema mwanafunzi. Hayo ni maneno ya mwanafunzi Hussein Abdalla Rashid   mwenye ulemavu mchanganyiko mkaazi wa Kwale gongo wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba. Abdalla ni mwanafunzi ambae anaisaka elimu katika mazingira magumu, kwani anakotoka kijiji cha mbali na kwenye mabonde na milima. ‘’Ninatoka kjiji cha mbali ambapo ni kilo mita 10, kutoka nyumbani kwetu hadi skuli, ila sijali   kwani ndoto yangu ni kuwa fundi wa umeme,’’ alisema Abdala. CHANGA MOTO ZA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU Abdalla Husein Rashid amesema kuwa anatamani siku moja   awe   fundi   mkubwa   wa   umeme,   lakini bado   wanakilio   kwenye Skuli zao   hakuna   walimu   wa kufundisha   wanafunzi wenye ulemavu. Amesema kitendo cha   wanafunzi wenye ulemavu kuchanganywa   darasa   moja na wasio na ule

TAMWA YAIBUA KASORO SHERIA ZA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI

Image
                                             13/2/2023. NA FATMA HAMAD PEMBA KATIKA   kupiga    vita suala la   udhalilishaji   wa   kijinsia, Serikali imeweka mikakati   mbali   mbali,   ikiwemo kufanya   marekebisho   ya   sheria, ambazo   zinahusu   masuala   ya   udhalilishaji   wa   kijinsia, ili   kuona   jamii   inaondokana   nalo. Lakini   licha   ya   marekebisho   hayo   bado    vipo   vifungu   kadhaa   vya sheria, ambavyo vinaonekana   bado   vina mapungufu   na vinaleta ukakasi   juu ya uendeshwaji na utolewaji wa hukumu   kwa kesi za udhalilishaliji   katika vyombo vya sheria.   WANAJAMII.                                                                  Kombo Ali Hamad mwanajamii kutoka wilaya ya Wete, amesema mtu yoyote atakae mnajisi mtu mwenye ulemavu asipewa dhamana kifuatwe kifungu cha 151 [1] cha sheria 7 ya 2018 sheria ya Mwenendo wa makossa ya Jina, kwani   wenye ulemavu na wao ni bidamu   na linathirika zaid   kundi hilo . ‘’ Mimi kwa maoni yangu nashau