JAMII YASHAURIWA KURUDISHA MALEZI YA ZAMAN.
NA FATMA
HAMAD
Mjumbe wa
kamati tendaji wa jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Faki Khamis
Simai ameitaka jamii kurudisha malezi ya
pamoja katika kuwalea watoto wao jambo
ambalo litapelekea
kupatikana kwa kizazi
chenye madili mema.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi huko katika
ofisi za wasaidizi wa sheria wilaya ya wete [WEPO] amesema
asilimia kubwa ya madili ya
wazanzibar yameporomoka ukilinganisha na miaka ya
nyuma
‘’Zamani watoto
walikua ni wa watu wote hakukua na
mtoto wa
Fulani wala wa Fulani akifanya
kosa anahukumiwa ni mtu yoyote wala hakuna tatizo lolote’’ alisema Faki
Simai.
Hivyo ni
wakati wazazi kuamka
na kukshirikiana kwa pamoja
ili kurudisha malezi
ya zamani jambo ambalo litakua ni muarubaini wa kupunguza mmongonyoko wa madili ya wazanzibar na kupelekea watu kuishi wakiwa na hkofu ya Allah [A,T].
Aidha kwa
upande mwengine ameitaka jamii kuwacha tabia ya kuzificha na kuzifanyia suluhu
wenyewe kwa wenyewe kesi za
udhalilishaji jambo ambalo litasaidia kuendelea kwa matukio ya udhalilishaji wa
wanawake na watoto ndani ya Nchi.
Kwa upande
wake afisa mipango kutoka jumuia ya
wasaidizi wa sheria wilaya ya wete Salim
Hamad Salim amewataka viongozi wa dini kushirikiana na wasaidizi wa sheria
kuielimisha jamii ili kuona wanakuwa mstari wa mbele kupiga vita vitendo viovu
ikiwemo udhalilishaji wa kijinsia, ubakaji na ujambazi.
‘’Viongozi wa dini na nyinyi mnamchango mkubwa katika kuhakikisha jamii inaishi kwa amani bila ya kuepo na matatizo yoyote’’ alieleza afisa mipango.
Nae
mkurugenzi wa jumuia hiyo Hemed Ali
Hemed amewataka wasaidizi wa sheria wasivunjike moyo bali waendelee kuielimisha
jamii ili kuhakikisha wanaifahamu sheria na kuweza kudai haki zao wakati zitakapo vunjwa.
Comments
Post a Comment