DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO
NA FATMA HAMAD – PEMBA
SHAHIDI BASHE MAKAME Khamis ambae ni Afisa kutoka Maabara ya Mkemia mkuu wa Serikali Zanzibar ameiambia Mahkama ya Mkoa iliyopo Wete Kaskazi Pemba, k baada ya kufanya uchunguzi wa vinasaba katika Mashine ya DNA vipimo vimengudua kwamba mtuhumiwa Bahati Mashauri ndie baba mzazi wa mtoto aliezaliwa na binti aliembaka.
Akitoa ushahidi wake mbele ya Mahkama hiyo ya Mkoa Bashe alidai kuwa baada ya kupokea vinasaba vya mtoto aliezaliwa na vya mtuhumiwa pamoja na mama aliezaa baada ya kubakwa, alianza kufanya uchunguzi wa vinasaba vya mtoto na mtuhumiwa na kugudua kwamba mtuhumiwa ndie baba mzazi wa mtoto kwa asilimia 9.99
Aidha alidai kuwa aliendelea kufanya vipimo vya vinasaba vya mtoto na mama yake pia aligundua kwamba mtoto ndie mama yake mzazi binti ambae amedaiwa kubakwa.
‘’Baada ya kufanya uchunguzi wa vinasaba vya mtuhumiwa, mtoto na mama kipimo chetu cha DNA kiligundua kwamba mtuhumiwa ndie baba mzazi wa mtoto, na yule binte ndie mama wa mtoto,’’alidai.
Alidai kuwa kwa mujibu wa majibu walioyagundua katika vipimo vyao ni wazi kwamba mtuhumiwa anaedaiwa kubaka ndie baba mzazi wa mtoto.
Baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake huo shahidi huyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP ) Juma Mussa Omar alidai walikua wamebakiwa na shahidi huyo mmoja na wanafunga ushahidi hivyo alimtaka Hakimu anaendesha kesi hiyo kuighairisha na kuipanga siku nyengine kwa ajili ya kuendelea na hatua nyengine.
‘’Mheshimiwa Hakimu sisi tulikua tumebakiwa na shahidi huyo mmoja na leo tunafunga ushahidi, hivyo tunaomba uighairishe hadi sikunyengine,’’alidai.
Nae Hakimu wa Mahkama hiyo ya Mkoa ambae ndie anaeisikiliza kesi hiyo Zuwena Mohamed Abdulkadir alikubaliana na ombi la upande wa mashataka, na aliighairisha hadi April 15 mwezi huu kwa hatua ya utetezi.
‘’Mtuhumiwa naipanga tarehe hiyo ya 15 ili tuje tuone kama una la kujibu ama laa,’’alieleza.
Ilidaiwa Mahkamani hapo mtuhumiwa huyo baina ya mwezi wa Mei na Juni mwaka jana majira ya saa 12:00 za usiku, katika kijiji cha Gando Chaoni Wete Pemba, alimbaka msichana wa miaka 14.
Ambapo kufanya kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 108 (1) (2) (e) na 109 (1) vya sheria ya adhabu, nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment