Posts

Showing posts from June, 2022

MAGUMU ANAYOYAPITIA MWALIMU WA MADRSA MWENYE ULEMAVU WA VIUNGO PEMBA HAYA HAPA.

Image
Saada Khamis: Mwalimu wa madrassa mwenye ulemeavu Awapatia watoto elimu kwenye mazingira magumu NA FATMA HAMAD, PEMBA ‘’KIPINDI cha mvua  wanafunzi hulazimika niwafungie  wasije madrasani mpaka  zitakapo malizika,’’ hayo ni maneno ya Sada  Khamis  Hamad  mwenye ulemavuwaviungo  ni  mwalimu wa madrssa. Kwake anasema ulemavu alionao  haukua mzigo kuwa  asitimize ndota zake za kuwa mwalimu wa madrassa. Hii ni baada ya kuukosa uwalimu wa skuli kutokana na changamoto za hapa na pale, ingawa hakukata tamaa. ‘’Nilikuwa natamani siku moja niwe darasani nafundisha   ila sikubahatika, kusoma skuli hata darasa moja, kwani ilikuwa iko maeneo ya mbali na siwezi kutembea,’’anakumbuka.  Ukosefu wa kiti mwendo kwa wakati huo, na hasa kutokana na ukata wa fedha waliokuwa nao wazazi wake, ulimkosesha elimu ya skuli. Yote hayo ni masikitiko ya Mwalimu wa Madrasa ya Qur-aan  Sada Khamis Hamad mwenye ulemavu wa viungo anaeishi katika kijiji cha Shumba Vyamboni Wilaya ya Micheweni Pemba. M

WANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZISOMA SHERIA

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Wandishi  wa  habari   wametakiwa  kuzisoma na kuzifahamu sheria  mbali mbali  ili waweze kuandika habari  zenye  ukweli ambazo zitaleta  tija kwa jamii. Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya  Mkoani Khatibu Juma Mjaja wakati akizungumza na wandishi wa habari katika mafunzo ya kujadili sheria ya habari huko gombani Chake chake Pemba. Amesema wandishi wa habari ni wadau wakubwa ambao mnaweza kuiletea nchi mabadiliko hivyo ni muhimu  kuzifahamu kanuni na sheria  ambazo zitawaongoza kuandika habari zenu kwa kuzingatia madili. ‘’Nyinyi wandishi wa habari ni wadau muhimu katika Nchi  hivyo ni lazima muzisome sheria ili muweze kuwa wadilifu katika kazi zenu’’ amesema Mkuu wa wilaya. Katibu mtendaji kutoka baraza la habari Tanzania [MCT]  Kajubi Mukajanga  amesema  kutokuzifahamu sheria sio kinga ya kutokuadhibiwa wakati unapoivunja,  hivyo ni lazima musome sheria ili muepuke  kuandika habari zenye  kusababisha migogoro. ‘’Msipo zifahamu sheria  mtandika habari am

huduma za maji kuboreshwa vijijini

    NA FATMA HAMAD PEMBA. Wananchi wa Vijiji vya Kigongoni, Miongoni pamoja na vijiji vyengine ambavyo havijafikiwa na huduma ya maji safi na salama wametakiwa   kuwa   wastahamilivu kwani    wizara husika tayari ipo katika mchakato wa kumaliza tatizo   la upatikana wa huduma hiyo   Vijijini humo. Hayo yamesemwa   na Waziri wa   Maji   Nishati na Madini Zanzibar   Shaib Hassan Kaduara katika ziara yake aliyoifanya Kisiwani Pemba, kwa ajili ya kuskiliza Kero za Wananchi za upatikanaji wa Huduma ya Maji Safi na Salama. Amesema tayari wameshaanza kuyafanyia kazi baadhi ya maeneo na sasa wanaboresha Miundombinu ili kuona huduma hiyo inapatikana   katika vijiji vyote vya   Pemba. ‘’Takribani vijiji vingi ambavyo vilikua na tatizo la ukosefu wa huduma ya maji tayari    kama vile Michungwani, Wesha   tayari vimeshapatiwa ufumbuzi ‘’ alieleza waziri. Wakitoa changamoto yao   mbele ya waziri huyo   Wananchi wa michungwani wilaya ya Chake chake    wamesema   maji wanayoyapata   yamec

WANAOHARIBU USHAHIDI WAONYWA

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Serikali ya mkoa wa Kusini pemba imesema  haitomvumilia  mtendaji yoyote  atakaebainika  anashiriki kuharibu ushahidi wa kesi ya udhalilishaji  kwa makusudi ili kesi hiyo isiendelee mahakamani. Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud katika madhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika  huko Gombani Chake  chake Pemba. Amesema  wapo baadhi ya watendaji  wakiwemo Madaktari hawataki kwenda mahakamani kutoa ushahidi hivyo  hatutokubali tutawachukulia hatua kali za kisheria  watakao kataa  kutoa ushahidi. ‘’Wapo madaktari ambao  mnawafanyia uchunguzi  wanaodhalilishwa  hamtaki kwenda kutoa ushahidi, lakini nimeshaliagiza jeshi la Polisi liwaweke ndani madaktari watakao kataa’’alisema mkuu wa Mko Amesema  vitendo vya udhalilishaji vimeshakua tishio kwa jamii hivyo kama  watu watakataa kutoa ushahidi hakuna kesi itakaopata hatia  na badalayake tutaendelea kuibebesha  mzigo wa lawama mahakama  kwamba haitendi haki. Mapema Ofisa mdhamini wizara

DC MICHEWENI APIGA VITA UNYANYAPAA DHIDI YA WATOTO WENYE ULEMAVU

Image
  NA FATMA HAMAD -- PEMBA. Wazazi    na    walezi    wenye   watoto   wenye   ulemavu   wametakiwa   kuwapeleka    Skuli pamoja na madrasa   ili nawao   waweze kujipatia haki yao   ya elimu kama watoto wengine. Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi   kwa njia ya simu alisema bado wapo wazazi wanatabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu na badalake kuwakosesha haki zao. ‘’Niwaombe wazazi waache tabia ya kuwafungia ndani watoto wenye ulemavu kwani   nawao   ni binadamu kama wengine wanahitaji kupata haki zote stahiki, ’’alisema mkuu wa Wilaya. Alieleza wapo wazazi katika jamii   wanapozaa watoto wenye ulemavu   wamekuwa wakiwanyanyapaa na kuhisi kama ni mkosi ndani ya familia yao, jambo ambalo haileti picha nzuri kwa mwenyewe mwenye ulemavu na hata kwa Mwenyezi Mungu. Alifahamisha watoto wenye ulemavu waliowengi wanapenda kusoma na mara nyingi Mungu huwajaalia kipaji, hivyo ni budi wapatiwe fursa   m

WANAFUNZI MASKULINI WAPEWA NENO.

Image
NA FATMA HAMAD PEMBA. Wanafunzi    wametakiwa   kuwa mstari wa mbele   kutoa   tarifa   kwa   walimu au wazazi wao wakati watakapoona   viashiria   vya udhalilishaji katika maeneo yao. Wito huo umetolewa na Msaidizi wa Sheria kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Micheweni Said Salum Khamis   alipokuwa akitoa elimu juu ya mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji   watoto huko skuli ya   Sizini   ikiwa ni shamra shamra ya madhimisho ya siku    ya mtoto wa afrika. Alisema   vitendo vya udhalilisha vinafanyika katika mazingira ya jamii hivyo wakati umefika kwa wanafunzi kuondosha   muhali bali watoe tarifa   pale wanapoona vitendo vya udhalilishaji ili viweze kuchukuliwa hatua za kisheria. ‘’Sasaivi udhalilishaji unafanyika   kila   pahala hivyo msiogope toeni tarifa msiogope’’ alisema Said Salum. Mapema Sanani Said Salum kutoka jumuia hiyo Wilaya ya Micheweni amewahimiza wanafunzi hao   kushughulikia masomo zaidi   na kujiepusha na vishawishi vinavyoweza kuwasababish