huduma za maji kuboreshwa vijijini

 

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wananchi wa Vijiji vya Kigongoni, Miongoni pamoja na vijiji vyengine ambavyo havijafikiwa na huduma ya maji safi na salama wametakiwa  kuwa  wastahamilivu kwani   wizara husika tayari ipo katika mchakato wa kumaliza tatizo  la upatikana wa huduma hiyo  Vijijini humo.

Hayo yamesemwa  na Waziri wa  Maji  Nishati na Madini Zanzibar  Shaib Hassan Kaduara katika ziara yake aliyoifanya Kisiwani Pemba, kwa ajili ya kuskiliza Kero za Wananchi za upatikanaji wa Huduma ya Maji Safi na Salama.

Amesema tayari wameshaanza kuyafanyia kazi baadhi ya maeneo na sasa wanaboresha Miundombinu ili kuona huduma hiyo inapatikana  katika vijiji vyote vya  Pemba.

‘’Takribani vijiji vingi ambavyo vilikua na tatizo la ukosefu wa huduma ya maji tayari   kama vile Michungwani, Wesha  tayari vimeshapatiwa ufumbuzi ‘’ alieleza waziri.

Wakitoa changamoto yao  mbele ya waziri huyo  Wananchi wa michungwani wilaya ya Chake chake   wamesema  maji wanayoyapata  yamechanganyika na madini chuma  kutokana na uchakavu wa miundombinu.

‘’Maji tunapata japo ni kwa mgao lakini ni machafu   tunashindwa hata kuyanywa  kwa kuhofia afya zetu’’ walisema wananchi wa michungwani.

 Mkurungezi wa Mamlaka ya  Maji Zanzibar Zawa Tawi la Pemba, Omar Mshindo Bakari amewatoa hofu wananchi hao juu ya usalama wa maji hayo.

‘’Kiwango cha madini chuma kilichomo katika maji hayo hana  athari yoyote  hivyo  ni waombe wananchi waendelee  kutumia  maji  hayo bila  wasi wasi wowote’’  alisema mkurugenzi.

Katika Ziara hiyo waziri Kaduara alitembelea  Vianzio vya maji katika  vijiji mbali mbali  ikiwemo Kijangwani na Michungwani  pamoja na kukagua zoezi la ufikishwaji wa umeme huko Chokocho Wilaya ya Mkoani Pemba.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.