Posts

Showing posts from August, 2023

WANDISHI WA HABARI WAPEWA MBINU ZA KUANDIKA HABARI ZA UDHALILISHAJI.

Image
                 NA FATMA HAMAD, Wandishi wa habari wametakiwa kufuata madili na miko ya  uwandishi wa habari wakati wanapoandika na kuripoti habari zao, ili kuepusha migongano isiyo ya lazima. Akizungumza na wandishi wa vyombo mbali mbali vya habari katika mafunzo ya kuwajengea uwezo jinsi ya  kuandika na  kuripoti  habari za udhalilishaji, Afisa mkuu wa mawasiliano na uchechemuzi kutoka chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar Safia  Ngalafi, huko mkanjuni Chake Chake Pemba. Alisema kwa mujibu wa  utafiti  wa kihabari  uliofanywa  na Tamwa  ili kuona jinsi gani  wandishi wa habari wanaripoti habari za udhalilishaji, imeonekana kuwa,  bado wandisi   hawajakuwa na uwelewa wa kutosha juu ya kuandika na kuripoti habari za udhalilishaji. ‘’ Tulifanya utafiti  kwa  kuangalia habari zinazoripotiwa na wandishi wa habari  kupitia Gazeti la Zanzibar leo, Nipashe, Habari leo,  Assalam fm, Furaha, pamoja na soio media.’’ Alisema bi safia. Alisema bado wandishi wa habari wanahitaji

ZAFELA YAWA MSAADA KWA WATOTO WA KIKE WALIOACHA SHULE

Image
  NA FATMA HAMAD, Mkurugenzi wa Jumuia ya  Wanasheria   wanawake Zanzibar   Zafela   Jamila Mahmo ud,  amezitaka asasi za kiraia kushirikiana kwa Pamoja na kuwajengea uwezo Watoto wa kike,  walioacha Skuli  ili  waweze  kurudi shuleni na kuendelea na masomo yao. Mkurugenzi huyo aliyasema hayo katika mkutano wa kuutambulisha mradi wa Malala, utakaoendeshwa na Zafela visiwani Zanzibar   kwa muda wa mwaka mmoja, kikao hicho kilichowajumuisha asasi mbali mbali za kirai kisiwani Pemba. Alisema katika utafiti wao walioufanya   waligundua kuwa ,kuna   wimbi kubwa la watoto wa kike   wamekuwa wakikatisha   masomo yao kutokana na sababu mbali mbali, ikiwemo kuolewa, kupata mimba za utotoni Pamoja na kufanyishwa   kazi za nyumbani. Alisema wamekuwa wakipokea kesi nyingi za Watoto wa kike, kuda haki zao, aidha waliolewa au waliojihusisha na mahusiano, ambao ukiwangalia umri wao   unapaswa     wawe wako shuleni na wanaendelea na masomo yao. ‘’Tumeamua kuleta mradi huu wa Malala   kwa aji

HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA INAVYOKOSESHA USINGIZI WANANCHI WA KIJIJI CHA MJINI KIUYU

Image
                             NA FATMA HAMAD PEMBA, Ukosefu wa huduma za maji safi na salama,  bado ni kilio kikubwa kwa wananchi wa kijiji cha  Mjini kiuyu wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazi Pemba. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao, mwananchi Bikame Bakar Darusi,  alisema  huu  ni  mwaka wa tano  sasa  wamekua  wakikosa  huduma  hiyo  ya  maji safi  na salama. Alisema wamekuwa wakipata tabu kwani wanashindwa kupata maji ya kutosha ya kufanyia  shughuli zao za nyumbani. ‘’Tunashindwa kupata maji hata ya kuwakoshea watoto wetu’’alieleza mwanachi Bikamae. Aliendelea kusema kuwa watoto wao wanakwenda skuli na uchafu  kutokana na kadhya hiyo. Kwa upande wake Bakar Hamad alisema suala la maji limekua ni tatizo sugu, ambalo linawatesa wanawake wa kijijini  hicho. Alisema  siku yanayotoka maji kwa baadhi ya mabomba  hutoka kuanzia  sa tano  hadi tisa za usiku,  hali ambayo inapelekea wamama kukesha kwenye foleni ya maji. ‘’Hakuna hata mwanamme  mmoja anaelala na mke wake w

UFAHAMU UZAZI WA MPANGO

Image
                                                 NA FATMA HAMAD PEMBA Wananchi kisiwani Pemba wameshauriwa  kutumia njia salama ya uzazi wa mpango hali ambayo itasaidia kuimarisha afya ya mama na mtoto.   Ushauri huo umetolewa na mtaalamu wa masuala ya Afya ya uzazi  Rahila Salim Omar kwa wandishi wa habari kisiwani Pemba alisema zipo njia kadhaa za kupanga uzazi ambazo zote ni salama. Alisema miongoni mwa  njia hizo  ni zile za kisayansi pamoja  na za kisasa   ambapo  hazina madhara yoyote. Alisema miongoni mwa njia  hizo ni kama vile kitanzi kwa mama ambaye hajajifungua sana, sindano,vipandikizi,vidonge ambazo zote ni salama na   hutolewa kulingana na afya ya mama. ''Sio kweli kwamba ukipanga uzazi unapata matatizo tusidanganyane, kitalamu hakuna hilo njia zote zipo salama, alifahamisha docta Rahila'' kwa upande wake Sheikh Mohamed Nassor  Abdala kutoka jumuia ya maimau Pemba [JUMAZA]  Alisema Uislamu  hujakataza  uzazi wa mpango. ''Kisheria mtoto anatakiwa an

VIKUNDI VYA USHIRIKA VYAOMBA KUUNGWA MKONO

Image
                          NA FATMA HAMAD PEMBA Wanakikundi cha Mapambano Co-Oparative   kinachojishuhulisha na ufugaji wa Samaki, Kaa na Kamba kilichopo Sizini wilaya ya Michewemi mkoa wa Kaskazini Pemba wameiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, pamoja na asasi nyengine kuviangalia na kuviunga mkono vikundi vya ushirika, ili viweze kwenda samba mba na Sera ya Serikali    ya Uchumi wa Buluu. Wakizungumza   na   mwandishi wa habari hizi   huko kwenye Kikundi   chao   Sizini Wilaya ya Micheweni walisema sera ya Serikali ya Uchumi wa Buluu ni kuhakikisha     wanaviinuwa   vikundi vya ushirika   ili viweze kutoa tija na kuondokana na umasikini. Alisema   wamekuwa wakipata faida kubwa   kwani tayari wameshapata   pesa za kuendeshea   maisha   yao kupitia mavuno   waliovuna msimu uliopita. ‘’ Tumeamua kufuga, Kamba na Samaki   jambo ambalo litatuwezesha kujingizia kipato, hivyo twaiomba Serikali ituunge mkono kihali na mali ili kutimiza malengo ya Serikali juu ya uchumi wa buluu,’’ wa

WANDISHI WAPEWA NENO

Image
                                     NA FATMA HAMAD PEMBA.   Wandishi wa habari   w ame takiwa ku toa elimu kwa jamii ili   kufahamu   umuhimu wa afya ya uzazi. Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini wizara ya afya wakati akifunga   Mafunzo ya Siku tatu yanayo husu   afya ya Uzazi kwa wandishi wa habari h uko katika ukumbi wa Chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania [TAMWA] Chake chake Pemba.   A lisema imeonekana   bado jamii haina uwelewa wa kutosha   kuhusu afya ya uzazi ,jambo ambalo linachangia   kukosa afya bora ya mama na mtoto. ‘’Ndugu zangu nyinyi wandishi wa habari ndio kioo kwa jamii, hivyo tunaomba mtusaidie kuielimisha jamii jambo ambalo litaepusha Vifo vitokanavyo vya uzazi,’’ alisema mdhamin bilali. Aidha   aliiasa jamii kuacha tabia ya kuwaozesha   waume mabinti zao ambao hawajafikia umri wa miaka 18, kwani kutawaepusha na matatizo mbali mbali yatokanayo     na uzazi. ‘’Siku hizi kuna matatizo mengi jamani yatokanayo na uzazi, hivyo wazazi tuacheni