HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA INAVYOKOSESHA USINGIZI WANANCHI WA KIJIJI CHA MJINI KIUYU
NA FATMA HAMAD PEMBA,
Ukosefu wa huduma za maji safi na
salama, bado ni kilio kikubwa kwa
wananchi wa kijiji cha Mjini kiuyu
wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazi Pemba.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao, mwananchi Bikame Bakar Darusi, alisema huu
ni mwaka wa tano sasa
wamekua wakikosa huduma
hiyo ya maji safi
na salama.
Alisema
wamekuwa wakipata tabu kwani wanashindwa kupata maji ya kutosha ya kufanyia shughuli zao za nyumbani.
‘’Tunashindwa
kupata maji hata ya kuwakoshea watoto wetu’’alieleza mwanachi Bikamae.
Aliendelea
kusema kuwa watoto wao wanakwenda skuli na uchafu kutokana na kadhya hiyo.
Kwa upande
wake Bakar Hamad alisema suala la maji limekua ni tatizo sugu, ambalo linawatesa
wanawake wa kijijini hicho.
Alisema siku yanayotoka maji kwa baadhi ya
mabomba hutoka kuanzia sa tano
hadi tisa za usiku, hali ambayo
inapelekea wamama kukesha kwenye foleni ya maji.
‘’Hakuna
hata mwanamme mmoja anaelala na mke wake
wakati wa usiku, kwani wanawake hulala kwenye
foleni za maji’’ alieleza mwananchi bakar.
Mapema Fatma
Khalfan Suleiman alisema kuwa ukosefu wa maji unaweza ukapelekea wananchi wa
kijiji hicho kupata maradhi hatarishi yatokanayo na uchafu.
‘’hatupati
maji tukaweza kusafishia vyoo pamoja na nyumba zetu’’
Nae Ali
Masoud alisema wananchi wa kijiji hicho
wameanguka kiuchumi kwani,
hawapati maji ya kumwagilia mazao yao.
‘’Kazi yetu
kubwa sisi ni kilimo cha mboga mboga ila kwa sasa kimetushinda, tunateseka na
watoto,’’ alisema Ali Masoud.
Hivyo
wameitaka wizara husika kukiona kilio chao ili waweze kuondokana na kadhya
hiyo.
Fatma Ali na
Asha Juma wanafunzi wa darasa la tano walisema wanakosa kusoma masomo ya vipindi vya mwanzo
darasani kutokana na kuchelewa kwenye
kutafuta maji kwa ajili ya matumizi ya
nyumbani.
Afisa uhusiano wa mamlaka ya maji [Zawa] Pemba Suleiman Anas Masoud, amekiri kuwepo kwa hilo kijiji hapo.
Alisema
tatizo hilo linasababishwa na kukosekana
kwa matangi pamoja na uchakavu wa miundombinu ya kusambazia maji.
Hivyo
amewataka wanachi hao kuwa na subra, kwani tayari wameshaingizwa kwenye mradi
mpya ambao, unamaliziwa kufanyiwa
upembuzi yakinifu, unaofadhiliwa na Benk ya watu wa ujerumani, ambao utajenga matangi kwenye vijiji vilivyo
na shida ya maji.
Comments
Post a Comment