Posts

Showing posts from May, 2022

RUSHWA MUHALI BADO NI TATIZO KWA JAMII

Image
  NA FATMA HAMAD PEMBA. Imebanika kuwa  rushwa  muhali  bado  ni  kilio  kikubwa  kinachoendelea  kuikumba  jamii  hali ambayo  inapelekea   kesi  nyingi  za  udhalilishaji  kufutwa  Mahakamani  kutokana  na kukosa  ushahidi. Wakizungumza  katika mkutano  wa  robo mwaka wa kujadili juu  ya  utekelezaji  wa  majukumu yao wana mtandao  wa kupinga udhalilishaji kutoka  wilaya  ya  Mkoani huko  ukumbi wa Chama cha Wandishi  wa habari Wanawake Tanzania [Tamwa] iliyopo chake chake Pemba. Wamesema licha ya juhudi  zinazoendelea  kuchukuliwa na Serikali pamoja na wanaharakati mbali mbali  ya kuwafahamisha jamii kufahamu  madhara ya udhalilishaji lakini bado juhudi hizo zinagonga mwamba. Wamesema  wamebaini kuwa  wengi wafanyaji  wa matukio hayo huwa ni ndugu wa familia  moja, hivyo huzimalizia mitaani hawaendi kutoa ushahidi  kwa kuhofia ugomvi katika familia zao. ‘’Sasa hivi kunapotokezea udhalilishaji huamua kupigishana faini wenye kwa wenyewe majumbani hawendi katika vyombo vya sheria kwa k

ANAYEDAIWA KUMLAWITI MTU MWENYE ULEMAVU WA AKILI PEMBA, APATA UZIWI GHAFLA MAHAKAMANI

NA FATMA HAMAD, PEMBA HAKIMU wa mahakama Mkoa Wete, Mwendesha mashtaka, Karani, na askari wa mahakama, wamepigwa na butwaa baada ya baba mzazi wa mtuhumiwa wa ulawiti, kudai mtoto wake ni kiziwi. Awali mtuhumiwa huyo alikuwa ni mzungumzaji mzuri, wakati kesi yake ikiendeshwa mahakamani hapo kabla ya kuondolewa kwa madai ya kudanganya umri. Ilibainika kuwa wazazi wa kijana huyo mwenye miaka 19, anaedaiwa kumlawiti kijana mwenzake mwenye ulemavu wa akili na kisha kupandishwa katika mahakama ya mkoa B Wete, Febuari 13, mwaka huu ingawa kesi yake iliondolewa mwezi Machi mwaka huu baada ya kudaiwa kudanganya umri. Ndipo mahakama ya mkoa ‘B’ ilipompandisha kwenye kizimba chake na kusomewa upya shtaka lake, kama mtu mzima, ingawa baba mzazi kabla ya mtoto wake [mtuhumiwa] kujibu lolote, alidai kuwa ni kiziwi. Hoja ya mzazi huyo, ilichukua takriban dakika mbili mahakamani hapo, ikijadiliwa baina ya hakimu, mwendesha mashtaka na baba mzazi, juu ya ulemavu ulioibuka ghafla na kuwashang

WALIMU WA MADRASA WAENDELEZA VIPAJI VYA QUR AN

Image
Walimu wa madrasa za Qurani   pamoja   na wazazi   wametakiwa kushirikiana kwa    pamoja   kuwasimamia   watoto   wao   kuhakikisha   wanaendeleza    suala la uhifadhi wa Qurani     ili kupatikana vipaji   vyenye ubora. Hayo yamesemwa na Mmoja wa wazazi   wa wanafunzi   wa madarasa za kurana   Ali Hamad Bakari   katika hafla ya mashindano ya tahfidh lkuran yaliofanyika Viwanja vya mpira Pwepweu viliopo   Tumbe wilaya ya Micheweni Mkoa waKaskazini Pemba   amesema uhifadhi wa kurani ni suala muhimu kwani hupelekea   kuwepo   na kizazi   chenye   madili. ‘’Mashirikiano ya pamoja ndio njia pekee inayopelekea wanafunzi kuendeleza masomo yao na kuibua vipaji’’ alieleza mzazi. Akitoa nasaha zake mara   bada ya kumalizika kwa mashindano hayo Msaidizi   wa Katibu   mtendaji Ofisi ya Mufti mkuu upande wa Pemba Said Ahmad amewawataka walimu wa madrasa    kuliendeleza   suala   la uhifadhi   wa guranai   ili kuviendeleza viapaji   hivyo ili kuweza kukipatia sifa nzuri Kisiwa cha Pemba. Mas