RUSHWA MUHALI BADO NI TATIZO KWA JAMII

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Imebanika kuwa  rushwa  muhali  bado  ni  kilio  kikubwa  kinachoendelea  kuikumba  jamii  hali ambayo  inapelekea   kesi  nyingi  za  udhalilishaji  kufutwa  Mahakamani  kutokana  na kukosa  ushahidi.

Wakizungumza  katika mkutano  wa  robo mwaka wa kujadili juu  ya  utekelezaji  wa  majukumu yao wana mtandao  wa kupinga udhalilishaji kutoka  wilaya  ya  Mkoani huko  ukumbi wa Chama cha Wandishi  wa habari Wanawake Tanzania [Tamwa] iliyopo chake chake Pemba.

Wamesema licha ya juhudi  zinazoendelea  kuchukuliwa na Serikali pamoja na wanaharakati mbali mbali  ya kuwafahamisha jamii kufahamu  madhara ya udhalilishaji lakini bado juhudi hizo zinagonga mwamba.

Wamesema  wamebaini kuwa  wengi wafanyaji  wa matukio hayo huwa ni ndugu wa familia  moja, hivyo huzimalizia mitaani hawaendi kutoa ushahidi  kwa kuhofia ugomvi katika familia zao.

‘’Sasa hivi kunapotokezea udhalilishaji huamua kupigishana faini wenye kwa wenyewe majumbani hawendi katika vyombo vya sheria kwa kuogopa mtuhumiwa asije akafungwa’’ walisema wadau.

Walisema licha ya kuwa shahidi  ambae amefanyiwa udhalilishaji atatoa ushahidi wake vizuri  katika hatua za awali  mwisho wa siku hupewa sumu ili kukanusha ushahidi alioutoa  ilimradi tu uonekane  kuwa ni wa uongo.


Kwa upande wake Rashidi Mshamata kutoka wilaya ya wete  amsema  ili  kuondosha hilo nivyema  Serikali  kuweka  nyumba salama za kuwekwa mashahidi  ambao pia ni wathirika wa matukio hayao.

‘’Shahidi akirudi kwenye jamii yake anapikwa anaiva hatoi ushahidi wa kweli, na laiti zingelikuepo hizo nyumba salama tungefanikiwa’’ alisema Rashid.

Nae mratibu chama cha wandishi wa habari Wanawake [TAMWA] Ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amewashauri  wanamtandao hao pamoja na wandishi wa habari wasivunjike moyo waendelee kuielimisha jamii ili kuondoka na udhalilishaji hapa Nchini.

Jumla ya kesi 10 za udhalilishaji wa kijinsia zimeibuliwa na wanamtandao hao katika wilaya ya Mkoani kwa kipindi cha January hadi Mei mwaka huu.





Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.