Posts

Showing posts from March, 2023

KATIBU MKUU CUF AACHA UJUMBE KWA VIONGOZI WENZAKE

Image
                                          NA FATMA HAMAD PEMBA.   Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Hamad Massoud Hamad amewataka viongozi wenzake wa vyama vya siasa nchini kuyaenzi na kuyalinda   maridhiano   ya Zanzinbar   ili kuwafanya watu wote kuwa kitu kimoja. Katibu huyo ametoa wito huo wakati akizungumza na wapenzi na wafuasi wa chama cha CUF   katika mkutano wake wa mwanzo tokea kuondolewa kwa zuio la mikutano ya hadhara na Rais   wa Jamuhuri ya Muungano   Samia Suluhu Hassan huko wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema kazi walioifanya viongozi wa Zanzibar   akiwemo marehemu maalimu Seif Sharif pamoja na rais mwinyi la kufanya mazungumzo na kuanzisha maridhiano ni jambo kubwa, hivyo niwajibu viongozi kuyaendelenza na kuyatunza maridhiano hayo yaendelee kudumu hapa Nchini. ''Tumekua tukishuhudia kunapomalizika kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar   katika vijiji vyetu hujitokeza migogoro mbalimbali ikiwemo kususiana, hivyo basi   Niwasihi viongozi w

WASAIDZI WA SHERIA WAHIMIZWA KUISAIDIA JAMII.

Image
                             NA FATMA HAMAD PEMBA. Jumuia za wasaidizi wa sheria zimetakiwa kuendelea kuisaidia jamii kwa kutoa msaada wa kisheria ili kupunguza migogoro pamoja na malalamiko yasiyo ya lazima. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa mdhamini   ofisi ya Rais, katiba   sheria, Utumishi na utawala bora   Halima Khamis   Ali   wakati akifungua   mafunzo ya siku moja   ya   kisheria ngazi ya jamii huko makonyo Chake chake Pemba. Alisema wasaidizi wa sheria wanajukumu kubwa katika kuhakikisha wanaielimisha jamii kuhusu masuala ya kisheria   ili kuibua matatizo yanayowakumba wanajamii na   kuweza kupatiwa ufumbuzi. ''Wasaidizi wa sheria mnajukumu kubwa hivyo ni lazima muwe   na uzalendo na   moyo wa kujitolea ili kuleta mabadiliko katika jamii zetu'' alieleza   mdhamini Halima. Alisema   kutokana na umuhimu wa kuepo kwa wasaidizi wa sheria ngazi ya jamii   Serikali imeweka mikakati mbali mbali   ili kuona wanaharakati hao wanatambulika   kisheria   katika ute