WASAIDZI WA SHERIA WAHIMIZWA KUISAIDIA JAMII.


 

                           NA FATMA HAMAD PEMBA.

Jumuia za wasaidizi wa sheria zimetakiwa kuendelea kuisaidia jamii kwa kutoa msaada wa kisheria ili kupunguza migogoro pamoja na malalamiko yasiyo ya lazima.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa mdhamini  ofisi ya Rais, katiba  sheria, Utumishi na utawala bora  Halima Khamis  Ali  wakati akifungua  mafunzo ya siku moja  ya  kisheria ngazi ya jamii huko makonyo Chake chake Pemba.

Alisema wasaidizi wa sheria wanajukumu kubwa katika kuhakikisha wanaielimisha jamii kuhusu masuala ya kisheria  ili kuibua matatizo yanayowakumba wanajamii na  kuweza kupatiwa ufumbuzi.

''Wasaidizi wa sheria mnajukumu kubwa hivyo ni lazima muwe  na uzalendo na  moyo wa kujitolea ili kuleta mabadiliko katika jamii zetu'' alieleza  mdhamini Halima.

Alisema  kutokana na umuhimu wa kuepo kwa wasaidizi wa sheria ngazi ya jamii  Serikali imeweka mikakati mbali mbali  ili kuona wanaharakati hao wanatambulika  kisheria  katika utendaji wa majukumu yao.

Aidha  mdhamini huyo aliwasihi wasaidizi wa sheria kutekeleza majukumu yao ya utoaji wa msaada  wa kisheria kwa kufuata  miko na  madili ya kazi yao.

''Kila kitu kina utaratibu wake na sisi wasaidizi wa sheria sio vizuri kutoa msaada wa kisheria bila kutambulika kisheria'' alisema mdhamini.

Alifahamisha kuwa kitendo walichokifanya jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake [CHAPO]  cha kuanzisha darasa maalumu la sheria ngazi ya jamii ni kitendo cha kupigiwa mfano na kinafaa kuigwa na jumuia zote za wasaidizi wa sheria zilizopo Zanzibar.

Kwa upande wake Afisa habari wa jumuia hiyo Haji Nassor Mohd alisema utoaji wa mafunzo hayo ni moja ya sehemu ya utoaji wa elimu ya kisheria ndani ya jamii.

Mafunzo hayo ya siku 10 ya  kisheria ya kuwajengea uwezo wanashehia  ambayo  yanatarajia kufanyika baada ya kumalizika kwa mwezi  mtukufu wa ramadhani  yatawajumuisha Masheha na wajumbe wao yameandaliwa na jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake [CHAPO]  ambapo mada mbali mbali zitawasilishwa ikiwemo Sheria ya mtoto sheria namba  6/2011 sheria ya Zanzibar.

 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.