Posts

Showing posts from October, 2023

MASHEHA WATAKIWA KUTOA ELIMU KWA JAMII KUFAHAMU ULIPAJI WA KODI YA MAJENGO

Image
                        NA FATMA HAMAD,PEMBA MKURUGENZI wa Bodi ya mapato (ZRA] kisiwani Pemba  Jmal Hassan Jamal amewataka Masheha kuielimisha Jamii  kufahamu umuhimu wa kulipa kodi ili  waweze kulipa kodi jambo ambalo litaipatia Nchi maendeleo. Mkurugenzi huo ameyasema hayo wakati akizungumza na Masheha pamoja na viongozi mbali mbali wa Serikali wa mkoa wa Kaskazini Pemba katika mkutano wa utoaji wa uelewa wa kodi ya majengo huko baraza la Wawakilishi Wete mkoa wa Kaskazini Pemba amesema ulipaji wa kodi ni moja ya chanzo kitakachoipatia Nchi kupiga hatua kimaendeleo. Alisema masheha wana nafasi kubwa katika jamii, hivyo ni jukumu lenu kuwaelimisha wananchi ili kuhakikisha wanatekeleza juku lao la ulipaji wa kodi. ‘’Ndugu zangu masheha ni wajibu wenu kutoa elimu kwa jamii ili kuona wanatekeleza wajibu wa Serikali wa ulipaji wa Kodi,’’alisema. Aidha  kwa upande mwengine alifahamisha kuwa  miongoni mwa majengo yatakayolipiwa kodi ni majumba  ya Ghorofa pamoja na majengo yanayo

RAIS WA ZANZIBA AMESEMA ONGEZEKO LA WATU NI CHANZO CHA KUONGEZEKA KWA MAHITAJI YA JAMII

Image
*RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema ongezeko la watu duniani linachangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa mahitaji mbalimbali ikiwemo maji.*   Amesema tatizo hilo pia husababisha uhaba wa huduma na vifaa mijini na vijijini na kuchangia chachu ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi.   Dk. Mwinyi aliyasema hayo hotel ya Verde Mtoni, mkoa wa Mjini Magharibi, alipofungua kongamano la 24 la maji lililoyashirikisha mataifa kutoka Mashariki na kusini mwa bara la Afrika.   Alisema, hali hiyo huibua maswala mengi yakiwemo kuzorota kwa vyanzo vya maji, uchafuzi wa mazingira, upotevu wa viumbe hai na upotevu wa afya ya mazingira kwa ujumla.    Alisema, ushahidi wa hayo unaonyesha mazingira ya nchi nyingi za bara la Afrika  yanabadilika mara kwa mara kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yanayohuhusishwa na mabadiliko ya hali ya hewa husababisha ongezeko la hatari kutokana na hali mbaya ya hewa.   Rais Dk. Mwinyi pia alieleza, changamoto hizo

Aga Khan Foundation yaihamasisha jamii kupanda miti

Image
                           NA ZUHURA JUMA, PEMBA JAMII imetakiwa kuwa na utamaduni wa kupanda miti katika maeneo yao wanayoishi, ili kuweka mazingira bora pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.   Akizungumza kwa niaba ya Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu Pemba, mwalimu Harith Bakar Waziri wakati wa upandaji miti kwa ajili ya kutengeneza msitu mdogo, katika skuli ya sekondari ya Hemed Pujini alisema,  Wizara itachukua juhudi za makusudi kuhakikisha msitu huo unatunzwa.   Alisema kuwa, ni manufaa makubwa kupata msitu huo kwani eneo hilo ni ukanda wa mashariki ambao umeathiriwa sana na mabadiliko ya tabianchi, hivyo utawasaidia sana wanafunzi, walimu na wanajamii kuwa na mazingira bora na mazuri.   "Muone kuwa kuwepo kwa msitu mdogo hapa ni jambo jema na ni fursa kwenu, hivyo kuna haja kwa jamii kuiga mfano huu na wapande miti maeneo mbali mbali katika mitaa yao," alieleza.   Aidha aliwataka kuulinda na kuuhifadhi msitu huo ili kuleta manufaa kwao na jamii nzim

WATOWA HUDUMA ZA MAMA MTOTO WATOWA YA MOYONI JUU YA HUDUMA YA M MAMA

Image
                                    NA FATMA HAMAD, PEMBA WAUGUZI  wanaotoa  huduma  za  Mama  na  Mtoto  wamesema  licha  ya  kuanzishwa  kwa  huduma  ya M mama  ambayo  imewekwa  kwa  lengo la  kutoa  usafiri  wa  haraka  wakati  ikitokezea  tatizo  kwa  mama  na  mtoto, bado  hauja  saidia  ipasavyo  katika  vituo  hivyo.   Wakizunumza na wandishi wa habari wauguzi wa vituo vya Afya Wesha na Pujini walisema inapotokezea tatizo la mama na mtoto huduma za kuwahamishia Hospitali ya Wilaya inakua tatizo kwa vituo hivyo. Amina   Ali Abdi ni Muguzi Mkunga kutoka kituo cha afya Wesha alisema mzazi anapopata tatizo akipiga simu kwa wahusika wa huduma ya M mama, kwa ajili ya kupata usafiri inakuwa ni shida,   jambo linalohatarisha maisha kwa Wazazi. ‘’Unaweza ukapiga simu tokea asubuhi kutaka usafiri kwa Uongozi wa huduma ya M mama kwa ajili ya kumuwahisha mgonjwa lakini haupatikani na hivyo unapopatikana haufiki kwa wakati, na kulazimika familia ya mzazi itowe gari yenyewe ndipo tuwez

WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA WAPIWA MSASA

Image
                                NA FATMA HAMAD,PEMBA AFISA mdhamini Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Halima  Khamis  Ali  amewataka Wasaidizi wa Sheria kuendelea kutoa Elimu kwa jamii kuhusu masuala mbali mbali ya kisheria ili waweze kuzifahamu sharia , Haki zao pamoja wajibu wao. Mdhamini huyo ameyasema hao katika hafla ya ufungaji wa mafunzo ya siku tatu juu ya kujadili mambo mbali mbali ya kimaendeleo   kwa wasaidizi wa sharia yaliofanyika   Gombani Chake chake Pemba. Alisema Wasaidizi wa Sheria wanadhima kubwa katika kuhakikisha jamii inapata uwelewa wa kutosha juu ya masuala mbali mbali ya kisheria pamoja na kufahamu haki zao stahiki. ‘’Ndugu zangu Wasaidizi wa Sheria nyinyi mnajukumu kubwa la kuhakikisha Jamii inazielewa Sheria, hivyo niwaombe tu muendelee kujitoa na kujituma ili kuona Wanachi wetu wanaishi kwa amani bila migogoro alieleza,’’. Alisema Wananchi waliowengi hawana uwelewa juu ya masula ya kisheria, hivyo ni jukumu la Wasaidizi wa Sheria

WANAFUNZI WATAKIWA KUVUNJA UKIMYA NA KUVIRIPOTI VITENDO VIOVU

Image
                                   NA SALIM HAMAD,PEMBA   WANAFUNZI wa Skuli za Mwambe za Dkt. Samia Suluhu Hassan Sekondari, Dk. Hussein Mwinyi Msingi na Mwambe Msingi wamehimizwa juu ya muhimu ya kutoa taarifa pale wanapokubwa na changamoto mbali mbali zikiwemo za viashiria vya vitendo vya kufanyiwa uzalilishaji wa kijinsia.   Wito huo umetolewa na Mratibu wa Chama cha Waandishi Wanawake Tanzania, Zanzibar (Tamwa)Fat-hiya Mussa Said wakati akiwasilisha mada juu ya Changamoto zinazowakabili watoto katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la Save the Children na kuwajumuisha wanafunzi wa Skuli hizo.   Alisema zipo changamoto nyingi zinazowakumba watoto ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia, kimwili, kingono, kutekelezwa na nyengine nyingi lakini watoto hao wamekuwa wakishindwa kuziripoti jambo ambalo husababisha wafanyaji kuendelea na vitendo hivyo wakitambua kuwa hawaulizwi.   Alisema watoto hao wanapaswa kuwaeleza wazazi wao, walimu, viongozi wa dini na watu wengine wa karibu kila

WAZIRI KADUARA ATOA MAGIZO KWA WIZARA YA KILIMO NA YA MAJI

Image
                       NA FATMA HAMAD, PEMBA WAZIRI wa Maji na Nishati Zanzibar   Shaib Hassan Kaduara   ameitaka wizara ya Kilimo kushirikiana na Wizara ya Maji kuhakikisha wanachimba Kisima katika eneyo la Chamanangwe pamoja na maeneo mengine, jambo ambalo litawasaidia wakulima kupata Maji na kuweza kuzalisha mazao kwa wingi. Waziri huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi pamoja na viongozi mbali mbali katika hafla ya   ufungaji wa siku ya Chakula duniani huko Chamanangwe   wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba alisema Maji ni moja ya chanjo kikubwa kinachotegemewa na wakulima wengi kwa ajili ya uzalishaji wa mazao. Alisema maji ndio msingi mkuu wa upatikanaji wa Chakula, hivyo ni wakati kwa wizara ya maji kuhakikisha wanasambaza maji katika maeneo mbali mbali na   wakulima waweze kuzalisha mazao mengi ili   kupatikana kwa chakula cha kutosha. ‘’Ni wakati kwa Mamlaka ya Maji pamoja na wizara ya   Kilimo kuchimba Kisima katika eneo la Chamanangwe na hata Vijijini k

WANCHI WA TUMBE WAPEWA USHAURI

Image
                             NA SALIM HAMAD,PEMBA WANANCHI wametakiwa kutoa mashirikiana kwa   Wasaidizi wa sheria ili waweze kuibua kero zinazowakumba wanajamii na kuweza kutatuliwa. Hayo yamezungumzwa na Msaidizi wa sharia shehiya ya Tumbe magharibi   Zaina Omar Othman wakati akizungumza na wananchi wa Tumbe   Raha kesho amesema kuna changamoto mbali mbali ambazo zimekuwa zikiwakumba wanajamii   ikiwemo masuala ya Udhalilishaji, na ya ndoa. Alisema endapo wanajamii watashirikiana na wasaidizi wa sheria kutasaidia kujulikana kwa kadhiya ambazo zimekuwa zikiwakumba wananchi na kuweza kuzisemea, ili kuona mamlaka husika zitakazo lalamikiwa zinachukuwa hatuwa. ‘’Ili kuona tunafikia lengo la kuondosha matatizo katika jamii ni vyema tuwe na mashirikiano ya pamoja baina yetu sisi wasaidizi wa sharia pamoja na wananchi,’’alisema. Kwa upande wake Msaidizi wa Sheria shehiya   ya Tumbe Mashariki Fatma Hamad ameitaka jamii kuwatumia wasaidizi wa sheria katika kueleza kero zao pamoja na m

WADAU WA HAKI ZA BINADAMU WATAKIWA KUONGEZA NGUVU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA VITENDO VYA UDHALILISHAJI

Image
                             NA SALIM HAMAD,PEMBA MKURUGENZI  wa Mashtaka Zanzibar, Mgeni Jailan Jecha amesema  bado kuna juhudi ndogo zinazochukuliwa na wadau katika  mapambano  ya vitendo vya udhalilishaji  kwani   baadhi yao huzisuluhisha kesi hizo kienyeji  jambo ambalo husababisha  kesi hizo  kupotea bila ya  kuchukuliwa hatua za kisheria.   Alisema bado wapo baadhi ya watendaji hao  hupatanisha kesi hizo Kiuenyeji ili zisiende mahakamani jambo ambalo linakwamisha juhudi za mapambano ya kesi hizo na kusababisha kuendelea kujitokeza Vitendo hivyo.   Mkurugenzi aliyasema  hayo  wakati akifungua  mafunzo elekezi juu ya kuchunguza na kuendesha kesi zinazohusiana na  udhalilishaji wa kijinsia  kwa wadau wa mapambano juu ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji ikiwa ni pamoja na waendesha mashtaka, madaktari,Maafisa na polisi  huko katika  ukumbi wa Makonyo Chake chake. Alisema sababu nyengine ni jamii kutotilia maanani katika mapambano ya vitendo vya udhalilishaji k