WANCHI WA TUMBE WAPEWA USHAURI
NA SALIM HAMAD,PEMBA
WANANCHI wametakiwa kutoa mashirikiana
kwa Wasaidizi wa sheria ili waweze kuibua
kero zinazowakumba wanajamii na kuweza kutatuliwa.
Hayo
yamezungumzwa na Msaidizi wa sharia shehiya ya Tumbe magharibi Zaina Omar Othman wakati akizungumza na
wananchi wa Tumbe Raha kesho amesema kuna
changamoto mbali mbali ambazo zimekuwa zikiwakumba wanajamii ikiwemo masuala ya Udhalilishaji, na ya ndoa.
Alisema endapo
wanajamii watashirikiana na wasaidizi wa sheria kutasaidia kujulikana kwa
kadhiya ambazo zimekuwa zikiwakumba wananchi na kuweza kuzisemea, ili kuona
mamlaka husika zitakazo lalamikiwa zinachukuwa hatuwa.
‘’Ili kuona
tunafikia lengo la kuondosha matatizo katika jamii ni vyema tuwe na
mashirikiano ya pamoja baina yetu sisi wasaidizi wa sharia pamoja na wananchi,’’alisema.
‘’Kama jamii mutawatumia ipasavyo wasaidiz wa sharia
katika kuwaelezea shida zenu, kutaepusha kutokea kwa mogogoro isiyo ya lazima,
na kuepuka kupelekana Mahamakamani kwa masuala madoggo madogo,’’alieleza.
Comments
Post a Comment