Posts

Showing posts from September, 2021

umasikini wapelekea Vilabu kushindwa kusaili na uhamisho wa wachezaji Kisiwani Pemba

Image
  SALIM HAMAD,PEMBA UKATA wa Kifedha unaovikabili Vilabu vya Madaraja mbali mbali Kisiwani Pemba,umesababisha Dirisha la usajili na uhamisho wa wachezaji kusuasua kutokana na baadhi ya Vilabu kushindwa kujitokeza katika Ofisi za Shirikisho la Soka (ZFF) Kisiwani hapa. Dirisha la Usajili na Uhamisho Visiwani Zanzibar limefunguliwa rasmi Septemba 21 ambapo litarajiwa kufungwa  Novemba 11. Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi  Katib Msadizi wa Shirikisho la Soka Kisiwani Pemba,Khamisi Hamad Juma alisema Zoezi la Usajili na uhamisho limekuwa gumu msimu huu kutokana na baadhi ya Vilabu kushindwa kuchukua fomu. Alisema moja ya sababu inayopelekea vilabu kutojitokeza kuchuka fomu za Usajili na wachezaji wanatka kuwasajili ni kutokana na ukata wa kifedha unaovikabili vilabu vya Pemba,jambo ambalo limepelekea zoezi hilo kusuasua. Alisema hadi sasa timu zilizojitokeza kuchuwa fomu kwa upande wa Primia ni timu ya Machomane United ambayo imechukua fomu 7 na timu ya Yoso Boys imechukua

RASIMU YA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MAFUTA NA GESI ASILIA YA ZANZIBAR ITAWEZA KUSAIDIA KUKUZA UCHUMI WA NCHI.

  SALIM HAMAD,PEMBA WADAU na Watendaji wa taasisi mbali mbali za Umma Kisiwani Pemba,wamesema iwapo rasimu ya marekebisho ya Sheria za mafuta na Gesi asilia ya Zanzibar itaweza kusadia kukuza maslahi ya Umma. Wakizingumza katika mkutano wa kujadili rasimu ya marekebisho ya Sheri za mafuta na gesi Asilia ya mwaka 2016 uliofanyika Gombani Chake chake Pemba wamesema itasadia kutatua changamoto kwa baadhi ya vifungu ambavyo vilikuwa vinajitokeza hapoawali. Akiwasilisha mada katika Mkutano huo Mwanasheria kutoka taasisiya ZPRA Omari Sururu Khalfani amefahamisha Vipengele vilivyofanyiwa marekebisho ikiwemo mkanganyiko watafsiri. Alisema tayari kwenye maeneo hayo walibaini kuna mapungufu na kuweza kuyafanyia marekebisho kuona mapungufu hayo yanaondoka. Afisa mdhamini Wizara ya Uchumi wa Bluu na Uvuvi Kisiwani Pemba,Dr Salum Mohd Hamza alisema lengo kuu la kuwakutanisha wadau mbali mbali ni kutafuta maoni juu ya marekebisho ya sheria za mafuta na gesi asilia. ‘’Tumefanya mkutano n

MAULID KHAMIS KASSIM NI MFANYABIASHARA MLEMAVU AOMBA MSAADA KWA WASAMARIA WEMA ILI AKUZE BIASHARA YAKE

Image
  Maulid Ali Kassim ambae ni Mlemavu wa viungo anaeishi Kijiji cha Wawi wilaya ya yake   chake   Mkoa wa Kusini Pemba aliyeamua kujishuhulisha na biashara ndogo ndogo kwa ajili ya kuondokana na   utegemezi na kujikwamua na umaskani wa kipato. Maulid mwenye   familia ya   watoto watano anasema kuwa   aliamua kuanzisha biashara zake ndogo ndogo mara baada ya kumaliza masomo yake ya lazima ya kidato cha 2 katika Skuli ya Sekondari Wawi kwa kuanzia na biashara ya malai, juice na biskuti za watoto kwa mtaji wa shilingi elfu arobaini. Kwa sasa Maulid anafanya biashara ya nguo za watoto huko Mjini Chake Chake   ambapo alianza na mtaji   wa shilingi laki mbili na hadi sasa   anasema mtaji wake unaweza kufika milioni moja. Ameeleza kuwa licha ya ulemavu wake alionao aliamua kujiajiri ili aepukane na omba omba, na utegemezi kwa watu wengine, huku akijua kuwa yeye anahitaji kuwa na mahitaji kama binadamu wote ikiwemo kuwa na mke na watoto.   ‘’Niliamua nijiajiri mwenyewe ili niepukane na

MASHEHA WATAKIWA KUTOA ELIMU KWA JAMII JUU UWEPO WA BARAZA LA KUMUWAKILISHA MTUMIAJI crc]

Image
  Masheha wa shehia mbali mbali kutoka wilaya ya Micheweni wametakiwa kuwa mabalozi wazuri   wa kuifikisha elimu juu ya kulijua na kulitumia baraza la kumuwakilisha mtumiaji wa huduma za maji na nishati katika shehia zao ili Wananchi waweze kufikisha kero zao katika baraza hilo. Hayo yameelezwa na Kaimu katibu Tawala wilaya ya Micheweni Kai Shaame Kai wakati akifungua mafunzo ya siku moja juu ya kulijua Baraza la kumuwakilisha mtumiaji wa huduma za maji a Niashati kwa masheha wa wilaya hiyo huko Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba.   Amesema Masheha wananafasi kubwa ya kuwafahamisha wanajamii juu ya matumizi ya huduma za maji na Nishati pamoja na kuwafahamisha uwepo wa baraza hilo kwa lengo la kufikisha changamoto zao . Akizungumzia juu ya uwepo wa Baraza hilo katibu mtendaji wa baraza   la kumuakilisha mtumiaji wa huduma za maji na Nishati [CRC ] Hadia Abdurahman Othman amesema lengo la kuwanzishwa chombo hicho ni kuwatetea watumiaji wa huduma hizo   katika kutatua kero zao na kuz

MAMA MWENYE WATOTO SITA WALEMAVU WA VIUNGO AOMBA MSAADA ILI AWEZE KUENDESHA MAISHA YA WATOTO WAKE

Image
JAMII imetakiwa kuwajali na kuwasaidia kupata mahitaji muhimu ikiwemo elimu, afya na mavazi Watoto wenye ulemavu wa akili  ili waondokane na dhana ya unyanyapaa .   Ushauri huo umetolewa na familia ya watoto wenye ulemavu wa viungo shehia ya Kinyasini Wilaya ya Wete Kisiwani Pemba baada ya watoto wao kushindwa kuendelea na masomo kutokana na ukali ya maisha.   Mama mazazi wa Watoto hao Mariam Ali Kombo amesema anashindwa kufanyakazi za maendeleo kutokana na changamoto zinazowakabili ikiwemo kufuata huduma ya maji.   “Nashindwa hata kufanya kazi kwa kuwalinda na kuwahudumia Watoto wangu, hivyo naomba yoyote mwenye uwezo anisaidie kuniunganishia maji pamoja na sabuni za kuoshea nguo”alisema.   Kwa upande wake Afisa  Idara ya watu Ulemavu Wilaya ya Wete Mohammed Mgau Said aliitaka jamii kushajishina na katika kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu kwani wanayofursa ya kupatiwa mahitaji ya msingi ikiwemo suala la elimu na kushirikishwa.   Amesema Pamoja na Watoto hawa kuwa na ulemav

WAFANYA KAZI WA KITENGO CHA ELIMU YA AFYA WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA JAMII KUTOA ELIMU ILI KUTOKOMEZA UGONJWA WA KIPINDU PINDU

Image
 Wafanyakazi wa kitengo cha kinga na elimu ya afya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wametakiwa kushirikiana kwa pamoja katika kuendeleza kinga ili kuondosha kabisa ugonjwa wa kipindupindu kisiwani Zanzibar. Akizungumza mratibu mkuu wa elimu ya afya Zanzibar Halima ali khamis wakati wa uwasilisho wa tafiti fupi iliyofanywa na kitengo hicho amesema matarajio ya serikali kupitia KOICA ni kumaliza maradhi hayo ifikapo 2027. Amengeza kuwa kutokana na mtarajio hayo zipo mbinu tofauti zinazochukuliwa na serikali kupitia mpango wa kupambana na kumaliza kipindupindu ikiwemo uhamasishaji wa uchimbaji wa vyoo na kuvitumia, upigaji wa chanjo na matumizi sahihi wa maji safi na salama mijini na vijijini. Kwa niaba ya afisi ya mufti pemba sheikh said ahmad mohammed amesema , hata dini imesisitiza juu ya kujikinga na maradhi mbalimbali hivyo hatuna budi kuhakikisha tunachukua hatua madhubuti katika hili. Ameongeza kuwa wao kama afisi ya mufti watahakikisha wanatumia fursa walioipata kwa lengo la k

KIJANA MOHD HAMAD WA KENGEJA MKOANI PEMBA BADO AENDELEA KUSOTA RUMANDE KWA TUHUMA ZA UBAKAJI

Image
  Kutokuwepo kwa Shahidi ambae ni askari mpelelezi kumemlazimu Hakimu wa mahakama ya Mkoa B’’ Lusiano Makoe Nyengo kughairisha kesi ya kuingilia kinyume na maumbile ambayo inamkabili   mtuhumiwa Ayoub Mohd Hamad mwenye umri wa miaka 18 mkaazi wa Kengeja Wilaya ya mkoani Pemba. Baada ya mtuhumiwa huyo kupanda kizimbani   wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka [DPP]   Ali Amour Makame amesema shauri hilo lipo kwa ajili ya kusikilizwa   na leo tulikua tunashahidi mmoja tu ambae ni askari mpelelezi ila hayupo mahakamani hapa. ‘’Mheshimiwa leo tulikua tunashahidi askari mpelelezi ila hayupo kwani yupo mafunzoni, hivyo tunaiomba mahakama yako uipangie tena siku nyengine kwa ajili ya kusikilizwa’’, Alisema DPP. Kwa upande wake Wakili   mtetezi anaesimamia kesi hiyo Zahrani Yussuf hakukubaliana na maelezo hayo yaliotolewa na wakili wa Serikali, kwamba shahidi hapatikani, hivyo ameiomba mahakama   itoe oda   kwa kuzingatia haki ya mshitakiwa kwani ameshakaa    rumande