KIJANA MOHD HAMAD WA KENGEJA MKOANI PEMBA BADO AENDELEA KUSOTA RUMANDE KWA TUHUMA ZA UBAKAJI


 

Kutokuwepo kwa Shahidi ambae ni askari mpelelezi kumemlazimu Hakimu wa mahakama ya Mkoa B’’ Lusiano Makoe Nyengo kughairisha kesi ya kuingilia kinyume na maumbile ambayo inamkabili  mtuhumiwa Ayoub Mohd Hamad mwenye umri wa miaka 18 mkaazi wa Kengeja Wilaya ya mkoani Pemba.

Baada ya mtuhumiwa huyo kupanda kizimbani  wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka [DPP]  Ali Amour Makame amesema shauri hilo lipo kwa ajili ya kusikilizwa  na leo tulikua tunashahidi mmoja tu ambae ni askari mpelelezi ila hayupo mahakamani hapa.

‘’Mheshimiwa leo tulikua tunashahidi askari mpelelezi ila hayupo kwani yupo mafunzoni, hivyo tunaiomba mahakama yako uipangie tena siku nyengine kwa ajili ya kusikilizwa’’, Alisema DPP.

Kwa upande wake Wakili  mtetezi anaesimamia kesi hiyo Zahrani Yussuf hakukubaliana na maelezo hayo yaliotolewa na wakili wa Serikali, kwamba shahidi hapatikani, hivyo ameiomba mahakama  itoe oda  kwa kuzingatia haki ya mshitakiwa kwani ameshakaa   rumande  kwa muda mrefu.

‘’Mheshimiwa tunaomba mahakama yako itoe oda,  na lazima tuangalie pande zote mbili,  hivyo tukiendelea tuu shahidi hapatikani  tunamuumiza mtuhumiwa, Alisema wakili mtetez’’.

Hakimu wa mahakama hiyo Lusiano Makoe Nyengo hakukubaliana na ombi la wakili mtetezi na kesi itaendelea tena tarehe 14/9/mwaka huu. Imedaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo siku ya tarehe 23/2/2021 majira ya 5;30 asubuhi, huko Likoni Kengeja wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba Alimuingilia kinyume na maumbile ambapo kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifu cha 133 [a] cha sheria ya adhabu sheria nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.