Posts

Showing posts from November, 2023

TATIZO LA MAJI LILILOKUWA LINAIKABILI KITUO CHA AFYA WESHA SASA LAPATA UFUMBUZI

Image
                            NA FATMA HAMAD, PEMBA Septemba 21 mwaka huu Blog ya Pemba ya leo iliibua changamoto ya kukosekana kwa huduma ya Maji safi na salama katika kituo cha Afya cha Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, ambapo kilio hicho kimepatiwa ufumbuzi kwa sasa. Wakizungumza na mwandishi wa habari huko kituo cha afya wesha Safinia Said na Rukia Khamis ambao ni wajawazito waliokwenda kupata huduma kituoni hapo walisema zaid ya miezi 3 kulikuwa hakuna maji kituoni hapo.   Walisema kwa sasa shida ya Maji imepungua kwani Maji yanapatikana ijapokuwa hayatoki siku zote ni kwa mgao. ''kwa sasa hatuendi na madumu ya Maji tunapokwenda kujifungua kwani Maji ya zawa ikifika zamu ya kutoka huwa yanapatikana hapa kituoni,, walisema Hivyo tunaiomba Wizara ya Maji iyongeze juhudi ili kuona Maji yanapatikana masa yote 24 kwani suala la uzazi ni kitu cha kila siku jambo ambalo litaondosha usumbufu kwa mama wajawazito pamoja na wazazi wanaokwenda kujifungulia kituoni hapo. Kwa u

WATU WENYE ULEMAVU WAIOMBA SERIKALI KUONDOSHA VIKWAZO KWENYE MIKOPO.

Image
                                            NA FATMA HAMAD,PEMBA VIKUNDI vya Ushirika vya Watu wenye ulemavu Kisiwani Pemba vimeiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwaondeshea vikwazo kwenye suala la upatikanaji wa Mikopo inayotolewa kwa ajili ya kuwawezesha Wananchi kiuchumi ili kuona watu wenye ulemavu nawao wananufaika na fursa hiyo. Hayo yamesemwa na Omar Kombo Hamad kutoka kikundi cha Twamshukuru Allah kilichopo   mbuzini na Fatma Salim Hamud wa kikundi cha Nia njema   kutoka Ole kianga cha watu wenye ulemavu mara baada ya kumaliza mafunzo ya ya utengenezaji wa bidhaa mbali mbali ikiwemo Mafuta ya mgando ya mwani, mafuta ya mkaratusi pamoja na Jiki huko Ole mihogoni Chake chake Pemba.   Walisema ili kuona watu wenye ulemavu wananufaika na fursa mbali mbali zilizomo kwenye Serikali, nivyema   kupatiwa mkopo   kwa mtu mmoja mmoja   na isiwe lazima wawepo kwenye Vikundi vya ushirika. ‘’Watu wengine wenye ulemavu hawawezi kuingiza Pesa[akiba] mule kwenye hisa kwani wengi haw

SERIKALI ITAENDELEA KUJENGA HOSPITALI, KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA

Image
                                              NA ZUHURA JUMA, PEMBA   RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendelea kujenga hospitali na vituo vya afya vyenye vifaa vya kisasa ili kuwapatia huduma bora za afya wananchi wake.   Akizungumza wakati akifungua hospitali ya Wilaya iliyopo Kinyasini Wilaya ya Wete, Dk. Mwinyi alisema tayari zimeshajengwa hospitali  za Wilaya kwa unguja na Pemba huku Serikali ikiendelea kujenga hospitali za mikoa, rufaa na mwanzo (dispensaries na vituo vya afya) ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya bila ya usumbufu.   Alisema kuwa, ujenzi wa hospitali hizo na vituo vya afya vitawapunguzia wananchi kwenda masafa marefu kuifuata huduma hiyo, sambamba ya kupata huduma bora kutokana na vifaa vya kisasa vilivyowekwa.   "Tutahakikisha tunasogeza huduma bora za afya kwa wananchi, ili wawe na afya njema na sehemu ambazo bado hatujajenga basi wananchi wawe na imani kwani

Dk. Mwinyi ataka usafi kwenye miji uimarike

Image
NA ZUHURA JUMA, PEMBA RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi amezitaka Halmashauri, Mabaraza ya Miji na Manispaa kudumisha usafi katika miji, ili kuiweka katika mazingira bora na haiba ya kuvutia.   kizungumza wakati akifungua kituo cha wajasiriamali Kifumbikai Wete pamoja na stendi ya Kinowe Konde Dk. Mwinyi aliziagiza taasisi hizo mambo matano, ikiwa ni pamoja na kufanya usafi katika miji, kujenga masoko, vituo vya ujasiriamali, maegesho na viwanja vya kufurahishia watoto ambayo hayo yatasaidia kuweka mazingira bora na mazuri.   Alisema kuwa, usafi ni muhimu katika maisha ya mwanadamu, hivyo ni wajibu wao kudumisha katika maeneo ya miji, kwa ajili ya kuweka mandhari nzuri na ya kuvutia.   "Tumebadilisha ugatuzi ili taasisi hizi ziweze kufanya kazi zake vizuri ikiwa ni pamoja na suala la kuimarisha usafi katika miji yetu, hivyo mna wajibu wa kuyatekeleza kwa vitendo ili kuimarisha maisha ya wananchi," alisema Rais Mwinyi.   Aidha

WAKULIMA WA MWANI WAHIMIZWA KULIMA KILIMO CHA KISASA

Image
                                                           NA FATMA HAMAD,PEMBA   Wakulima wa mwani wametakiwa kulima kilimo cha kisasa ili waweze kuzalisha zao hilo kwa wingi.   Ushauri huo umetolewa na Afisa Mazimgira kutoka idara ya mazimgira na Ofisi ya makamo wa kwanza wa Rais  Hassan Hamad Hassan wakati akizunumza na wanavikundi vya ulimaji wa mwani huko kilindi Chake chake  Pemba.   Amesema Sera ya Serikali ya Uchumi wa buluu ni kuhakikisha inawainua wakulima wa mazao ya baharini ili waondokane na umaskini.   Hivyo alisema ni wakati kwa Wakulima wa Mwani kuondokana na kilimo cha zamani, na badala yake walime kilimo cha kisasa (walime kwa ajili ya biashara) jambo ambalo litawawezesha kuvuna zao hilo kwa wingi na kujipatia  kipato.   "Niwaombe Wakulima mbadilike msilime kimazoe, mlime kilimo cha kisasa na mlime Mwani kwa ajili ya biashara, msilime panatosha,"alisema.   Sheha wa Shehiya ya kilindi   Nassor Muhammed Khamis aliwataka wakulima hao waliopatiwa maf

BARAZA LA USHINDANI HALALI WA BIASHARA MUARUBAINI KWA WADAU WA BIASHARA

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA Afisa   Mdhamini wizara ya Biashara na Viwanda kisiwani Pemba Ali Suleiman Abeid amewataka wadau wa biashara kuitumia fursa ya kupata huduma katika Baraza la Ushindani Halali wa Biashara ili waweze kupata majibu sahihi  na  kwa wakati muafaka dhidi ya mashauri yao mbali mbali yanayohusiana na biashara. Afisa huyo ameyasema hayo wakati akifunguwa kongamano la kuwajengea uwelewa Masheha wa Chake chake na Mafisa Wandamizi wa Mamlaka za Udhibiti kulifahamu baraza la ushindani halali wa Biashara huko Tibirinzi kisiwani Pemba. Amesema uwepo wa Baraza hilo la Ushindani halali wa Biashara kunakisi azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya dhamira yake ya kuweka mfumo thabiti wa kusimamia na kuimarisha mazingira  rafiki ya biashara na uwekezaji Nchini. Alisema  ni vyema Masheha kuwaelimisha wadau wa biashara  pamoja na watumiaji ili wawe na ulewa wa hali ya juu na kuona wanalitumia Baraza hilo pale ambapo hawakuridhika na mamuzi yaliyotolewa na Mamlaka za udhibi