BARAZA LA USHINDANI HALALI WA BIASHARA MUARUBAINI KWA WADAU WA BIASHARA
Afisa huyo
ameyasema hayo wakati akifunguwa kongamano la kuwajengea uwelewa Masheha wa
Chake chake na Mafisa Wandamizi wa Mamlaka za Udhibiti kulifahamu baraza la
ushindani halali wa Biashara huko Tibirinzi kisiwani Pemba.
Amesema uwepo wa Baraza hilo la Ushindani halali wa Biashara kunakisi azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya dhamira yake ya kuweka mfumo thabiti wa kusimamia na kuimarisha mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji Nchini.
Alisema ni vyema
Masheha kuwaelimisha wadau wa biashara
pamoja na watumiaji ili wawe na ulewa wa hali ya juu na kuona
wanalitumia Baraza hilo pale ambapo hawakuridhika na mamuzi yaliyotolewa na
Mamlaka za udhibiti.
‘’Nyinyi Masheha mnanafasi
kubwa katika Jamii hivyo ni vyema kutoa Elimu kwa Wafanyabiashara na watumiaji
ili kuona wanalitumia Baraza hilo kwa kupeleka kero zao,’’ alisema.
Nao baadhi
ya washiriki wa Kongamano hilo wameushukuru Uongozi wa baraza Halali la
Ushindani wa Biashara kwa kuwapatia elimu hiyo, hivyo wameahidi kuifanyia kazi
ili kuona wafanyabiashara wanafanya biashara zao kwa mujibu wa sheria namba 5
ya mwaka 2018 kama ilivyoelekeza.
Comments
Post a Comment