WATU WENYE ULEMAVU WAIOMBA SERIKALI KUONDOSHA VIKWAZO KWENYE MIKOPO.


                                           NA FATMA HAMAD,PEMBA

VIKUNDI vya Ushirika vya Watu wenye ulemavu Kisiwani Pemba vimeiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwaondeshea vikwazo kwenye suala la upatikanaji wa Mikopo inayotolewa kwa ajili ya kuwawezesha Wananchi kiuchumi ili kuona watu wenye ulemavu nawao wananufaika na fursa hiyo.

Hayo yamesemwa na Omar Kombo Hamad kutoka kikundi cha Twamshukuru Allah kilichopo  mbuzini na Fatma Salim Hamud wa kikundi cha Nia njema  kutoka Ole kianga cha watu wenye ulemavu mara baada ya kumaliza mafunzo ya ya utengenezaji wa bidhaa mbali mbali ikiwemo Mafuta ya mgando ya mwani, mafuta ya mkaratusi pamoja na Jiki huko Ole mihogoni Chake chake Pemba.

 Walisema ili kuona watu wenye ulemavu wananufaika na fursa mbali mbali zilizomo kwenye Serikali, nivyema  kupatiwa mkopo  kwa mtu mmoja mmoja  na isiwe lazima wawepo kwenye Vikundi vya ushirika.

‘’Watu wengine wenye ulemavu hawawezi kuingiza Pesa[akiba] mule kwenye hisa kwani wengi hawana kazi ya kufanya mpaka tuwape sisi wazazi wao, hivyo tunaiomba Serikali  iangalie tena kwa jicho la pili  kwani masharti ya mkopo wawe kwenye kikundi ni shida kwa watu hawa,’’ walisema.

Walisema ni vyema Serikali kuwapatia posho  kila  mwisho wa mwezi kama vile Pencheni ya Wazee ili iweze kuwasaidia katika maisha yao .

Samba mba na hilo wameiomba Serikali kuwapa kipaombele watu wenye ulemavu katika Sekta mbali mbali ikiwemo ajira ili kuona nawao wanashika nyadhifa na kupata fursa zilizomo kwenye Serikali yao.

Mauwa ali Hamad wa kikundi cha Subira yavuta kheri cha Mvumoni  na  Chake chake alisema mafunzo hayo ya utengenezaji wa bidha hizo yamewafumbuwa macho, hivyo ameahidi kuyafanyia kazi ili kuona wanafanya biashara hizo jambo ambalo litaendesha kikundi chao pamoja na kujipatia kipato.

Naimu Abdala Ali kutoka kikundi cha mwisho mwema kilichopo Mabaoni Chake chake ameutaka  uongozi wa (TAMWA) kupitia mradi wake wa Kijaluba kuendelea kutoa mafunzo ya utengenezaji wa bidhaa mbali mbali kwani kutainua zaidi kipato cha watu wenye ulemavu kisiwani humo.

Nae Afisa mradi wa Kijaluba kutoka Chama cha Wandishi wa Hbari Wanawake Tanzania Tamwa Ofisi ya Pemba Muhamed Salim Khamis alisema lengo la kutoa mafunzo hayo kwa  Vikundi vya watu wenye ulemavu ni kuwawezesha watu hao kiuchumi na waweze kujikwamua na umasikini uliokithiri.

Alisema watu wenye ulemavu wamekuwa wakisahauliwa katika fursa mbali mbali za kimaendeleo, hivyo wameamua kuleta mradi huu ili kuona nwao wanashiriki katika nyanja mbali mbali mbali jambo ambalo litawafanya nawao waisha katika maisha mazuri kama watu wengine wasio na ulemavu.

‘’Tuliona miradi mingi inayoletwa na Serikali pamoja na mashirika binafsi imekuwa ikiwacha nyuma watu wenye ulemavu, hivyo tumeleta mradi huu wa kijaluba na kuwapatia mafunzo ya utengenezaji wa vitu mbali li  ili kuwapunguzia hali ngumu za kimaisha,’’ alieleza.

Jumla ya vikundi 23 vya watu wenye ulemavu kutoka wilaya ya Chake chake vimepatiwa mafunzo hayo yaliondaliwa na Chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanziba( TAMWA ) kupitia mradi wake wa kijaluba  ambao unaendeshwa na Tamwa pamoja na Shirikisho la Jumuia za watu wenye ulemavu Zanzibar (Shijuwaza) chini ya ufadhili wa Jumuia ya watu wenye ulemavu  (NADI) kutoka NORWAY.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.